Haya ni mawazo yangu tu wanajamii!!
Inawezekana wakawepo wengi tu katika CCM wanaoutolea mate urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya JK. Miongoni mwao ni Edward Lowassa, Samwel Sitta na Ben Membe. Kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitoa kauli zinazoonesha nia yao hiyo.
Katika mihadhara yao wanayoifanya aidha kwa kuitwa au wao wenyewe kuita watu wamekuwa wakiongelea mambo mengi yanayohusu mustakabali wa Taifa letu.
Lakini unapochaambua sana mambo ambayo huwa wanayaongelea utabaini kuwa Edward Lowassa amewazidi sana wanasiasa wenzake wa CCM(Kwa muktadha wa uchambuzi huu Samweli Sitta na Ben Membe)
Kwa upande wa Lowassa kila anapopata nafasi ya kuongea na wananchi amekuwa akionesha uwezo mkubwa wa kubuni na kutanabaisha njia ya nini kifanyike katika kulijenga Taifa(Sijui kama anachokisema kinatoka moyoni au lengo ni kupata populality), ila kwa kuwa waswahili wanasema kimtokacho mtu mdomoni ndicho kilichopo moyoni hatuna budi kuamini kuwa anayoyasemaa Lowassa ndiyo yaliyopo moyoni mwake.
Lowassa mara kwa mara amekuwa akiongelea suala la ajira kwa vijana na alifika mbali hata kuyaomba mashirika ya dini na ya binafsi kuanza kujenga shule na vyuo vya ufundi ambavyo vitawafundisha vijana fani mbalimbali ambapo mara baada ya kuhitimu wanaweza kujiajiri wenyewe kama siyo kuajiriwa.
Lowassa pia amekuwa akisisitiza suala la elimu bora. Amewahi kuongelea kuhusu kuundwa kwa tume ambayo itafanya uchambuzi wa mfumo wa elimu kama unaendana na mazingira ya sasa na kama itabainika kuwa hauendanibasi mfumo huo ufumuliwe na kusukwa upya(Haya aliyasema katika mahafali ya shule ya Benjamini Mkapa, Dar)
Lowassa akiwa katika harambee ya kuchangia Saccos ya walimu mjini Moshi ameelezea kuwa anayo ndoto kuwa siku moja Elimu kwa watoto wa kitanzania itakuwa bora na maisha yaa mwalimu yatakuwa bora. Na hapa nahusianisha na kauli mbiu yake Kilimo kwanza, Elimu kabla. Akiwa na maana, kama kilimo ni chapter one, basi elimu ni Preamble.
Lakini pia Lowassa amekuwa akikwepa sana kulumbana na wanasiasa wa ndani ya chama chake na hata nje ya chama chake(achilia mbali kauli katika majukwaa ya siasa). Sijawahi kumsikia Lowassa akiwatupia vijembe wapinzani wake (wa ndani ya chama chake au nje ya chama chake) kuwa hawastahili kuwa viongozi.
Kwa upande wa Samweli Sitta na Ben Membe, wamekuwa wakiongelea kero za wananchi kwa kiwango kidogo sana hata kuwa vigumu kujua wamesimamia wapi. Kila wanapopata upenyo wamekuwa wakilalamika na kurusha matope na kejeli kwa mahasimu wao wa kisiasa. Kila Sitta atakapoalikwa au atakapoalika watu ataongelea suala la uchaguzi wa 2015 na alivyotendwa kwa kunyang'anywa uspika wake. Muda wote utamsikia "mimi nimefanya kazi na Nyerere. Msifanye makosa mkampa kura mtu ambaye si muadilifu".
Membe pia wimbo ni huo huo. Hawaoneshi ubunifu wa namna ya kutatua matatizo ya watanzania ili tuweze kuwapa credity. Kama hawatamsema Lowassa katika namna ya mafumbo(wanasheria wanaita innuendo) basi wataingia katika malumbano yasiyo na maana na watani wao wa Chadema.
Kwa haya machache naamini Lowassa yupo mbele ya Samweli Sitta na Ben Membe kwa zaidi ya maili nyingi sana.
Wasalaam
Inawezekana wakawepo wengi tu katika CCM wanaoutolea mate urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya JK. Miongoni mwao ni Edward Lowassa, Samwel Sitta na Ben Membe. Kwa nyakati tofauti wamekuwa wakitoa kauli zinazoonesha nia yao hiyo.
Katika mihadhara yao wanayoifanya aidha kwa kuitwa au wao wenyewe kuita watu wamekuwa wakiongelea mambo mengi yanayohusu mustakabali wa Taifa letu.
Lakini unapochaambua sana mambo ambayo huwa wanayaongelea utabaini kuwa Edward Lowassa amewazidi sana wanasiasa wenzake wa CCM(Kwa muktadha wa uchambuzi huu Samweli Sitta na Ben Membe)
Kwa upande wa Lowassa kila anapopata nafasi ya kuongea na wananchi amekuwa akionesha uwezo mkubwa wa kubuni na kutanabaisha njia ya nini kifanyike katika kulijenga Taifa(Sijui kama anachokisema kinatoka moyoni au lengo ni kupata populality), ila kwa kuwa waswahili wanasema kimtokacho mtu mdomoni ndicho kilichopo moyoni hatuna budi kuamini kuwa anayoyasemaa Lowassa ndiyo yaliyopo moyoni mwake.
Lowassa mara kwa mara amekuwa akiongelea suala la ajira kwa vijana na alifika mbali hata kuyaomba mashirika ya dini na ya binafsi kuanza kujenga shule na vyuo vya ufundi ambavyo vitawafundisha vijana fani mbalimbali ambapo mara baada ya kuhitimu wanaweza kujiajiri wenyewe kama siyo kuajiriwa.
Lowassa pia amekuwa akisisitiza suala la elimu bora. Amewahi kuongelea kuhusu kuundwa kwa tume ambayo itafanya uchambuzi wa mfumo wa elimu kama unaendana na mazingira ya sasa na kama itabainika kuwa hauendanibasi mfumo huo ufumuliwe na kusukwa upya(Haya aliyasema katika mahafali ya shule ya Benjamini Mkapa, Dar)
Lowassa akiwa katika harambee ya kuchangia Saccos ya walimu mjini Moshi ameelezea kuwa anayo ndoto kuwa siku moja Elimu kwa watoto wa kitanzania itakuwa bora na maisha yaa mwalimu yatakuwa bora. Na hapa nahusianisha na kauli mbiu yake Kilimo kwanza, Elimu kabla. Akiwa na maana, kama kilimo ni chapter one, basi elimu ni Preamble.
Lakini pia Lowassa amekuwa akikwepa sana kulumbana na wanasiasa wa ndani ya chama chake na hata nje ya chama chake(achilia mbali kauli katika majukwaa ya siasa). Sijawahi kumsikia Lowassa akiwatupia vijembe wapinzani wake (wa ndani ya chama chake au nje ya chama chake) kuwa hawastahili kuwa viongozi.
Kwa upande wa Samweli Sitta na Ben Membe, wamekuwa wakiongelea kero za wananchi kwa kiwango kidogo sana hata kuwa vigumu kujua wamesimamia wapi. Kila wanapopata upenyo wamekuwa wakilalamika na kurusha matope na kejeli kwa mahasimu wao wa kisiasa. Kila Sitta atakapoalikwa au atakapoalika watu ataongelea suala la uchaguzi wa 2015 na alivyotendwa kwa kunyang'anywa uspika wake. Muda wote utamsikia "mimi nimefanya kazi na Nyerere. Msifanye makosa mkampa kura mtu ambaye si muadilifu".
Membe pia wimbo ni huo huo. Hawaoneshi ubunifu wa namna ya kutatua matatizo ya watanzania ili tuweze kuwapa credity. Kama hawatamsema Lowassa katika namna ya mafumbo(wanasheria wanaita innuendo) basi wataingia katika malumbano yasiyo na maana na watani wao wa Chadema.
Kwa haya machache naamini Lowassa yupo mbele ya Samweli Sitta na Ben Membe kwa zaidi ya maili nyingi sana.
Wasalaam