Kipi ni bora na busara zaidi kati ya kuasili mtoto na kulea mtoto wa ndugu?

Ni jambo jema kufikiria hivyo na kuwa na plan B, na ni lipi bora hasa mtoto wa ndugu au adoption, option zote inategemea matokeo unayoyatarajia kutokana na maamuzi yako

1.Ukiwa unataka tu kulea na kusaidia ndugu wanaweza kuwa option nzuri, ingawa option hii inachangamoto ya kuingiliwa na familia husika ya ndugu, na ukiwa na ndugu wa lawama inaeeza kukuweka ktk mazingira magumu( Nimeongea kwa kuzingazia evidence nilizoziona), hii option huwa naiona ni nzuri ukiwa na mtoto mmoja au wawili then ukawa na ndugu wa kusaidia, ila tegemea mtoto anaweza kuondolewa ktk familia yako muda wowote.

2.Option ya kuadopt binafsi naiona nzuri zaidi, kwanza unampa fursa mtoto ambaye angeweza kukulia ktk vituo vya watoto yatima ambavyo sio mazingira rafiki sana ya makuzi, pili unapata fursa ya kumlea kulingana na mnavyoona inafaa, kwa namna yenu na imani yenu, na huyu mtoto mtakuwa naye maisha yenu yote tofauti na ndugu.
Changamoto za kuingiliwa ktk malezi hazipo, na mtoto anakuwa akitambua kuwa nyie ndio wazazi wake.
Kwangu hii ni better option
Naunga mkono hoja hii ya ku adopt badala ya kulea mtotot wa ndugu. Kulea mtoto wa ndugu ni kazi sana, mtoto bado ataendelea kukuona wewe sio mzazi wake hata ukimuwezesha kupata mafanikio bado atakwenda kuwasaidia zaidi wazazi wake kuliko wewe. Na mara zote wazazi wa mtoto unayemlea huwa hawaamini kuwa unamlea vizuri mtoto.
 
Kulea ndugu/mtoto wa ndugu ni lawama sana mwisho wa siku wanakuona takataka tu hata simu hawakupigii.Ndugu saidia wakiwa kwao huko utaumia kiuchumi lakini hutopata kero zao na za wazazi wao. Ni bora adoption unalea bila ya lawama ya kiumbe chochote.
 
Zote sawa ila nilisaidia watoto wa ndugu nikawa ninawalipia ada na kuhudumia elimu. Nilisafiri na mawasiliano yakawa mabovu, Christmas ikafika sijatuma pesa ya shopping. Wasianze kulalamika mtu mwenyewe hana mtoto sijui pesa anapeleka wapi. Nilisononeka lakini nilijikaza wakamaliza shule na kuagana nao
Pole sana
 
Kaka ndugu wana maneno ya maudhi sana, hasa pale mtoto wao utakapomuweka sehemu fulani ambayo wao wasingeweza kimaisha. Kuasili ni vizuri sana ila nenda ukaasili nchi nyingine maana binadamu hawachelewi kuja kusema huyo ni mwanangu na ninamtaka baada ya kuona amekuwa mwenye mafanikio. Haya tumeyashuhudia but kwa mimi sitochagua njia yoyote kati ya hizo kwa kuwa kuwa na mtoto au kutokuwa naye sio dhambi as long as Jongoo anawika mambo ni saaaafi kabisa.
Huyu ni mimi maana sipendi kelele ndani ya nyumba. Pesa ikiwepo hutokosa wa kukuuguza wala kuongea nae, hayo mambo ya kuasili ni magumu kidini na kiserikali, usipofuata vigezo na Masharti utamuudhi Mungu pia.
 
Back
Top Bottom