konda msafi
JF-Expert Member
- Sep 5, 2018
- 1,666
- 8,523
Hivi hapa duniani kipi ni kitu cha fahari zaidi kati ya kuwa mwanasiasa na kufikia mafanikio ya kuwa waziri au rais kabisa, na kuwa mfanyabiashara bilionea kama alivyokuwa Mengi au Mohamed Dewji (Mo)?
Kuwa kiongozi wa kiasa kuna raha yake, kusafishiwa njia na ving'ora kwa pembeni ukiwa unapita, ulinzi wa kutosha wa TISS, polisi na jeshi, nchi nzima inakujua na full heshima, ukitoa amri kila mtu anatekeleza.
Ukiwa bilionea level ya akina Mo au Bill Gates nako kuna raha yake, full kula bata na kuenjoy life unavyotaka maana pesa sio tatizo kwako. Sasa huwa najiuliza hapa duniani kati ya hivi vitu viwili, kipi kinachokupa ufahari wa hali ya juu.
Kumbuka Mo na mihela yake alitekwa ila mwanasiasa kama waziri au rais sio rahisi kumteka. Pia kumbuka mwanasiasa kuna kustaafu baada ya muda na kuuacha huo utukufu wote wa madaraka, lakini mfanyabiashara haina kustaafu ni kuponda raha hadi kufa labda ufirisike. (Bill Gates hawezi kufirisika).
Kuwa kiongozi wa kiasa kuna raha yake, kusafishiwa njia na ving'ora kwa pembeni ukiwa unapita, ulinzi wa kutosha wa TISS, polisi na jeshi, nchi nzima inakujua na full heshima, ukitoa amri kila mtu anatekeleza.
Ukiwa bilionea level ya akina Mo au Bill Gates nako kuna raha yake, full kula bata na kuenjoy life unavyotaka maana pesa sio tatizo kwako. Sasa huwa najiuliza hapa duniani kati ya hivi vitu viwili, kipi kinachokupa ufahari wa hali ya juu.
Kumbuka Mo na mihela yake alitekwa ila mwanasiasa kama waziri au rais sio rahisi kumteka. Pia kumbuka mwanasiasa kuna kustaafu baada ya muda na kuuacha huo utukufu wote wa madaraka, lakini mfanyabiashara haina kustaafu ni kuponda raha hadi kufa labda ufirisike. (Bill Gates hawezi kufirisika).