Kipindupindu chaibuka tena Dar, mwananchi atakayemkamata mchafuzi wa mazingira kupewa 20,000

Johnny Sack

JF-Expert Member
Jan 21, 2017
8,779
18,746
Ugonjwa wa kipindupindu umeibuka tena Dar na halmashauri ya manispaa ya Temeke itatoa adhabu kali kwa wataokuwa wanatupa taka hovyo Dar
Mkuu wa wilaya ya Temeke Felix Lyaniva kimepiga hodi baadhi ya maeneo kutokana na wananchi kutupa taka hovyo na kutiririsha maji machafu

MKuu wa idara ya usafi na mazingira manispaa ya Temeke amesema atayeleta takataka siku ambayo siyo ya usafi atatozwa faini ya 50,000 na aliyemkamata na kumripoti atapata 40%ya faini hiyo
 
Masikini mkuu wa wilaya! Ingekuwa busara kuanza kuzoa taka ambazo tayari zimekwisha tupwa na madimbi ya maji machafu yaliyosababishwa na mvua badala ya kufikiria kupata mapato.
 
Bora angekuwa mbunifu zile condom pale sugar ray zimejaa bidhaa adimu,angezitafutia soko kwenye viwanda vya lubricants
 
Kipindupindu daresalaam siyo kitu cha kushangaza, jiji chafu mno.Sijui kwa nini wanashindwa kuiga mji wa Moshi!
 
Back
Top Bottom