Kiranga sio atheist ni non-believer

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,632
697,749
Kinara mbishi asiyekubali kuwa kuna Mungu. Mbishi kwa viwango vyote unavyojua ila mwepesi wa hoja.

Kiranga sio atheist, kwa tafsiri rahisi atheist ni mtu asiyejua lolote kuhusu Mungu ama miungu (Hana ABC zozote kuhusu hizo imani za Mungu na miungu)

Kiranga sio mmojawapo. Kiranga ni mmojawapo wa wale waliokengeuka imani, walizaliwa katika ukristo wakabatizwa na kuishi maisha ya ukristo... Lakini along the way wakabahatika kusoma doctrines za kikristo, Mungu nk.

Ni katika hizo doctrines wakashindwa kukubaliana na vifungu kadhaa hivyo wakakengeuka na kuwa wapinga Uwepo wa Mungu mkuu.

Ni watu wenye elimu kubwa kuhusu dini hasa ukristo halafu wakasoma na doctrines nyingine zinazopinga uwepo wa Mungu na kuchagua kuyaamini hayo.

Kipengele muhimu hawa watu wasio waaamini ni kule kutaka wanachokikwepa ni kile cha kutotaka kutambua kuwa ishu za kiroho, Kimungu hazina ithibati za kisayansi.

Wote tuna akili. Je, kuna ithibati? Na kama hatuna akili tuna ithibati? Lakini uhalisia unasemaje?

Kwahiyo Kiranga anataka umuoneshe Mungu as if ni kitu solid. Kiufupi hawa sio atheists bali non believers!!!
 
Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali." Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu.

Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
 
Mimi watu sijui wanaopinga uwepo wa Mungu ,huwa hata wakiongea wanatapika dhahabu naishiaga kuwadharau tuuu.

Niivi " Kwa Mungu kila goti litapigwa ,uwe mwanga ,nabii fek. Mchawi, Msali nusu, ajuaye Mungu yupo lkn haishi kujitanabaisha kwa jamii kua hayupo Mungu , Muhun,mwizi , kahaba. Malaya, Atheist sijui uwe nani ukoo , KWA MUNGU KILA GOTI LITAPIGWA TUU , watu tutaruka ruka weeeeee lkn Kwa Mungu kila Goti litapigwa !!
 
Umenena kweli kabisa mkuu. Ila Mungu ni mkuu na wa ajabu, huwajaaria watu hawa ukuu na maarifa baadaye hutumia maarifa hayo kumbomoa lakini yeye huendelea kuwabariki. Mungu haweki hasira juu ya asiye muamini.
Kiranga haamini uwepo na uwezo wa Mungu sababu kwake alitaka Mungu awe kama alivyo rais wa nchi, kwamba leo anaweza akaenda bandarini akaokota vichwa vya treni, akagawa mapapai, akagawa mabulungutu ya hela, akawapigia simu watendaji kwenye mkutano wa hadhara watendaji wake na kutoa maagizo.

Huyu Mungu wetu angeweza kuyafanya yote haya huku Kiranga akishuhudia basi angeweza kuamini kuwa kuna Mungu. Kwake mtu huyu ni mungu zaidi ya Mungu tunayemuamini.
 
Wasema atheist ni yule asiyejua lolote kumhusu Mungu ama miunngu. Lakini ili tupate tofauti halisi ya nonbeliever na atheist ni lazima tuangalie engo mbalimbali, kama vile; Elimu ya mtu, jamii alimozaliwa, uwezo wa kiuchumi wa mtu au taifa atakapo, upatikanaji wa machapisho ya kidini n.k.

Sasa ukija kuangalia vigezo hivyo utagundua kua kuna watu wanaamini uwepo wa Mungu pasipo kuwa na elimu yoyote kumhusu Mungu na hawana hoja imara za kutetea uwepo wa Mungu.

Hawa ni wale wanaoishi chini ya umaskini mkubwa katika maeneo maskini ambayo wakati fulani yaliwahi kufikiwa na waeneza dini ambao walipata wafuasi fulani lakini baadaye mawasiliano yale yakakata hivyo wafuasi waandamizi wakakosa elimu ya kile walichorithi toka kwa wazazi wao, na wao kubaki tu na majina yanayoashiria dini ile hivyo kuendelea kuitwa waamini.

Vilevile utaona pia kuna watu wamezaliwa kwenye mataifa ya kidini ambamo dini ni sehemu ya maisha katika jamii husika, lakini wao hawaamini katika hizo dini bila kujali kama walipata elimu ya dini ama la na hawapingani na yeyote kumhusu Mungu. Hivyo wanasalia kuitwa waamini pasipo wao kuamini.

Pia kuna wengine wamesoma kanuni na miongozo mbalimbali ya kidini, lakini wao wakaichukulia kama vitabu na machapisho mengine ya kutoa elimu wakashika maarifa yaliyomo na wasifuate njia za kuabudu za kundi lile. Mfano mzuri ni Japan nchi inayoongoza kuwa na maatheist wengi lakini bado huwa wanasoma authoritative books ambazo zimeandaliwa na watu wa dini kwa lengo la kuwaelimisha waamini wao.

Mtazamo mwingine dhidi ya nonbeliever na atheist waweza kuangaliwa kupitia wale wanaojiita waamini ama wenye dini. Kwa miaka mingi kumekua na matamshi kutoka kundi fulani la wanaojiita wenye dini kuwaita wafuasi wa kundi jingine kama wasioamini (nonbelievers) kwa sababu tu, wanatofautiana katika imani zao kumwelekea Mungu. Na hii inatokana na ubinafsi wa kila mwenye dini kuamini kuwa dini yake ni sahihi kuliko ya mwingine.

Hitimisho, kwa hayo machache waweza kuona namna ilivyo vigumu kupata kategoria rahisi za kuwatofautisha nonbelievers na maaatheists. Kwa sababu dunia ya sasa yenye teknologia bora kabisa ya kuwezesha watu kupata machapisho mbalimbali yahusuyo dini na miongozo yake imekua ikishuhudia kuongezeka kwa kasi kwa kundi la wale wanaoitwa wakana Mungu.
 
Kiranga ukitaka kumuuluza kama uchawi upo,atakwambia ufafanue zaidi kuhusu uchawi unao uzungumzia,Mara atasema mambo ya titration za chemistry binafsi Mimi naona kiranga anamsimamo mkali sana nahii imetokana na uwezo wake mkubwa sana wa kielemu kuhusu hizi dini za duniani
 
Back
Top Bottom