Kipi chao.... Kipi chetu!?

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
kila jamii ina taratibu zake na mifumo yake ya jinsi ya kuishi. Haya yafuatayo ni mambo ambayo nadhani kwamba yanagawanyika katika jamii ni yepi ya kufanywa na wanaume au wanawake na yepi ni majukumu ya nani kwenye familia na ni zipi ni haki za nani kwenye familia. Tupe mawazo yako kwako yamekaaje.

1. Kumiliki mali za familia ni haki ya nani?

2. Kutoa na kuosha vyombo baada ya kula ni wajibu wa nani?

3. Kubadilisha na kufua nepi za mtoto ni kazi ya nani?

4. Kutandika Kitanda ni shughuli ya nani?

5. Kufagia chumba/Nyumba nani afanye?

6. Kulipia bili mbali mbali kama za maji na Umeme yupi atoe hela yake?

7. Kulipia karo za watoto shuleni pamoja na matumizi yao ni nani awajibike?

8. Kufua nguo za wawili (Wenza) nani hasa anahusika?

9. Haki ya kutoa talaka kila mmoja anayo au ni ya jinsia moja tuu?

10. Watoto majina ya ukoo wachukue kwa nani, baba au mama?

11. Kanuni za jinsi ya kuishi ndani ya nyumba ziwekwe na nani? Mume au mke, ama wote wawili?

Haya ni mambo yanayotofautiana kati ya watu na watu na jamii na jamii lakini sisi kama wana MMU tunayaonaje?
 
kila jamii ina taratibu zake na mifumo yake ya jinsi ya kuishi. Haya yafuatayo ni mambo ambayo nadhani kwamba yanagawanyika katika jamii ni yepi ya kufanywa na wanaume au wanawake na yepi ni majukumu ya nani kwenye familia na ni zipi ni haki za nani kwenye familia. Tupe mawazo yako kwako yamekaaje.

1. Kumiliki mali za familia ni haki ya nani?

2. Kutoa na kuosha vyombo baada ya kula ni wajibu wa nani?

3. Kubadilisha na kufua nepi za mtoto ni kazi ya nani?

4. Kutandika Kitanda ni shughuli ya nani?

5. Kufagia chumba/Nyumba nani afanye?

6. Kulipia bili mbali mbali kama za maji na Umeme yupi atoe hela yake?

7. Kulipia karo za watoto shuleni pamoja na matumizi yao ni nani awajibike?

8. Kufua nguo za wawili (Wenza) nani hasa anahusika?

9. Haki ya kutoa talaka kila mmoja anayo au ni ya jinsia moja tuu?

10. Watoto majina ya ukoo wachukue kwa nani, baba au mama?

11. Kanuni za jinsi ya kuishi ndani ya nyumba ziwekwe na nani? Mume au mke, ama wote wawili?

Haya ni mambo yanayotofautiana kati ya watu na watu na jamii na jamii lakini sisi kama wana MMU tunayaonaje?




in red aweke mke ndo inapendeza
 
Back
Top Bottom