Kipindi cha kuvunja taa ya V8 na kukimbia sasa kimepitwa na wakati, kijana anatengeneza taa kwa pesa ya supu Tabata

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Sep 4, 2013
36,039
40,701
Mabibi na mabwana, kile kipindi cha kuvunja taa ya V8 na kukimbia eneo la ajali sasa kimepitwa na wakati, kwa sasa ukivunja taa ya V8 wewe simama ongea tu na mwenye gari kisha mpeleke Tabata Sanene kwenye kiwanda cha kutengeneza taa, badala ya kutumia milioni 4 kununua taa moja, sasa utatumia pesa ya ‘supu na chapati mbili’ tu, karibuni tumsapoti. Huduma zao ni za uhakika.

 
Sanene sehemu gani? nna li gari nataka kumpelekea kesho.
6B9074D3-415A-4ED9-B0D9-4A2D287D0CE9.jpeg
 
Kazi nzuri, hapa Serikali ingefaa wamuwezeshe kimafunzo zaidi. Taasisi kama Sido ndo ingefaa imshike mkono aweze kufanya molding kwa shape tofautitofauti.
 
Bongo hawakawii kutuma kikosi kazi cha TBS kufunga kiwanda
Bila kuwasahau wale wa TRA, hii nchi sio kwamba inashindikana kuemdelea, bali tumejiwekea mtego wenyewe wa kuuwa kila kinachotaka kukua na kukimaliza kabisa.., sasa hivi utasikia kafungiwa, kumbe nyuma yaboazia wafanyabiashara wa taa kariakoo wanakuwa wamemuundia zengwe tu ili waendelee kupiga pesa..
 
Kazi nzuri, hapa Serikali ingefaa wamuwezeshe kimafunzo zaidi. Taasisi kama Sido ndo ingefaa imshike mkono aweze kufanya molding kwa shape tofautitofauti.
Badala ya kufanya haya, wao watatuma kikosi kazi cha TBS kwenda kumfungia, akili yao ni kufungia watu, na si kuwawezesha, wakati huyu ni msaada mkubwa sana kwa taifa hili!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom