Kipi bora: Kusoma ukijua hakuna ajira au kuacha kusoma

Umomi

JF-Expert Member
Mar 31, 2020
677
983
To be honest, hakuna kitu kinaumiza graduates nikiwemo mimi kama kusoma huku nikijua kabisa ajira ni ya kusotea sana. Nikipiga mahesabu pesa niliyotumia kusomea chuo kikuu Ni zaidi ya 9.5m ilikuwa inatosha kujiajiri. Naumia sana ila sina cha kufanya. Najua wengi mtahuji kuwa nilisaini mkataba wa kuajiriwa baada kumaliza kusoma.

Jibu ni kwamba kujiajiri naweza sana lakini tayari nimetumia pesa na kupoteza muda mwingi sana kusoma masomo ya chuo kikuu. Yani bora ningeishia form nikafanya mishe mishe make haya maisha niliyaona kipindi cha Corona ni MAGUMU nilikuwa napiga biashara ndogo ndogo ila hali ni ngumu sana. Niseme ukweli kabisa nilianza biashara kwama tarehe 28/3/2020 ila mpaka tunafungua vyuo sikuwahi kupata Faida 20000 kwenda juu kwa siku. Nakumbuka siku nimepata faida kubwa sana nilipata 14500 but siku zingine nilikuwa naishia 4000 mpaka 10500.

Jamani Mimi Kama mhitimu wa Elimu ya juu siyo kwamba sipendi kujiajiri napenda sana lakini mtaani Ni kugumu sana, niseme ukweli kabisa nawaza sana. Ila kinachoniumiza zaidi n kwenda kuanza upya baada ya kumaliza kusoma na umri umesonga sana hivyo hata kwenda kukaa nyumbani ama kwa ndugu naona aibu sana. Mi nimesoma ualimu wa Elimu ya msingi (Bachelor of Education in Primary Education). Naomba hata mwenye connection na shule anifanyie mpango kweli hata nikaanze maisha jmn. Mtaji nimejichanga ila naona hautoshi kwa plani zangu.

Naomba kuwasilisha
 
‘Bachelor Of Education In Primary Education’

Kuna hii Degree Program kweli ??
 
Mkuu hebu punguza tamaa kidogo, yaani uliweza kufikia faida ya elfu 10 kwa siku alafu unasema hukuwahi kuona faida? Hivi unadhani wanaovuna milion kwa siku walianza wanavuna hizo pesa kwa siku? Naona unatamani ajira, sasa nakuombea siku moja upate ajira uone kama hiyo elf kumi kwa siku itapatikana ukigawa mshahara wako kwa siku 30
 
Yani hata chuo ujamaliza unakata tamaa kijana vipi bwana life is gambling usiogope wewe tunza afya heshimu watu alafu usiwe na usongo sana na Maisha wewe tulia ila pambana fursa inapojitokeza usisite jaribu
 
Yani hata chuo ujamaliza unakata tamaa kijana vipi bwana life is gambling usiogope wewe tunza afya heshimu watu alafu usiwe na usongo sana na Maisha wewe tulia ila pambana fursa inapojitokeza usisite jaribu
Mkuu life linatisha sana
 
Mkuu hebu punguza tamaa kidogo, yaani uliweza kufikia faida ya elfu 10 kwa siku alafu unasema hukuwahi kuona faida? Hivi unadhani wanaovuna milion kwa siku walianza wanavuna hizo pesa kwa siku? Naona unatamani ajira, sasa nakuombea siku moja upate ajira uone kama hiyo elf kumi kwa siku itapatikana ukigawa mshahara wako kwa siku 30
Mkuu siyo kwa nilikuwa napa elfu 10 kila siku hapana kuna siku nilikuwa napata hata 4500 niwe tu mkeli. Ila Kuna siku zilikuwa zikienda vzr unapata mpaka 8000 au elfu 10 au zaid
 
Mkuu life linatisha sana
Usiogope kila mtu yupo hapa duniani kuwa sababu na ukitaka kujua kwanini upon duniani na mungu ana sababu na wewe angalia Maisha katika pande zote usiangalie upande mmoja kinachokutesa wewe unangalia Maisha katika upande wa mafanikio tu hivyo unajawa na hofu kwanini ukiangalia mbele unaona kiza amino nakwambia Furaha ya Maisha ipo katika upande nyingi sana

Uzima ulionao ni mafanikio tayali yakimaisha ukitizama upande wa wagonjwa waliolala kitandani hawaitaji utajiri wanaitaji uzima tu

Uhuru wa akili na kimazingira ni mafanikio tayali huwezi kuwaza unachowaza sasa ukiwa gerezani mfungwa anatamani Uhuru tu mengine hana mpango kwaiyo usipanic relax Maisha yana maajabu Mengi sana ukiwa na panic unaweza kosa vyote na ukapoteza hata ulichonacho

Mche mungu uku ukiamini siku yako ipo uku unapambana believe me Sikh itafika hizi changamoto zipo usiogope
 
Mtaani ni kugumu kweli itabid ukaze , std 7 wapo kibao wametusua why not you, degree holder? Be creative, just come up with your solution to solve the society 's challenges, and then it's will be your an opportunity.

Wewe zao la kombolera na Ukuti wa meme.

Binafsi wagonjwa wa Ukimwi na Corona nawaonaga mitandaoni na kwenye TV ila hivi live sijawai kumuona huyu ana HIV/AIDS huyu Corona.

Hivyohivyo STD 7 waliotoboa nawashuhudia kwenye TV na mitandaoni ila ueaiani sijaona STD 7 aliyetoboa...iko hivi mtaa wowote hapa Tz wasomi ni 2% ya watu wa mtaa mzima kwamaana kutwa mzima unaweza amka ukazunguka mtaa mpaka jioni ukaona wasomi 3 ila waliobaki wote STD 7 hao STD 7 asilimia kubwa 1M ya pamoja hawawezi kuimiliki hawana maisha kabisa sasa kutoboa sijui ikimaanisha nini...kitu pekee labda washatengeneza uhakika wapi wanapata kipato Chao ila msomi akifika mtaani ndio ana Hustle kupata sehemu.

Tz kutoboa kuna njia mbili tu
1)Kuajiriwa (ajira rasmi)
2)kuimiliki Biashara

STD 7 95% hawana hivyo viwili na wengi hawana focus ya kuvipata.
 
Hapa utapewa hamasa uchwara, ushauri, kejeli na pole.

Najua hali unayopitia mkuu, jipe moyo
 
Wewe zao la kombolera na Ukuti wa meme.

Binafsi wagonjwa wa Ukimwi na Corona nawaonaga mitandaoni na kwenye TV ila hivi live sijawai kumuona huyu ana HIV/AIDS huyu Corona.

Hivyohivyo STD 7 waliotoboa nawashuhudia kwenye TV na mitandaoni ila ueaiani sijaona STD 7 aliyetoboa...iko hivi mtaa wowote hapa Tz wasomi ni 2% ya watu wa mtaa mzima kwamaana kutwa mzima unaweza amka ukazunguka mtaa mpaka jioni ukaona wasomi 3 ila waliobaki wote STD 7 hao STD 7 asilimia kubwa 1M ya pamoja hawawezi kuimiliki hawana maisha kabisa sasa kutoboa sijui ikimaanisha nini...kitu pekee labda washatengeneza uhakika wapi wanapata kipato Chao ila msomi akifika mtaani ndio ana Hustle kupata sehemu.

Tz kutoboa kuna njia mbili tu
1)Kuajiriwa (ajira rasmi)
2)kuimiliki Biashara

STD 7 95% hawana hivyo viwili na wengi hawana focus ya kuvipata.
Na huo ndo ukweli, ata Mimi hao wa 7 waliotoboa nawatafuta siwaoni ila kidogo wa form 4 ndiyo wametoboa kiasi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom