Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,349
- 6,476
Wakati afande Mambosasa akiwa kwenye press conference, alikuwa na mambo mawili, la kwanza ni lile la wabunge wa CHADEMA na meya kukamatwa kule Segerea, na la pili ni ajali ya gari. Alianza kwa kusema, '... wafuasi wa chama cha maendeleo na wananchi - CHADEMA.'
Maswali: hivi kirefu cha Chadema ni chama cha maendeleo na wananchi? Au maana hii ni kutokana na michango ya wananchi kulipa faini ya wabunge wa Chadema? Huko ni kuteleza au ndio aonavyo yeye kutokana na wananchi kuchangia faini ya wabunge wa Chadema? Au siku zote hakujua kirefu cha Chadema kuwa ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo? Au msamiati DEMOKRASIA haupo kabisa kwenye kapu la misamiati la Kamanda? Je, hicho kirefu kipya cha Chadema na chenyewe anakipeleka kwa umma?
Msikilize kamanda katika video hii sekunde 35 za mwanzo.
Maswali: hivi kirefu cha Chadema ni chama cha maendeleo na wananchi? Au maana hii ni kutokana na michango ya wananchi kulipa faini ya wabunge wa Chadema? Huko ni kuteleza au ndio aonavyo yeye kutokana na wananchi kuchangia faini ya wabunge wa Chadema? Au siku zote hakujua kirefu cha Chadema kuwa ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo? Au msamiati DEMOKRASIA haupo kabisa kwenye kapu la misamiati la Kamanda? Je, hicho kirefu kipya cha Chadema na chenyewe anakipeleka kwa umma?
Msikilize kamanda katika video hii sekunde 35 za mwanzo.