Kipimo halisi cha kiongozi kukubalika au kupendwa na raia wake wengi

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
36,569
44,223
Uongozi wowote unaojinadi unakubalika na raia walio wengi hupimwa kwa uchaguzi huru na wa haki. Kudai kiongozi anapendwa na wengi bila kipimo hiki ni ujuha.

Huwezi kusema kiongozi anakubalika na raia wengi kama huyo kiongozi na serikali yake wamepatikana katika uchaguzi ambao Tume ya uchaguzi sio huru, wapinzani wanabughudhiwa kufanya siasa na kampeni, vyombo vya habari haviko huru kuwapa wapinzani nafasi au kukosoa watawala na ametumia faida ya dola kujipatia madaraka.

Huwezi kuwahoji watu wachache kwa TV au redio ukatumia hiko kama kigezo cha kupima viongozi, kwenye nchi zenye demokrasia dhaifu hata kura za maoni "opinion polls" bado sio kipimo cha kuaminika.Mwisho pia huwezi kutumia wingi wa watu waliohudhuria mazishi yake kama kipimo cha kukubalika.

Sanduku huru la kura tu ndio kipimo sahihi.
 
Uongozi wowote unaojinadi unakubalika na raia walio wengi hupimwa kwa uchaguzi huru na wa haki. Kudai kiongozi anapendwa na wengi bila kipimo hiki ni ujuha.

Huwezi kusema kiongozi anakubalika na raia wengi kama huyo kiongozi na serikali yake wamepatikana katika uchaguzi ambao Tume ya uchaguzi sio huru, wapinzani wanabughudhiwa kufanya siasa na kampeni, vyombo vya habari haviko huru kuwapa wapinzani nafasi au kukosoa watawala na ametumia faida ya dola kujipatia madaraka.

Huwezi kuwahoji watu wachache kwa TV au redio ukatumia hiko kama kigezo cha kupima viongozi, kwenye nchi zenye demokrasia dhaifu hata kura za maoni "opinion polls" bado sio kipimo cha kuaminika.Mwisho pia huwezi kutumia wingi wa watu waliohudhuria mazishi yake kama kipimo cha kukubalika.

Sanduku huru la kura tu ndio kipimo sahihi.
Kwenye msiba hata mchawi aliyekuwa anaua au kuwapa maradhi wananchi wenzie huzikwa na watu wengi kwa kuwa watu hutaka kuhakikisha kama kweli amekufa? Na pili kuchimba kaburi refu ili huyo mchawi asijekurudi kwa kufufuka.

Hiyo ndiyo sababu iliyopelekea Magufuli kuangaliwa akiwa amekufa Wala siyo kupendwa, utampendaje shetani?
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom