Kisa cha Kikwete kupigwa mawe huko Jijini Mbeya

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Oct 31, 2014
5,321
11,386
Nimekuwa nikifahamu kwa jinsi ambavyo watu wa bara wanatudharau sana sisi watu wa Pwani. Namfahamu jamaa mmoja tulikuwa naye shule yeye alikuwa hafichi dharau zake.

Akitusema kuwa tunakuwa nyonde nyonde, wavivu, waongo waongo, wanafiki na tusiofaa. Sikuwa napenda tabia ya dharau aliyokuwa akionesha huyo jamaa.

Ila sikudhani kama chuki ile ingefikia hatua ya kumpiga mawe Rais wa Nchi kwa kumwona kuwa ni mswahili swahili. Jamaa waliwaza nini kufikia kumpiga mawe Rais wa nchi?

Wadau nakumbuka kisa hicho ambacho kilisababisha vijana wa eneo hilo wengi kukimbia kijiji chao. Walitafutwa vijana wa kijiji hicho pasipo kujali wahusika na kupigwa sana. Wengi wao hawakuonekana kujutia kosa.

Rais wa nchi anapaswa aheshimiwe hata kinafiki. Tusifikie hatua ya kumpiga mawe, au kumzomea. Leo hii hawa wanaopiga mawe kama wangepata mabomu si wangerusha?

WALE NDUGU NI KWANINI WALIAMUA KUMPIGA MAWE RAIS WA JMT?

Hao wanaozomea mnadhani wakipata risasi hawatamrushia Rais? Tujifunze kuvumiliana. Wazee walisema

"AKUMULIKAYE MCHANA,USIKU ATAKUCHOMA MOTO"
 
Walikuwa wapumbavu tu hao waliopiga mawe!

Walikuwa wanakula na kuvimbiwa kisha wa kaona sehemu ya kupunguza ugali waliovimbiwa ni kumrushia mheshimiwa mawe. Sasa hivi Magu kawakimesha hakuna wa kuokota kokoto wala jiwe, muda huo watatoa wapi wakati chooni kwenyewe hakuendeki
 
Dk slaa aliwafanya vijana wajione wamekuwa makomando wakati ni nyanya tu ,aliwaita makamanda wakawawanapigana na Polisi na kuvunjwa tu ,waliumia yeye sasa yuko ulaya anatesa vijana huwa nawaambia waacheane na siasa za upinzani hailipi

Kule ukonga kuna vijana mpaka Leo ni vilema wakimpigania mwita Leo ni naibu waziri wa CCM

Kule arusha kuna vijana walikufa orasiti kisa wamejazwa upepo wa kijinga na wanasiasa


MBEYA
.ulikuwa ujinga kurusha kumtupia mawe mtu aliyemo ndani ya gari ni upuuzi gari INA bullet proof wewe unarusha jiwe ,kuna vijana pale mpaka Leo ni walemavu

Bangi za mbeya sio


State agent
 
ilikuwa 2008 ile,pindi nipo advance mbalizi wale bwana walijazwa ndani ya karandinga mpaka huruma..Lakin wenyew wakawa wanajimbia tu nyimbo nadhan walikuwa hawajui kifuatacho na kilichofuata sentro mpaka leo sidhan kama wanaweza kusimulia
 
Nimekuwa nikifahamu kwa jinsi ambavyo watu wa bara wanatudharau sana sisi watu wa Pwani. Namfahamu jamaa mmoja tulikuwa naye shule yeye alikuwa hafichi dharau zake.

Akitusema kuwa tunakuwa nyonde nyonde, wavivu, waongo waongo, wanafiki na tusiofaa. Sikuwa napenda tabia ya dharau aliyokuwa akionesha huyo jamaa.

Ila sikudhani kama chuki ile ingefikia hatua ya kumpiga mawe Rais wa Nchi kwa kumwona kuwa ni mswahili swahili. Jamaa waliwaza nini kufikia kumpiga mawe Rais wa nchi?

Wadau nakumbuka kisa hicho ambacho kilisababisha vijana wa eneo hilo wengi kukimbia kijiji chao. Walitafutwa vijana wa kijiji hicho pasipo kujali wahusika na kupigwa sana. Wengi wao hawakuonekana kujutia kosa.

Rais wa nchi anapaswa aheshimiwe hata kinafiki. Tusifikie hatua ya kumpiga mawe, au kumzomea. Leo hii hawa wanaopiga mawe kama wangepata mabomu si wangerusha?

WALE NDUGU NI KWANINI WALIAMUA KUMPIGA MAWE RAIS WA JMT?

Hao wanaozomea mnadhani wakipata risasi hawatamrushia Rais? Tujifunze kuvumiliana. Wazee walisema

"AKUMULIKAYE MCHANA,USIKU ATAKUCHOMA MOTO"
Acha uchochezi!
Unachochea matukio ya chuki unafaidika nini?
 
Waafrika wengi bado hatujui nini maana ya uhuru wa demokrasia, wengi ukiwauliza wanakuambia ndio fursa ya kumtukana rais, kuponda kila nzuri analofanya.
 
Waafrika wengi bado hatujui nini maana ya uhuru wa demokrasia, wengi ukiwauliza wanakuambia ndio fursa ya kumtukana rais, kuponda kila nzuri analofanya.

..pia siyo fursa ya chama tawala kutukana wapinzani.

..au chama tawala kutumia vyombo vya dola na mahakama kudhuru na kudhulumu wapinzani.

..pia siyo makosa kwa mwenyekiti wa chama tawala kuwa juu ya sheria na katiba.
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom