Kipi ni bora kwenda a-level au college?

College kwenda kusomea nini na A -level kusoma combination gani?
 
College lazima kwanza uwe umefaulu vizuri masomo ya sayansi,na ni nzuri sana maana inakupa njia nzuri ya kuanza maisha vizuri maana kama hutafaulu vizuri diploma ya college basi unaingia mtaani ukiwa na professional yako so utapata kazi kama fundi mchundo na ukifauli yaani ukiwa na GPA nzuri basi unaendelea na Beng kwa college nyingi kama DIT,Arusha Tech na hata Mbeya sasa ila ukienda A-level lazima ufaulu ili uweze kwenda chuo na ukifeli inakula kwako maana huna ujuzi wa kukuwezesha kupatya ajira popote maana hujasomea professional yeyote so unarudi mtaani kama aliyemaliza form four
so uchaguzi upo mikononi mwako
 
Kabla ya kujibu ulipaswa useme mambo mawili (1) Una nini? (2) Unaenda wapi?

(1) Una nini? Matokeo yako yako je? Uwezo wako kiuchumi uko je?
(2) Kwenye maisha una malengo ya kufika wapi au umedhamiria kuwa nani? Kuajiriwa & wapi & muda gani. Kujiajiri kwenye nini n.k.
 
Option ipi ni rahc na marketable kati ya kwenda a level au kwenda college?,waungwana nisaidieni.

Bora ukae nyumbani kuuza sambusa...! Mtiririko wa elimu ni kuwa ni wajibu kupitia A-level, sasa hao wanaoshindwa kufika A-level ni kwa vile uwezo wao ni mdogo sio by choice i.e. badala ya kupanda ferry ya Magufuli pale magogoni ww unajitupa kwenye maji kuogelea ili uvuke; halafu unataka kulinganisha hayo mawili
 
nenda A-LEVEL haraka, siku hizi principal mbili tu (2E's) uko university, tofauti na enzi zetu.
 
Nenda advance elimu ya diploma itakufanya uwe dhaifu kabisaaaaa kasome advance hizo diploma za wazembe
 
Mkuu hebu kasome A-level faster bila kupoteza wakati huko college, piga hata HKL HGL PCM sawa tu lakin hakikisha comb utayoisoma unahimudu vyema ili upate kugusa tu chuo kirahisi.
 
Nataka nikuhakikishie Collage ni bora kuliko A-level hasa vyuo vya technical na hawachukui vilaza ukitoka hapo wewe sio wa kawaida ni fully utaalamu wengi vyuoni wanaenda kukalili ni hakuna ujuzi asikudanganye mtu Technical ni noma ukimaliza Dip ukasoma na BEng hakuna mtu ataguza hapo
 
nataka nikuhakikishie collage ni bora kuliko a-level hasa vyuo vya technical na hawachukui vilaza ukitoka hapo wewe sio wa kawaida ni fully utaalamu wengi vyuoni wanaenda kukalili ni hakuna ujuzi asikudanganye mtu technical ni noma ukimaliza dip ukasoma na beng hakuna mtu ataguza hapo
uongo mtupu
 
Basic option ni kuendelea na masomo haijalishi ni marketable au la,kila kitu kitajulikana mbele ya safari kwani uwezo wa kufikiri,kutambua na kuelewa nao ubadilikabadilika kulingana na mazingira.Unapotumia neno marketable hapa napata tabu kidogo kwani yawezekana wewe unahiitaji elimu fulani kama cheti cha pesa na si elimu kama elimu yenyewe inavyotaka.Kwa tafsiri hii ndio maana wapo watu ambao wanaogopa kuitafuta elimu kwa jasho lao wenyewe bali kutwa nzima kubuni namna gani ya kufoji,kununua ama kutumia vyeti vya wenzao.
 
Kijana, kama utakuwa unajiweza kwenye masomo ya sayansi vizuri, mimi nashauri nivizuri tena sana ukajiunga na chuo, hapo itakuwezesha wewe kujiandaa vizuri katika maisha yako yausoni, asikudanganye mtu A-level sawa ni nzuri lakini chuo nibora zaidi kwani ukimaliza kule ukafaulu unaendelea kwenye kuisaka degree yako na nirahisi ukiwa Sirius, lakini A-level ikitokea hukufanya vyema itakula kwako na utakuwa huna thamani tofauti na ambaye hakufanya vyema chuoni! :juggle:
 
dogo, hizo technical college(DIT, MIST & ATC) hata syllabus hawana, wanatumia syl. za urusi za 1970's usiende mwaya.
 
dogo, hizo technical college(DIT, MIST & ATC) hata syllabus hawana, wanatumia syl. za urusi za 1970's usiende mwaya.


kama hujui usiandike chochote. syllabus zipo tena chini ya NACTE na uzuri vyuo vyote vinatoa kuanzia NTA 4-8 yaani diploma NTA 6,higher National Diploma NTA 7 na Bachelor NTA 8
 
Kijana, kama utakuwa unajiweza kwenye masomo ya sayansi vizuri, mimi nashauri nivizuri tena sana ukajiunga na chuo, hapo itakuwezesha wewe kujiandaa vizuri katika maisha yako yausoni, asikudanganye mtu A-level sawa ni nzuri lakini chuo nibora zaidi kwani ukimaliza kule ukafaulu unaendelea kwenye kuisaka degree yako na nirahisi ukiwa Sirius, lakini A-level ikitokea hukufanya vyema itakula kwako na utakuwa huna thamani tofauti na ambaye hakufanya vyema chuoni! :juggle:

mkuu kama ulishindwas wewe A level basi msaidie mwenzako na sio kumdanganya ili aende kusoma syllabus za urusi za mwaka 1970 huko college.
 
mkuu kama ulishindwas wewe A level basi msaidie mwenzako na sio kumdanganya ili aende kusoma syllabus za urusi za mwaka 1970 huko college.

Mkuu Kishalu keshakujibu, sikweli kwamba vyuovyetu tuponyuma kiasi chakutokwenda na wakati, kumbuka kuwa hapa unamsaidia mtu ili aweze weka mambo sawa. Hivyo basi nibora uwe nahakika ya uyasemayo.
 
Back
Top Bottom