Kipi kifanyike ili kutibu ama kuondoa tatizo la chumvi majumbani?

King Rabbit

JF-Expert Member
Mar 29, 2015
736
2,672
Ushauri, maoni yote yanakaribishwa kwa yeyote mwenye mawazo chanya katika kuondoa au kumaliza tatizo la chumvi majumbani kwetu.

1. Mimi ni mkazi wa Dodoma(Ilazo) na kwa bahati mbaya sana nyumba nyingi wanahangaika na hii kitu na ina tabia ya kula sana maeneo ambako kwa kawaida kuna matumizi makubwa ya maji mfano chooni,bafuni.

2.Kwa bahati mbaya chumvi imetafuna nyumba yangu ambayo ilikuwa imeshapigwa skimming tayari kiasi kwamba naogopa hata kupiga rangi nahisi nitakuja kutia huruma baada ya muda mfupi.

3. Picha zifuatazo hapo chini ni picha halisi za matokeo ya chumvi.

#Karibuni kwa maoni na ushauri.

IMG20210331121013.jpg
IMG20210331082558.jpg
IMG20210331121138.jpg
IMG20210331121211.jpg


IMG20210331082542.jpg
 
Pole sana kiongozi.
Angalia ni kwa namna gani msingi wako unaingiza maji,maana tulikuja gundua kuwa maji yakizidi katika eneo,huanza kupanda juu ya nyumba na kusababisha hali hiyo.
Hatua tulizo chukua ni kuweke hata,pia kuzungusha peeving kuzunguka nyumba au kumwaga zege kuzunguka nyumba,lengo likiwa ni kuzuia maji kutokupanda juu.
Baada ya kuona hali hiyo ilibidi tupige cigar kuzuia ukuta kuoza zaidi.
 
Pole sana kiongozi.
Angalia ni kwa namna gani msingi wako unaingiza maji,maana tulikuja gundua kuwa maji yakizidi katika eneo,huanza kupanda juu ya nyumba na kusababisha hali hiyo.
Hatua tulizo chukua ni kuweke hata,pia kuzungusha peeving kuzunguka nyumba au kumwaga zege kuzunguka nyumba,lengo likiwa ni kuzuia maji kutokupanda juu.
Baada ya kuona hali hiyo ilibidi tupige cigar kuzuia ukuta kuoza zaidi.
Asante mkuu,na baada ya kufanya hivyo tatizo lilisha kabisa???
 
Waona hawa jamaa..wanatibu hilo tatizo na hutoona tena likijirudia

NORPAD GS CO.
+255 753 318 131
 
Umejenga kwenye ardhi yenye chumvi. Chimba mtaro urefu wa mita moja na nusu kuzunguka nyumba. Jenga mtaro wa upana wa nusu mita kuzunguka nyumba huku upande wa ndani ukiacha matobo ili yanyonye maji yasipande kwenye nyumba. Maji yanayokuwa drained yaelekeze kwenye karo maalum kwa maji ya chumvi.
 
Hali hii ya Chumvi kula ukuta, hujitokeza sana kwenye kuta za Bafu au vyoo vya ndani.

Suluhisho: Weka tiles kwenye kuta zote za Bafu na choo cha ndani.
 
Umejenga kwenye ardhi yenye chumvi. Chimba mtaro urefu wa mita moja na nusu kuzunguka nyumba. Jenga mtaro wa upana wa nusu mita kuzunguka nyumba huku upande wa ndani ukiacha matobo ili yanyonye maji yasipande kwenye nyumba. Maji yanayokuwa drained yaelekeze kwenye karo maalum kwa maji ya chumvi.
Hapa kwenye karo siwezi kuelekeza kwenye karo la maji taka??
 
Hali hii ya Chumvi kula ukuta, hujitokeza sana kwenye kuta za Bafu au vyoo vya ndani.

Suluhisho: Weka tiles kwenye kuta zote za Bafu na choo cha ndani.
Ndani bafuni pamoja na chooni nmepiga tiles pako safi kabisa shida hapo nje,pako kama jinsi panavyoonekana.
 
Pole sana kiongozi.
Angalia ni kwa namna gani msingi wako unaingiza maji,maana tulikuja gundua kuwa maji yakizidi katika eneo,huanza kupanda juu ya nyumba na kusababisha hali hiyo.
Hatua tulizo chukua ni kuweke hata,pia kuzungusha peeving kuzunguka nyumba au kumwaga zege kuzunguka nyumba,lengo likiwa ni kuzuia maji kutokupanda juu.
Baada ya kuona hali hiyo ilibidi tupige cigar kuzuia ukuta kuoza zaidi.
Problem ilikuwa solved mkuu???!
 
Back
Top Bottom