Kiprotokali Waziri akienguliwa akiwa katikati ya majukumu yake mikoani mambo gani husitishwa kwake mara moja?

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,551
Somo tajwa hapo juu lahusika.

Waziri ni mteule wa Rais. Hupewa ulinzi na pengine msafara ama malazi / usafiri / chakula na mengineo kiprotokali.

Akiwa mikoani katikati ya majukumu yake halafu akaenguliwa anasitishiwa huduma gani au mambo gani right on the spot ?

Vitu gani anavikosa papo hapo hata akiwa safarini ? Au ni mpaka apewe official letter ndipo huanza kuhudumu kama Mbunge wa kawaida ?

Ni hili tu.
 
kwenye ofisi za kawaida ukifukuzwa kazi au ukuacha kazi.. unapewa clearance fomu ambapo utarudisha kila kitu cha ofisi within a working day inayofata.. labda uwe na dharura kama ugonjwa...

nina imani waziri nae anafanya hivyo.. ila kumlazimisha same day sio fair.. jumapili au jumamos unamrudishia nani gari au kitambulisho au simu. ofisi gani ipo wazi
 
Somo tajwa hapo juu lahusika.

Waziri ni mteule wa Rais. Hupewa ulinzi na pengine msafara ama malazi / usafiri / chakula na mengineo kiprotokali.

Akiwa mikoani katikati ya majukumu yake halafu akaenguliwa anasitishiwa huduma gani au mambo gani right on the spot ?

Vitu gani anavikosa papo hapo hata akiwa safarini ? Au ni mpaka apewe official letter ndipo huanza kuhudumu kama Mbunge wa kawaida ?

Ni hili tu.

Mimi najua ambacho Mtu hukikosa haraka ni kama ' akitumbuliwa ' ni kutovalia tu tena kwa Kujiamini na Madaha yote ' Skafu ' yake yenye Bendera ya Tanzania inayoijumuisha pia na Mkoa wa Singida.
 
Gari la Ofisi

Nyumba ya Waziri Dsm na Dodoma

Simu ya Mkononi

Mlinzi

Msafara

Secretary / Katibu wake

Kitambulisho chake

Bendera ya Taifa


Vyote hunyang'anywa paaapu!

Hivi kinachotangulia kukabithiwa ni gari au ofisi?
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom