Kisa cha punda na mkulima

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,606
696,724
Mkulima mmoja alikuwa na Punda ...Punda aliyedumu nae kwa miaka mingi sana aliyemsaidia shughuli za kilimo na uchukuzi..alikaa naye toka akiwa mtoto mpaka punda akawa mzee kabisa.
Siku moja wakiwa wanatoka shambani, kwa bahati mbaya yule punda alitumbukia kwenye kisima kirefu sana ambacho kwa wakati ule kilikuwa kimekauka.
Yule Mkulima akawaza sana atafanyaje kumtoa yule punda..na baada ya kutafakari sana akasema kwanza hata hivyo huyu punda ameshazeeka ni hasara kuingia gharama za kumtoa...akaona vema tu amzike humo humo
Akaenda kuita majirani ,wakaja na sepetu wakaanza kumwagia udongo ,mchaka na kokoto shimoni kumfukia.
Mwanzoni tu ni kama punda alijua kinachoendelea..akapaza sauti na kulia kwa sauti kali ajabu..sauti ya malalamiko...hawakujali waliendelea kufukia..kwa kutupia kila aina ya taka taka
Baadae kidogo kwa mshangao wa wengi ghafla punda alinyamaza kimya kabisa sauti ikapotea....baada ya kutupia taka kadhaa..mkulima yule akaamua kuchungulia shimoni....Alistushwa mno na alichokiona
Kila taka na mchanga ulipokuwa ukiangukia mgongoni mwa punda...alikuwa akifanya kitu cha kushangaza.
Kila udongo ulipomwangukia..alijitingisha ukamwagika na akaukanyaga akainuka juu kidogo...kila ulipokuja aliendelea kufanya hivyo hivyo..hatimaye baada ya Muda mkulima na majirani walishangaa kuona amefika juu kabisa ya ukingo wa kisima na akatoka kwa furaha kabisaa.
Kuna wakati maisha yanakurushia matakataka ya kila aina,acha kulia na kupiga kelele, jitingishe...yafanye ngazi..Kila jaribu linalotupata ni ngazi ya kupandia.
Kamwe hatuwezi toka kwenye visima virefu kwa kulia peke yake..bali kwa kupambana kuchomoka.
Wacha waone uko kimya baada ya makombora waliokurushia...yatake yapange..yafanye ngazi ya kupandia...
Changamoto yeyote unayopitia sasa...ni shimo na michanga..sisi ni zaidi ya punda..acha kulia, jikung`ute, yakanyage ,nyanyuka juu, toka Kanyaga Twende

Jr
 
Mkulima mmoja alikuwa na Punda ...Punda aliyedumu nae kwa miaka mingi sana aliyemsaidia shughuli za kilimo na uchukuzi..alikaa naye toka akiwa mtoto mpaka punda akawa mzee kabisa.
Siku moja wakiwa wanatoka shambani, kwa bahati mbaya yule punda alitumbukia kwenye kisima kirefu sana ambacho kwa wakati ule kilikuwa kimekauka.
Yule Mkulima akawaza sana atafanyaje kumtoa yule punda..na baada ya kutafakari sana akasema kwanza hata hivyo huyu punda ameshazeeka ni hasara kuingia gharama za kumtoa...akaona vema tu amzike humo humo
Akaenda kuita majirani ,wakaja na sepetu wakaanza kumwagia udongo ,mchaka na kokoto shimoni kumfukia.
Mwanzoni tu ni kama punda alijua kinachoendelea..akapaza sauti na kulia kwa sauti kali ajabu..sauti ya malalamiko...hawakujali waliendelea kufukia..kwa kutupia kila aina ya taka taka
Baadae kidogo kwa mshangao wa wengi ghafla punda alinyamaza kimya kabisa sauti ikapotea....baada ya kutupia taka kadhaa..mkulima yule akaamua kuchungulia shimoni....Alistushwa mno na alichokiona
Kila taka na mchanga ulipokuwa ukiangukia mgongoni mwa punda...alikuwa akifanya kitu cha kushangaza.
Kila udongo ulipomwangukia..alijitingisha ukamwagika na akaukanyaga akainuka juu kidogo...kila ulipokuja aliendelea kufanya hivyo hivyo..hatimaye baada ya Muda mkulima na majirani walishangaa kuona amefika juu kabisa ya ukingo wa kisima na akatoka kwa furaha kabisaa.
Kuna wakati maisha yanakurushia matakataka ya kila aina,acha kulia na kupiga kelele, jitingishe...yafanye ngazi..Kila jaribu linalotupata ni ngazi ya kupandia.
Kamwe hatuwezi toka kwenye visima virefu kwa kulia peke yake..bali kwa kupambana kuchomoka.
Wacha waone uko kimya baada ya makombora waliokurushia...yatake yapange..yafanye ngazi ya kupandia...
Changamoto yeyote unayopitia sasa...ni shimo na michanga..sisi ni zaidi ya punda..acha kulia, jikung`ute, yakanyage ,nyanyuka juu, toka Kanyaga Twende

Jr
maneno ya msingi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshana Jr na bandiko lenye hekima.Usichoke mkuu kuleta mabandiko yenye mafunzo humu jamvini.Salute comrad.
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom