Shemasi Jimmy
Member
- Apr 23, 2021
- 93
- 104
KISA CHA NABII MZEE NA NABII KIJANA JINSI KINAVYOWEZA KUIMARISHA IMANI YAKO
Na Shemasi Jimmy 0659611 252
Awali ya yote nawasalimu kwa Jina kuu kupita majina yote; Bwana Yesu apewe sifa.
Ungana nami shemasi wako katika simulizi hii nzuri inayopatikana katika kitabu cha 1fal 13:1-34, huku tukitazama jinsi simulizi hii inavyoweza kuimarisha imani na tumaini tulionalo ndani ya mioyo yetu.
Ikiwa baada ya mgawanyiko wa makabila 12 ya wana wa Israeli(Israeli na yuda), mfalme Yerobohamu wa Israeli ya kaskazini alianza kufanya chukizo mbele za Mungu. Na hivyo Mungu akaamua kumtuma mjumbe wake(nabii kijana) kwa lengo la kumuonya mfalme ili aache uovu. Baada ya kufika na kumuonya mfalme Yerobohamu ambae alikua kwenye madhabahu ya miungu akitoa dhabihu na kufukiza uvumba, mfalme Yerobohamu alinyoosha mkono wake akiamuru walinzi wamkamate mara moja nabii huyo, mara ghafla mkono wa mfalme Yerobohamu ukakatika na kudondoka chini. Mfalme yerobohamu akamuomba nabii kijana akimsihi amuombe Mungu wake ili amrudishie tena mkono wake. Yule nabii akaomba na mkono ukarejea tena kama awali.
Mfalme Yerobohamu akamwalika nabii Yule ili wapate kula na kunywa pamoja kama sehemu ya shukurani yake kwa mtu huyo wa Mungu. Nabii kijana akakataa mwaliko ule akimueleza kua Bwana amemuamuru asile wala kunywa tena asirudi kwa njia aliotumia kufika mahali pale. Nabii Yule akaondoka na njia nyingine kama alivyoagizwa na Bwana.
Kumbe wakati nabii Yule kijana akinena kufanya yote yale mbele ya mfalme,kulikuepo watoto waliosikia na kuona yote yaliotendeka kwa mfalme. Watoto hao walipeleka habari kwa baba yao(nabii mzee). Yule nabii mzee akamfuata na kumlaghai mtu wa Mungu, akimkaribisha chakula na vinywaji nyumbani kwake lakini mtu Yule wa Mungu(nabii kijana) akamweleza ukweli jinsi neno Mungu alivyomzuia kula wala kunywa tena asirudi kwa njia aliyopita awali.
Nabii mzee akamlaghai kwa kumwambia kua mimi ni nabii wa Bwana kama wewe, Bwana ameniambia nikwambie tuambatane pamoja hadi nyumbani kwangu, ule na kunywa pamoja name. walakini nabii huyo alikua muongo. Nabii kijana akamwamini nabii mzee akafanya kama alivyoambiwa na nabii huyo, kinyume na neno la Bwana. Akala na kunywa nyumbani kwa nabii mzee, akarudi kwa njia aliyopita awali kinyume na agizo la Bwana. Ndipo neno la Bwana likamjia nabii mzee, akamwambia nabii kijana huku akilia kua Bwana amesema hakika atakufa kwa kua amekiuka agizo la Bwana.
TUNAPATA FUNZO GANI
1)USIAMINI KILA ROHO INAYOKUJIA BALI ICHUNGUZE KWANZA.(1 YOH 4:1, MIT 14:15). Nabii kijana ni mfano wa wakristo wengi tunaoamini kila roho pasipo kuichunguza. Nabii kijana alikua na nafasi ya kumuuliza Mungu yale aliyoambiwa na nabii mzee akini hakufanya hivyo. Tujenge tabia ya kusoma neon la Mungu ili tupata uwezo wa kupima roho zote zituijiazo. Mfano huu hauna tofauti na jinsi shetani alivyomlaghai Hawa katika mwanzo3:4 kinyume na agizo la Mungu katika mwanzo 2:17. Mkristo kua makini tupo katika nyakati za mwisho.
Je, wewe umejifunza nini kupitia simulizi hii.
Na Shemasi Jimmy 0659611 252
Awali ya yote nawasalimu kwa Jina kuu kupita majina yote; Bwana Yesu apewe sifa.
Ungana nami shemasi wako katika simulizi hii nzuri inayopatikana katika kitabu cha 1fal 13:1-34, huku tukitazama jinsi simulizi hii inavyoweza kuimarisha imani na tumaini tulionalo ndani ya mioyo yetu.
Ikiwa baada ya mgawanyiko wa makabila 12 ya wana wa Israeli(Israeli na yuda), mfalme Yerobohamu wa Israeli ya kaskazini alianza kufanya chukizo mbele za Mungu. Na hivyo Mungu akaamua kumtuma mjumbe wake(nabii kijana) kwa lengo la kumuonya mfalme ili aache uovu. Baada ya kufika na kumuonya mfalme Yerobohamu ambae alikua kwenye madhabahu ya miungu akitoa dhabihu na kufukiza uvumba, mfalme Yerobohamu alinyoosha mkono wake akiamuru walinzi wamkamate mara moja nabii huyo, mara ghafla mkono wa mfalme Yerobohamu ukakatika na kudondoka chini. Mfalme yerobohamu akamuomba nabii kijana akimsihi amuombe Mungu wake ili amrudishie tena mkono wake. Yule nabii akaomba na mkono ukarejea tena kama awali.
Mfalme Yerobohamu akamwalika nabii Yule ili wapate kula na kunywa pamoja kama sehemu ya shukurani yake kwa mtu huyo wa Mungu. Nabii kijana akakataa mwaliko ule akimueleza kua Bwana amemuamuru asile wala kunywa tena asirudi kwa njia aliotumia kufika mahali pale. Nabii Yule akaondoka na njia nyingine kama alivyoagizwa na Bwana.
Kumbe wakati nabii Yule kijana akinena kufanya yote yale mbele ya mfalme,kulikuepo watoto waliosikia na kuona yote yaliotendeka kwa mfalme. Watoto hao walipeleka habari kwa baba yao(nabii mzee). Yule nabii mzee akamfuata na kumlaghai mtu wa Mungu, akimkaribisha chakula na vinywaji nyumbani kwake lakini mtu Yule wa Mungu(nabii kijana) akamweleza ukweli jinsi neno Mungu alivyomzuia kula wala kunywa tena asirudi kwa njia aliyopita awali.
Nabii mzee akamlaghai kwa kumwambia kua mimi ni nabii wa Bwana kama wewe, Bwana ameniambia nikwambie tuambatane pamoja hadi nyumbani kwangu, ule na kunywa pamoja name. walakini nabii huyo alikua muongo. Nabii kijana akamwamini nabii mzee akafanya kama alivyoambiwa na nabii huyo, kinyume na neno la Bwana. Akala na kunywa nyumbani kwa nabii mzee, akarudi kwa njia aliyopita awali kinyume na agizo la Bwana. Ndipo neno la Bwana likamjia nabii mzee, akamwambia nabii kijana huku akilia kua Bwana amesema hakika atakufa kwa kua amekiuka agizo la Bwana.
TUNAPATA FUNZO GANI
1)USIAMINI KILA ROHO INAYOKUJIA BALI ICHUNGUZE KWANZA.(1 YOH 4:1, MIT 14:15). Nabii kijana ni mfano wa wakristo wengi tunaoamini kila roho pasipo kuichunguza. Nabii kijana alikua na nafasi ya kumuuliza Mungu yale aliyoambiwa na nabii mzee akini hakufanya hivyo. Tujenge tabia ya kusoma neon la Mungu ili tupata uwezo wa kupima roho zote zituijiazo. Mfano huu hauna tofauti na jinsi shetani alivyomlaghai Hawa katika mwanzo3:4 kinyume na agizo la Mungu katika mwanzo 2:17. Mkristo kua makini tupo katika nyakati za mwisho.
Je, wewe umejifunza nini kupitia simulizi hii.