Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,500
Jamani hii imenikuta mimi mwenyewe last week nikiwa nasimamia arusi ya jamaa mmoja ambaye mkewe ni rafiki sana na mke wangu na wamesoma pamoja.
Arusi imefanyika katika ukumbi mmoja Sinza na mimi na mke wangu ndio tulikuwa wasimamizi kwa wanafamilia hawa wapya. Ilipofika wakati wa chakula, bibi arusi na matron wake (my wife) waliitana kando kuteta huku bibi harusi akionekana kupoteza uchangamfu kidogo.
Baada ya muda si mrefu, walirejea tulipokuwa na mazungumzo ya hapa na pale yaliendelea. Kisha wife wangu akaniita chemba kidogo akaanza kunieleza kwamba Bibi harusi yupo katika sintofahamu kubwa.
Kisa na mkasa wa sintofahamu hiyo ni kwamba bibi harusi hajawahi kufanya mapenzi hata siku moja na yeye ni bikira. Kipindi chote walichokuwa katika uchumba hawakuwahi kufanya mapenzi na mchumbake ambaye sasa wameunganishwa na kuwa mumewe. wasiwasi alionao ni kwamba anajua siku hiyo atapata uchungu mkubwa kwani atafanya mapenzi kwa mara ya kwanza katika maisha yake.
Uchangamfu ulimpotea kutokana na kuwazia sana hilo tendo ambalo anaamili lazima litamletea maumivu makali na hata kutoka damu. Wife akanishauri kuwa nijaribu kuzungumza na Bw Arusi ili awe na na subira katika kufanya tendo hilo usiku huo katika hoteli watakakokwenda kulala ili kmwenzake asipate maumivu.
Hii sio hadithi wakuu, imenitokea mimi mwenyewe nikisimamia arusi hii na ukweli nilipigwa na butwaa kwani ni nadra sana kukuta hadi siku ya arusi mtu bado bikra hasa Dar es salaam yetu hii.
Ungekuwa wewe ungemweleza nini Bwana Harusi katika scenario hiyo?
Arusi imefanyika katika ukumbi mmoja Sinza na mimi na mke wangu ndio tulikuwa wasimamizi kwa wanafamilia hawa wapya. Ilipofika wakati wa chakula, bibi arusi na matron wake (my wife) waliitana kando kuteta huku bibi harusi akionekana kupoteza uchangamfu kidogo.
Baada ya muda si mrefu, walirejea tulipokuwa na mazungumzo ya hapa na pale yaliendelea. Kisha wife wangu akaniita chemba kidogo akaanza kunieleza kwamba Bibi harusi yupo katika sintofahamu kubwa.
Kisa na mkasa wa sintofahamu hiyo ni kwamba bibi harusi hajawahi kufanya mapenzi hata siku moja na yeye ni bikira. Kipindi chote walichokuwa katika uchumba hawakuwahi kufanya mapenzi na mchumbake ambaye sasa wameunganishwa na kuwa mumewe. wasiwasi alionao ni kwamba anajua siku hiyo atapata uchungu mkubwa kwani atafanya mapenzi kwa mara ya kwanza katika maisha yake.
Uchangamfu ulimpotea kutokana na kuwazia sana hilo tendo ambalo anaamili lazima litamletea maumivu makali na hata kutoka damu. Wife akanishauri kuwa nijaribu kuzungumza na Bw Arusi ili awe na na subira katika kufanya tendo hilo usiku huo katika hoteli watakakokwenda kulala ili kmwenzake asipate maumivu.
Hii sio hadithi wakuu, imenitokea mimi mwenyewe nikisimamia arusi hii na ukweli nilipigwa na butwaa kwani ni nadra sana kukuta hadi siku ya arusi mtu bado bikra hasa Dar es salaam yetu hii.
Ungekuwa wewe ungemweleza nini Bwana Harusi katika scenario hiyo?