Novatus
JF-Expert Member
- Jul 28, 2007
- 330
- 37
Saccos ni njia sahihi ya kumwokoa mjasiriamali wa kawaida. Mpango huu wa kuweka na kukopa unasaidia sana sana watu walio wengi.
saccos zilianzishwa nyingi lakini siku hadi siku zinakufa. Wanahisa walio wengi hawaelewi ni kwa nini zife wakati zinapoanzishwa zinakuwa na gawio linakuwa kubwa.
utafiti niliofanya katika Saccos zaidi ya tatu ni kuwa kifo cha ushirika huu kinaanza ambabo Benki zinaingilia SAccos hizi kama wadhamini au kuwaongezea mtaji. Kwanza kwakuwa Benki zinawekeza pesa nyingi kuliko ya wanachama wanalazimisha Saccos ziendeashwe na Wataalamu waliosomea Ushirika/uhasibu. Sina pingamizi na hili. ILA sasa Benki ndio wanaoajiri wafanyakazi hawa ambao wanajifanya ni waelewa waliobobea na zaidi ajira zinaenda kiundugu wala sio sifa halisi. matokeo yake wanaongeza mzigo wa gharama za uendeshaji, wengine wanakiuka misingi na kanuni zilizowekwa katika kukopesha na kurejesha. Wengine wananakiuka taratibu wanajikopesha mikopo mikubwa kama taasisi nyingine eti watakatwa kwenye mishahara.
Matokeo yake unakuta wanahisa baada ya mwaka wanaambiwa hakuna gawio. Iweje taasisi ikae na fedha yako millioni kumi isizae wakati imekuwa ikopeshwa? Jambo hili linawakatisha tamaa watu na kukosesha imani kwenye saccos
Ni wakati muafaka serikali iingilie kati kutatua jambohili au wanahisa wategemee pesa yao wakopeshane wasimamie wenyewe wataona faida ya ushirika huu
WanaJF tafadhali changia mada hii kwa faida ya watanzania
saccos zilianzishwa nyingi lakini siku hadi siku zinakufa. Wanahisa walio wengi hawaelewi ni kwa nini zife wakati zinapoanzishwa zinakuwa na gawio linakuwa kubwa.
utafiti niliofanya katika Saccos zaidi ya tatu ni kuwa kifo cha ushirika huu kinaanza ambabo Benki zinaingilia SAccos hizi kama wadhamini au kuwaongezea mtaji. Kwanza kwakuwa Benki zinawekeza pesa nyingi kuliko ya wanachama wanalazimisha Saccos ziendeashwe na Wataalamu waliosomea Ushirika/uhasibu. Sina pingamizi na hili. ILA sasa Benki ndio wanaoajiri wafanyakazi hawa ambao wanajifanya ni waelewa waliobobea na zaidi ajira zinaenda kiundugu wala sio sifa halisi. matokeo yake wanaongeza mzigo wa gharama za uendeshaji, wengine wanakiuka misingi na kanuni zilizowekwa katika kukopesha na kurejesha. Wengine wananakiuka taratibu wanajikopesha mikopo mikubwa kama taasisi nyingine eti watakatwa kwenye mishahara.
Matokeo yake unakuta wanahisa baada ya mwaka wanaambiwa hakuna gawio. Iweje taasisi ikae na fedha yako millioni kumi isizae wakati imekuwa ikopeshwa? Jambo hili linawakatisha tamaa watu na kukosesha imani kwenye saccos
Ni wakati muafaka serikali iingilie kati kutatua jambohili au wanahisa wategemee pesa yao wakopeshane wasimamie wenyewe wataona faida ya ushirika huu
WanaJF tafadhali changia mada hii kwa faida ya watanzania