East African
JF-Expert Member
- Nov 27, 2013
- 704
- 989
Nilikuwa mpenzi mzuru wa kufuatilia kipindi cha Jahazi cha Clouds FM hasa wakati kikiendeshwa na Gadna, lakini tangu aondoke hakuna kinachoendelea hapo. Ni kelele za watangazaji hasa Kibonde anaboa hazi basi maana anajifanya anajua kila kitu.
Kipindi kinaanza saa 10;00 hadi 1;00 uck takribani masaa 3 lakini hakuna cha maana tunachoweza kujifunza. Ni segment moja tu ya taarifa ya habari ya saa 12;00 ndiyo inayovutia, lakini mambo yanayobaki ni porojo tupu za Kibonde na sasa amewaharibu hata wale wenzake ambao wanaonekana kuwa na kauelewa kidogo.
Nakuomba mkurugenzi wa matangazo na vipindi uliangalie hili kwani unapoteza washabiki wengi sana katika kipindi hiki cha Jahazi. Hakuna jipya zaidi ya kusikia salamu za Kibonde(ASALAM ALEIKUM na habari za town ambazo eti anazisoma kutoka katika magazeti ya asubuhi ambayo habari zake zisha expire.
Pamoja na hayo napenda kumpongeza sana sana Mtangazaji maarufu Millard Ayo wa kipindi cha Amplifaya kweli huyu dogo yuko safi sana hana masihara katika kipindi chake na ninapendekeza apewe tuzo ya kipindi bora zaidi cha CLOUDS FM.
Kipindi kinaanza saa 10;00 hadi 1;00 uck takribani masaa 3 lakini hakuna cha maana tunachoweza kujifunza. Ni segment moja tu ya taarifa ya habari ya saa 12;00 ndiyo inayovutia, lakini mambo yanayobaki ni porojo tupu za Kibonde na sasa amewaharibu hata wale wenzake ambao wanaonekana kuwa na kauelewa kidogo.
Nakuomba mkurugenzi wa matangazo na vipindi uliangalie hili kwani unapoteza washabiki wengi sana katika kipindi hiki cha Jahazi. Hakuna jipya zaidi ya kusikia salamu za Kibonde(ASALAM ALEIKUM na habari za town ambazo eti anazisoma kutoka katika magazeti ya asubuhi ambayo habari zake zisha expire.
Pamoja na hayo napenda kumpongeza sana sana Mtangazaji maarufu Millard Ayo wa kipindi cha Amplifaya kweli huyu dogo yuko safi sana hana masihara katika kipindi chake na ninapendekeza apewe tuzo ya kipindi bora zaidi cha CLOUDS FM.