Kipi kimesababisha bei za mafuta kupaa hivi?

Bei imezidi kupanda maradufu
Screenshot_20210602-231009_Truecaller.jpg
 
90
Umenikumbusha huu mchezo walicheza na kuimba watoto zamani...

Eee moja moja embassy
Eee mbili mbili embassy
Eee tatu tatu embassy
Eee nne nne embassy....

Inaendelea hivyo hadi kumi halafu sauti inapanda...😅

Wewe wa ngapi...!??
90's
 
Kwa waziri huyu wa fedha.
Tutachapisha noti ya laki moja na milioni moja ndani ya hii mitano ya SSH.
Zimbabwe ilianza hivi hivi, mtu anaharibu wilayani anapandishwa kua mtawala wa mkoa. Wabunge COVID 19 Hawakemewi ilhali kila mtu anajua Sabufa mbovu.
 
Kwa waziri huyu wa fedha.
Tutachapisha noti ya laki moja na milioni moja ndani ya hii mitano ya SSH.
Zimbabwe ilianza hivi hivi, mtu anaharibu wilayani anapandishwa kua mtawala wa mkoa. Wabunge COVID 19 Hawakemewi ilhali kila mtu anajua Sabufa mbovu.
Hahahah waziri anakula ndumu
 
Huko uliko bei ya mafuta ya petrol ni Tsh ngapi? Hali imeanza kuwa Tete baada ya kupanda Kwa bei ya mafuta. Hali ikiendelea hivi, tutamkumbuka Magufuli mara kumi . Serikali isipo angali Jambo hili tunaelekea kusiko julikana .
Tuondolee mawazo mgando hapa! Jiwe ndiye alikuwa anapanga bei ya petroli duniani? Mafuta yalikuwa yanachimbwa chato au? Labda uniambie kuwa yeye ndiye alileta corona ikadisturb uchumi wa dunia hadi mafuta yakashuka vile
 
Ikifika December $1=Tzs 3,000 Lita moja 3,000
Dollar inasumbua dunia nzima huko SA ilikua $1 =15rand sasa hivi imekomaa mpaka rand 12 siku ingine rand 13 kwa dollar moja mafuta na wao wanatengeneza mengine kwa kutumia makaa ya mawe yamepanda mara mbili zaidi mpaka sisi wanunua bidhaa huko imetutingisha kidogo swala la dollar na mafuta ni mfumuko wa Dunia sio Bongo tuu..
 
Wakuu hivi hii hali inaelekea wapi? Kulingana na bei mpya kuna baadhi ya mikoa lita ya petrol imefika 2480. Ni kweli huko duniani mafuta yamepanda au hapa kwetu tu tunakomoana.

Je ni halali nauli kuendelea kubaki pale pale? Au tutegemee ongezeko huko mbeleni.

Huko tunakoenda nadhan kuna watu wataenda kupaki magari yao, mimi leo 20k nimeambulia lita 8 na point nikabak nashangaa kumbe bei zishapaa.
Gharama za usafirishaji si mafuta pekee, nauli hazitapanda
 
Mbona kama mnalazimisha Magufuli akumbukwe?kwamba angekuwepo yeye angefanyaje?vitu vungapi vimepanda bei tangu aingie mafarakani mpaka anakufa havijawai kushuka bei?
 
Back
Top Bottom