May Day
JF-Expert Member
- May 18, 2018
- 6,162
- 8,820
Wengine huita 'mood swing'
Kwa watu wazima wote nadhani tayari tuna uzoefu wa kuishi Wawili chini ya paa moja kwa muda, kama wenza, Mke na Mume, huku wote mmekutana mkiwa na historia tofauti za kimalezi.
Sasa je, kipi bora kati ya Watu wa aina hizo mbili. Yaani Mwenza wa kujichanganya sana na Marafiki, simu yake ipo bize muda mwingi...lakini akifika nyumbani anaamshaamsha, ana maneno mazuri, matamu...ukimwambia unajisikia vibaya ana "react" hapohapo...atampigia dokta au atakimbia duka la dawa...au kama ni kuandaa dawa asili(home remedy) ataingia jikoni hapo hapo bila kujiuliza mara mbili.
Au uwe na mwenza mtiifu wa ndoa, ambaye akitoka tu kazini breki ya kwanza nyumbani, lakini ndio hata akikukuta kitandani hakuulizi kulikoni...ukimwambia unaumwa akijitahidi sana atakuuliza "umeshaenda hospitali?" zaidi ya hapo atatulia tuli kwenye kochi asubiri msosi akalale.
Kwa watu wazima wote nadhani tayari tuna uzoefu wa kuishi Wawili chini ya paa moja kwa muda, kama wenza, Mke na Mume, huku wote mmekutana mkiwa na historia tofauti za kimalezi.
Sasa je, kipi bora kati ya Watu wa aina hizo mbili. Yaani Mwenza wa kujichanganya sana na Marafiki, simu yake ipo bize muda mwingi...lakini akifika nyumbani anaamshaamsha, ana maneno mazuri, matamu...ukimwambia unajisikia vibaya ana "react" hapohapo...atampigia dokta au atakimbia duka la dawa...au kama ni kuandaa dawa asili(home remedy) ataingia jikoni hapo hapo bila kujiuliza mara mbili.
Au uwe na mwenza mtiifu wa ndoa, ambaye akitoka tu kazini breki ya kwanza nyumbani, lakini ndio hata akikukuta kitandani hakuulizi kulikoni...ukimwambia unaumwa akijitahidi sana atakuuliza "umeshaenda hospitali?" zaidi ya hapo atatulia tuli kwenye kochi asubiri msosi akalale.