kipigo toka kwa mpenzi, mke au mume... ni mapenzi ya dhati

Smile

JF-Expert Member
Jul 18, 2011
15,347
11,610
kuna thread nimesoma humu bwana ikanikumbusha maisha ya nyuma
kidogo
nilikuwa na mahusiano na jamaa mmoja dah huyu jamaa alikuwa ananipenda kweli kusema kweli ,ila tatizo lake ni kipigo
alishanipa mkongoto wa haja kama mara tatu hivi
alinipa kipigo jamani siku moja kidogo nife nikaona cha kujifia
yaani nilipigwa siku hiyo duh nikamwambia mother nimeanguka kwenye mti wa parachichi ilikuwa maafa
tatizo ilikuwa ni simu tu jamani kiukweli nilikuwa nachat chati na mwanaume mwingine ila alikuwa sio mpenzi wangu.jamaa alikuwa anamind simu yangu sijui vile aliinunua...nilichezea vichapo sio kidogo.
at last nikamkimbia
ila nimenotice mwanaume /mke anaekupiga ana upendo wa kweli hawezi kuishi bila wewe so anatumia any defenceve mechanism kukukeep!
sio mtu kakupigia tu hujapokea simu anakupiga chini..kwani mimi operator wa simu kila saa nipokee simu
au wrong sms umeikuta kwenye simu ya mpenzi au mke unamuacha sio fair bwana fight for your love !
 
Bora kipigo unapata fundisho kwamba what u did was wrong rather than kujitia unamuacha mtu bila kutoa explanations....
 
inategemea na tamaduni za watu. kuna wengine wanaamini kupiga mke ni ishara ya upendo wakati to others ni njia ya kukulaza mahabusu lol.

personally: no to hitting your wife/hubby as i dont derive joy in causing pain kwa mtu mwingine. nor do i express upendo using physical violence
 
Smile umenichekesha sana yaani nakuvutia picha jinsi ulivyokua unapata kipondo lol pole sana. Mapenzi ya kupigana inategemea wahusika wanapenda nini ni vigumu kusema hayafai au yanafaa . Kila mmoja ana namna yake ya kupenda. Yaani bado nacheka jinsi ulivyodanganya home.
 
Last edited by a moderator:
Ila nimenotice mwanaume /mke anaekupiga ana upendo wa kweli hawezi kuishi bila wewe so anatumia any defenceve

Dah!!! Smile story yako inataka kunifanya niwe mchokonozi.

Sasa kama ndio hivyo hapo juu, vipi kwa jamaa uliyemkacha? Maisha yake yakoje? mawazo yamemtawala au ulimuonea huruma ukamrudia?
:focus:
Ila jamani kupigwa kunahitaji mtu mwenye moyo mgumu, lasivyo ndani hakutakalika(virago vyako vitakuhusu).
Copy to Mwita Maranya
 
Last edited by a moderator:
Smile nadhani huyo mpenzi wako pamoja na kuwa kweli alikuwa anakupenda sana lakini nadhani alikuwa na tatizo la kutodhibiti hasira zake. Tunaambiwa tuwe na hasira lakini tusitende dhambi, hivyo ni swala tu la kujifunza kudhiti hasira ambalo hata wewe ungemshauri maana kwa andiko lako hili inaonesha bado huyo bwana ana nafasi ya mapenzi ndani yako.

Kupigana kwenye mahusiano/ndoa kupo sana tu kwa watu wengi sana, sema jambo linalosaidia wengi ni pale usiku unapoingia mnapoingia maeneo ya kuunganika kuwa kitu kimoja hakika mmoja wapo akipatwa na hisia ya tendo la ndoa basi mchezo unaisha na maisha mapya yanaanza tena.

Ablessed usicheke sana ndg, hayo mambo yapo, japo tunaweza kusema yamepitwa na wakati, lakini mara nyingine hutokea hata mtenda mwenyewe bila kupanga kufanya hivyo, so hata baadaye anaweza kuanza kujuta juu ya kitendo alichofanya, sema tu wengi wetu hata kusema sorry tunaona so tena, mfumo dume huo.
 
Last edited by a moderator:
Dah!!! Smile story yako inataka kunifanya niwe mchokonozi.

Sasa kama ndio hivyo hapo juu, vipi kwa jamaa uliyemkacha? Maisha yake yakoje? mawazo yamemtawala au ulimuonea huruma ukamrudia?
:focus:
Ila jamani kupigwa kunahitaji mtu mwenye moyo mgumu, lasivyo ndani hakutakalika(virago vyako vitakuhusu).
Copy to Mwita Maranya
ni mtu fresh tu kimaisha tuliachana sio kwa ajili ya kipigo hata ni story ingine
 
Iam allergic na vipigo aisee......

Na toka mwanzo wa mahusiano namweleza mtu kabisaaaa mwili wangu ni wa starehe sio wa vipigo....
Maana ukinishinda nguvu hata kisu nitakurushia sasa mambo ya kuonja majengo ya serikali nani anayataka?
ahaaa mimi nilijitahidi kujihami siku moja nilichukua lispeaker la sub lile lirefu nikamtwaga nalo ila daah kupigana sio kabisa my dear acha tu
 
ni mtu fresh tu kimaisha tuliachana sio kwa ajili ya kipigo hata ni story ingine

Mambo Smile? aisee pole sana kwa kumbukumbu ya kipigo ingawa naona ulikuwa mvumilivu kwa kiwango cha kutosha. Yani ungefaa kuwa mke wangu kwakuwa mara moja moja huwa namfinya mama Rhobi.
 
Last edited by a moderator:
kufunzwa adabu ni vizuri babu...unadhani nilivokuwa nachat chat na wanaume wengine nilikuwa nafanya vizuri basii

Ina maana wewe ni punda shurti kwa magongo?

Tangu nazaliwa hadi umri huu sijawahi kupigwa hata siku moja, si nyumbani si shuleni, na kama kufunzwa nikafunzika si haba
 
Mwanaume kupigana ni alama ya kushindwa kwake ku-solve problems. It means he is unable or unwilling to solve the problem and he resorts to violence to kill the matter once and for all. unfortunately all he does is postpone the unavoidable moment when he will have to deal with it, and he adds another problem: a violent relation.
 
Ina maana wewe ni punda shurti kwa magongo?

Tangu nazaliwa hadi umri huu sijawahi kupigwa hata siku moja, si nyumbani si shuleni, na kama kufunzwa nikafunzika si haba
heri yako mwenzangu mi kila mahali nimepigwa nyumbani shuleni na kwa mpenzi
 
Ni wazi ulikuwa umezoea kupigwa na bila ngumi ulikua uendi ndio maana nio mara tatu na kwa uchunguzi nilio ufanya kupitia ulicho andika ni wazi ulipigwa mara nyingi na sababu ya kuachana na jamaa si kwa sababu alikuwa ana kupiga bali ni sababu nyingiune. Wewe kupigwa ulizoea na ilikuwa part ya mapenzi kwako na ndio maana ilikuwa zaidi ya mara tatu.

Ni wazi wewe bila mikwara ya kipigo usongi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom