Kwa upande wangu naona hakuna hata mmoja wote Nyerere ameipokea nchi kutoka kwa wakoloni ikiwa imejaa mashamba ya mkonge,buni na vyenginevyo na Kikwete nae hana changamoto amerithi utawala.
Changamoto au chalenge itapatikana wakati Nchi itakapopata mtawala kutoka Chama kingine na sio CCM ,ni maoni yangu.
Kwa upande wangu naona hakuna hata mmoja wote Nyerere ameipokea nchi kutoka kwa wakoloni ikiwa imejaa mashamba ya mkonge,buni na vyenginevyo na Kikwete nae hana changamoto amerithi utawala.
Changamoto au chalenge itapatikana wakati Nchi itakapopata mtawala kutoka Chama kingine na sio CCM ,ni maoni yangu.
Ndugu Mwiba,
Umeelewa swali? Au unataka kuwa Yogi Berra?
Swali ni comparison ya challenges alizozipata Nyerere wakati anachukua nchi vs alizozipata Kikwete, zipi zilikuwa kubwa zaidi?
Sasa utasemaje "hakuna hata mmoja"? Swali si nani alifanikiwa kuzifanyia kazi challenges hizi, ni zipi zilikuwa tough zaidi.
Kusema kwamba "hamna hata mmoja" kwa maan ya kwamba wote walikuwa na 0 challenge ni utovu wa maoni, kwa sababu nilizozitaja katika post yangu hapo juu.
Duh! mkuu hili swali zito lakini nadhani linaweza kujibiwa kinamna!..
Nyerere alitawala wakati wa wajinga wengi... na Kikwete ametawala wakati kuna Wajanja wengi, sasa hapa inategemea hizo challenges unazozungumzia ni zipi..
Kuyapata Maendeleo ukiwa na wajinga wengi ni kazi nzito sana (hawakuelewi) lakini pia ni kazi nyingine kuyapata maendeleo ukiwa na wajanja wengi (wanaelewa kuliko wewe) hao - Mafisadi!
Hakuna chochote ni ubovu wa utawala wa CCM ,wote wameikuta nchi katika amani na utulivu,wameshindwa kuliendeleza hilo,na wote wameikuta nchi ni tajiri wameshindwa kuulinda na kuutumia kwa ajili ya maendeleo kwa wananchi.
Kusema Nyerere alikuta watu wajinga hilo sio kweli,si Nyerere peke yake alikuwa msomi wakati huo ,yeye Nyerere aliwakuta watu wakiwa katika harakati za siasa.Kikwete ni mrithi wa utawala ni kama mtoto wa Mfalme kwenye utawala huu wa sisi au huyu ni mwenzetu.
Msimamo wangu ni kuwa Challenge itakuja yatakapotokea mabadiliko ya uongozi kichama na si kimtu katika kuiongoza Tanzania.
Huwezi kusema unakutana au umekutana na Challenge wakati system nzima ya utawala liusalama kiulinzi ipo chini yako inasikiliza amri tu ,nini wafanye,hatua gani wachukue ,leo ukubwa huo na cheo hicho hakitumiki ni kuendeleza kuogopana ,wandugu challenge iliyopo ni kushindwa kwa wakubwa wa Chama tawala kuchukua au kutumia madaraka yao kama viongozi wakuu wa nchi ,wanaheshimiana ,wanalindana ,ni mrafiki jamani katika kuongoza nchi unaleta udugu na urafiki ,kweli tutafika ?,CCM wameshindwa kuendeleza nchi wapo pale pale kila anaekuja anachukua chake mapema , halafu unategemea kuwa anaerithi aendeshe nchi tofauti na wenziwe ambao bado wamo katika system ,si unaona kila Raisi aneondoka huwa anashiriki katika maamuzi mbona nchi nyengine hatuoni utumbo huu si kwenye utawala wala kwenye chama ,huyo hapo Mandela tokea aache Uraisi humsikii katika harakati za kiserikali wala za kichama iweje hapa Tz viongozi wastaafu wawe ving,ang'anizi kama si kukiritimba ni kitu gani ,vipi utamweka Raisi aliekuwepo kuwa anakutana na challenge wakati wote wamo kwenye chungu kimoja.
Chama mbadala katika uongozi ndicho kitakachokutana na Challenge ya kuhakikisha yale ya kuogopana yote yanafanyiwa kazi kikamilifu na sio kusuasua.
Mkuu labda hapa umeshindwa kuelewa maana...Kusema Nyerere alikuta watu wajinga hilo sio kweli,si Nyerere peke yake alikuwa msomi wakati huo ,yeye Nyerere aliwakuta watu wakiwa katika harakati za siasa.Kikwete ni mrithi wa utawala ni kama mtoto wa Mfalme kwenye utawala huu wa sisi au huyu ni mwenzetu.
Ndugu Mwiba,
Umeelewa swali? Au unataka kuwa Yogi Berra?
Swali ni comparison ya challenges alizozipata Nyerere wakati anachukua nchi vs alizozipata Kikwete, zipi zilikuwa kubwa zaidi?
Sasa utasemaje "hakuna hata mmoja"? Swali si nani alifanikiwa kuzifanyia kazi challenges hizi, ni zipi zilikuwa tough zaidi.
Kusema kwamba "hamna hata mmoja" kwa maan ya kwamba wote walikuwa na 0 challenge ni utovu wa maoni, kwa sababu nilizozitaja katika post yangu hapo juu.
Kwiii! kwiii! kwii! Mkuu hapo tupo pamoja..Kulinganisha challenge za Kikwete na za Nyerere ni sawa sawa na kulinganisha challenge za kujenga nyumba -kuanzia msingi kwenda juu- na challenge za mtu kufanya maintenance.
Nyerere alijenga nyumba, Kikwete kaikuta nyumba anafanyia maintenance.
Kati ya kujenga nyumba na kuifanyia maintenance wapi kuna challenge kubwa?