Sita na Membe ni watu wa visasi na wapo kambi moja na Mwigulu na Nape, Mh Lowasa ni mtu mwenye busara na hana mambo ya visasi
MwiguluHawa wote lao moja na pia mkumbuke kuwa JK was thought to be THE LAST TRUSTED PRESDENT FROM NYINYIEM. Lowasa naye hafai kabisa, Leo Nasari kala kipondo kibaya Makuyuni Arusha unafikiri waliompiga walitumwa na nani?
Watajwa wote hapo wanatofautiana kwa nyanja nyingi lakini wanaunganishwa na CCM hivyo kuwaondelea utofauti.
Tunahitajika kujikomboa kifikra ili kuondokana na mawazo mgando kuwa lazima wagombea watoke CCM.
Kuna Watanzania wenye uwezo na sifa lakini tumejikita kuwa jadili watu ambao hawawezi kuiokoa nchi hii katika kipindi kama hiki.
Tutumie milango yote ya fahamu, kujifungua toka minyororo ya fikra finyu na tutazame mbele juu ya mstakabali wa nchi yetu kwa mapana tuone watu wanaoweza kuikomboa nchi hii na ikiwezekana tuwaombe waiongeze nchi,kuliko hao ambao wanandoto ya kuitawala nchi kwa lengo la kuneemesha jamii zao na kuiacha nchi taabani.
Kwa vipindi walivyotumikia nchi hii maisha ya watanzania baada ya miaka 50 ya uhuru bado yapo duni na hii ni kutokana na mchango wao kwa vipindi wakiwa kwenye madaraka makubwa.Wamechangia nini?
Ni busara wakae pembeni wastaafu na kuwaachie wengine wapate nafasi ya kuiokoa nchi hii mahali walipofikisha.