Mngurimi
JF-Expert Member
- May 27, 2020
- 819
- 789
Hiki ni kisa ambacho kinaweza kuwagusa wengi hasa wale vijana wa kiume katika maisha ya mahusiano. Mara nyingi unakuta katika pilikapilika za hapa na pale za kusaka mpenzi/mchumba, kijana wa kiume anampenda msichana kwa wakati fulani lakini unakuta msichana huyo hataki kuridhia muda huo hadi pale anapotendwa na mwingine au kutelekezwa.
Miaka ya nyuma kidogo kulikuwa na msichana fulani hivi nilitokea kumpenda sana. Msela nilikuwa nikijaribu kutema cheche kila kukicha bila mafanikio yoyote. Urembo, tabia na upole wake ni vitu ambavyo vilikuwa vikinivutia kiasi cha kutamani kuwa naye. Nilijaribu hadi kutumia marafiki zake wa karibu ili wajaribu kumshawishi, lakini mtoto hakutaka hata kunielewa. Mmoja kati ya rafiki yake mkubwa alisema yule dada bado hajajua na hadhani hata kama ameshakutana na mtu yeyote yule kimwili.
Baada ya kuona nyavu zangu hazinasi, ilibidi nimpotezee niendelee na maisha mengine. Baada ya hapo nilisafiri kwenda masomoni kwa muda wa miaka miwili. Kitu cha kushangaza baada ya kurudi nilishangaa kumkuta dada wa watu akiwa na mtoto wa miezi miwili. Nilishangaa sana japo moyoni nikasema tayari wahuni washamkomesha. Kilichonishangaza zaidi yule dada baada ya kupata taarifa kuwa nimerudi, alitafuta namba yangu na kuomba tuonane.
Kabla ya kumkubalia, nilikataa sana ila baadaye ilibidi nikubali wito wake. Siku ya kuonana iliwadia na katika maongezi yake alikuwa akidai kuwa nimsamehe kwa sababu ananipenda. Kusema kweli, nilikataa na kudai kuwa "laiti kama angekuwa ananipenda, basi angenikubalia tangu mwanzo". Isitoshe mimi tayari nilikuwa kwenye mahusiano na mtu mwingine hivyo isingekuwa rahisi kuwa naye tena.
Baada ya mazungumzo nikamtia moyo na nikamwambia aendelee na yule aliyemzalisha japo kwa maelezo yake anasema, baada ya kujifungua jamaa alianza visa na kukwepa majukumu kisha wakaachana. Kusema ukweli, mimi niliumia maana sina moyo wa chuma wa kustahimili mtu azae na mwingine kisha aje kwangu kama kimbilio.
Swali langu:
Hivi mtu wa namna huyo unaweza kumkubalia kwa lipi?
Kama alikuwa ananipenda ni kwa nini asingekubali tangu wakati ule kiasi cha kunitesa moyo wangu kiasi kile?
Mambo haya huchochewa na nini hasa kwa wasichana?
Karibuni tushauriane.....
Miaka ya nyuma kidogo kulikuwa na msichana fulani hivi nilitokea kumpenda sana. Msela nilikuwa nikijaribu kutema cheche kila kukicha bila mafanikio yoyote. Urembo, tabia na upole wake ni vitu ambavyo vilikuwa vikinivutia kiasi cha kutamani kuwa naye. Nilijaribu hadi kutumia marafiki zake wa karibu ili wajaribu kumshawishi, lakini mtoto hakutaka hata kunielewa. Mmoja kati ya rafiki yake mkubwa alisema yule dada bado hajajua na hadhani hata kama ameshakutana na mtu yeyote yule kimwili.
Baada ya kuona nyavu zangu hazinasi, ilibidi nimpotezee niendelee na maisha mengine. Baada ya hapo nilisafiri kwenda masomoni kwa muda wa miaka miwili. Kitu cha kushangaza baada ya kurudi nilishangaa kumkuta dada wa watu akiwa na mtoto wa miezi miwili. Nilishangaa sana japo moyoni nikasema tayari wahuni washamkomesha. Kilichonishangaza zaidi yule dada baada ya kupata taarifa kuwa nimerudi, alitafuta namba yangu na kuomba tuonane.
Kabla ya kumkubalia, nilikataa sana ila baadaye ilibidi nikubali wito wake. Siku ya kuonana iliwadia na katika maongezi yake alikuwa akidai kuwa nimsamehe kwa sababu ananipenda. Kusema kweli, nilikataa na kudai kuwa "laiti kama angekuwa ananipenda, basi angenikubalia tangu mwanzo". Isitoshe mimi tayari nilikuwa kwenye mahusiano na mtu mwingine hivyo isingekuwa rahisi kuwa naye tena.
Baada ya mazungumzo nikamtia moyo na nikamwambia aendelee na yule aliyemzalisha japo kwa maelezo yake anasema, baada ya kujifungua jamaa alianza visa na kukwepa majukumu kisha wakaachana. Kusema ukweli, mimi niliumia maana sina moyo wa chuma wa kustahimili mtu azae na mwingine kisha aje kwangu kama kimbilio.
Swali langu:
Hivi mtu wa namna huyo unaweza kumkubalia kwa lipi?
Kama alikuwa ananipenda ni kwa nini asingekubali tangu wakati ule kiasi cha kunitesa moyo wangu kiasi kile?
Mambo haya huchochewa na nini hasa kwa wasichana?
Karibuni tushauriane.....