Tempus Fugit
JF-Expert Member
- Jun 22, 2016
- 835
- 2,157
Ni kweli kuwa mbingu ni halisi na ni kweli kuwa jehanam itakuwepo...ila kwa sasa haipo. Hakuna mahala ambapo watu wakifa now wanaenda either mbinguni au wanaenda kuchomwa moto jehanum.
Kama kweli watu wakifa tu now wanaenda mbinguni au Jehanum kuna haja gani sasa ya kuwa na ufufuo aliouahidi Yesu? Yaani kama mtu keshafika mbinguni aliko Mungu...anafufuliwa kwenye kiyama ili iweje tena? Anafufuliwa ili arudishwe tena huko huko mbinguni ambapo alishaenda alipokufa? Illogical.
Maandiko yanasema kuwa kutakuwa na ufufuo wa aina mbili. Ufufuo wa wenye haki na waovu...hawa wote watafufuliwa kupokea malipo yao ktk hukumu...yaani wenye haki kuupata uzima wa milele na waovu kupotea milele.
Ikiwa kama watu wakifa wanaenda direct mbinguni au jehanum kama ulivyosema...kuna haja gani huo ufufuo wa mwisho na hukumu kuwepo?
Kwa sasa hakuna hiyo Jehanum maana kwa mujibu wa kitabu cha Ufunuo 20 moto utakaowaunguza waovu utashuka kutoka mbinguni baada ya waovu kufufuliwa na kuhukumiwa ktk ufufuo wa 2. Kwa maana hiyo moto wa jehanum ni tukio lililoko in the future si sasa.
Yesu pia alisema atakapokuja atawatuma malaika zake wawakusanye wenye haki toka kila kona ya nchi...wakifufuliwa toka makaburini na kuungana na wenye haki watakaokuwa hai wakati huo ili wamlaki Yesu mawinguni awapeleke heaven.
Sasa ikiwa tukio la kuwafufua wafu wenye haki na waovu liko mbeleni, yaani ajapo Yesu...hao unaosema wanakufa na kwenda directly mbinguni na jehanum ni akina nani?
Ufunuo 20 inasema kuwa ktk huo moto wa Jehanum utakaoshuka toka mbinguni atatupwa shetani pia na malaika zake na waovu wote...lakini kwenye kisa chako unasema kuwa kuna majitu ya kutisha yalimfata nduguyo ili kumpeleka Jehanum na malaika wa Mungu wakaingilia kati..
Sasa kati yako na biblia nani mkweli? Maana shetani hana control ya moto wa jehanum kiasi kwamba atume malaika zake wawapeleke waovu motoni...maana Shetani mwenyewe atachomwa na moto huo huo wa Jehanum.
Lastly...Mungu hakuumba majitu ya kutisha kama hayo majitu mawili uliyosema ndugu yako aliyaona yakimfuata. Malaika walioasi wakiongozwa na shetani mwenyewe waliumbwa wakiwa na mwonekano mzuri na wako hivyo hata sasa. Sasa sijui hao majitu unaowasemea wametokea wapi?
Kama kweli watu wakifa tu now wanaenda mbinguni au Jehanum kuna haja gani sasa ya kuwa na ufufuo aliouahidi Yesu? Yaani kama mtu keshafika mbinguni aliko Mungu...anafufuliwa kwenye kiyama ili iweje tena? Anafufuliwa ili arudishwe tena huko huko mbinguni ambapo alishaenda alipokufa? Illogical.
Maandiko yanasema kuwa kutakuwa na ufufuo wa aina mbili. Ufufuo wa wenye haki na waovu...hawa wote watafufuliwa kupokea malipo yao ktk hukumu...yaani wenye haki kuupata uzima wa milele na waovu kupotea milele.
Ikiwa kama watu wakifa wanaenda direct mbinguni au jehanum kama ulivyosema...kuna haja gani huo ufufuo wa mwisho na hukumu kuwepo?
Kwa sasa hakuna hiyo Jehanum maana kwa mujibu wa kitabu cha Ufunuo 20 moto utakaowaunguza waovu utashuka kutoka mbinguni baada ya waovu kufufuliwa na kuhukumiwa ktk ufufuo wa 2. Kwa maana hiyo moto wa jehanum ni tukio lililoko in the future si sasa.
Yesu pia alisema atakapokuja atawatuma malaika zake wawakusanye wenye haki toka kila kona ya nchi...wakifufuliwa toka makaburini na kuungana na wenye haki watakaokuwa hai wakati huo ili wamlaki Yesu mawinguni awapeleke heaven.
Sasa ikiwa tukio la kuwafufua wafu wenye haki na waovu liko mbeleni, yaani ajapo Yesu...hao unaosema wanakufa na kwenda directly mbinguni na jehanum ni akina nani?
Ufunuo 20 inasema kuwa ktk huo moto wa Jehanum utakaoshuka toka mbinguni atatupwa shetani pia na malaika zake na waovu wote...lakini kwenye kisa chako unasema kuwa kuna majitu ya kutisha yalimfata nduguyo ili kumpeleka Jehanum na malaika wa Mungu wakaingilia kati..
Sasa kati yako na biblia nani mkweli? Maana shetani hana control ya moto wa jehanum kiasi kwamba atume malaika zake wawapeleke waovu motoni...maana Shetani mwenyewe atachomwa na moto huo huo wa Jehanum.
Lastly...Mungu hakuumba majitu ya kutisha kama hayo majitu mawili uliyosema ndugu yako aliyaona yakimfuata. Malaika walioasi wakiongozwa na shetani mwenyewe waliumbwa wakiwa na mwonekano mzuri na wako hivyo hata sasa. Sasa sijui hao majitu unaowasemea wametokea wapi?