kipi bora kusoma bachelor home na kwenda kusoma nje ya nchi

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
nalimwaga hili sababu kuna Afisa mmoja wa serikali kanitisha sana Kuna anaosema kwamba elimu ya nchi za nje haifai kwasababu kuna utofauti mkubwa wa mitaala na ufundishaji kwamba wanafunzi wanaosoma vyuo vikuu hapa bongo wanapiga msuli sana hasa UDSM na waalimu pia wa kibongo quality yao ipo juu sana tofauti na waalimu wa nje ya nchi pia kuna nchi inabidi ujifunze lugha yao mwaka mzima au miaka 2 then uanze bachelor kwa kutumia lugha yao ama kiingereza pia system ya nje masomo ni mengi sana kama shule za msingi ukilinganisha na bongo sasa nimeomba kujua kipi bora kati ya kusoma nje ya nchi au nibaki hapahapa bongo maana nimepata offer ya kwenda kusoma bachelor nje ya nchi ila huko natakiwa nijifunze lugha yao mwaka mzima then ndipo nianze bachelor miaka 4 so kuna Afisa mmoja wa serikari ananishauri kama ni uchumi bora nisome vyuo vya hapahapa bongo!waungawana naombeni ushauri.hasa kwa mliopo vyuo nje ya nchi hasa nchi za Europe.
 
Mr Kilimasera kwangu mimi nioanavo inategema nchi na nchi.kama umepata offer ya kwenda nje nadhani mitala yake imeanishwa ktk website ya chuo hicho ww binasfi angalia ni masomo mangapi wanafundisha kwa semister na kama wanafundisha kiingereza ni poa zaidi usiiache hiyo offer hata kama utasoma lugha yao kwa mwaka mzima,kama ukijituma na kujiibiisha hakuna lisilowezekana.Asikutishe mtu kwa hilo.Lau pia kama umepata adm ya UDSM kusoma bcom sikushauri sana pale tumepiga msuli sana tatizo ni kuwa walimu wanafurahia kukamata badala ya kufurahia wanafunzi kufaulu huu ni ujinga wa walimu wetu wa kibongo.kama umepata chuo kinachotambulika we nenda wala usihofu utapata upeo wa kujifunza mengi zaidi kutoka kwa watu mbalimbali.Cha muhimu ni bidii ktk masomo basi.Wengi wanasema ni vema kusoma digree ya kwana bongo lakini kama umepata nje kwa nn usiende? kazi kwako.Wengi tumesoma bongo kwa kuwa hatukuwa na altenative ya chuo kingine ila kwa wewe ndugu nenda fasta.
 
huyo bosi wako amewahi kusoma nje? Au anaongelea kutokana na masimulizi aliyoyasikia kwa watu?
 
Usiiache hiyo nafasi ya kwenda kusoma nje ikapita bure tu yangu.............achana na vyuo vya bongo kama umepata chuo nje ya nchi, nenda ukasome!
 
nalimwaga hili sababu kuna Afisa mmoja wa serikali kanitisha sana Kuna anaosema kwamba elimu ya nchi za nje haifai kwasababu kuna utofauti mkubwa wa mitaala na ufundishaji kwamba wanafunzi wanaosoma vyuo vikuu hapa bongo wanapiga msuli sana hasa UDSM na waalimu pia wa kibongo quality yao ipo juu sana tofauti na waalimu wa nje ya nchi pia kuna nchi inabidi ujifunze lugha yao mwaka mzima au miaka 2 then uanze bachelor kwa kutumia lugha yao ama kiingereza pia system ya nje masomo ni mengi sana kama shule za msingi ukilinganisha na bongo sasa nimeomba kujua kipi bora kati ya kusoma nje ya nchi au nibaki hapahapa bongo maana nimepata offer ya kwenda kusoma bachelor nje ya nchi ila huko natakiwa nijifunze lugha yao mwaka mzima then ndipo nianze bachelor miaka 4 so kuna Afisa mmoja wa serikari ananishauri kama ni uchumi bora nisome vyuo vya hapahapa bongo!waungawana naombeni ushauri.hasa kwa mliopo vyuo nje ya nchi hasa nchi za Europe.
Ningekuwa mimi ningeenda kusoma kwa hao waalimu vilaza, kama kweli ni vilaza wa nje ya nchi!.
 
Mkuu mi nadhani inategemea mambo mengi,
aina ya chuo, nchi kilipo chuo, mdhamini nk.
Kwa maoni yangu bora uende nje kama chuo ni cha uhakika,
tatizo la tz ni kweli watu wanakamua sana lakini sio kuelewa bali kuepuka kukamatwa mashati na malectures wanao ona raha ukifeli.
Mfumo wa vyuo bongo upo kupasi zaidi wakati wenzetu kuelewa kwanza ndio uta pasi.
 
Nenda nje kijana achana na vyuo vya kibongo mi mwenyewe km kakayako nimesoma chuo kikuu bongo hamna lolote zaidi ya kuepuka suprementary ya malecturer kasome hulo uweze kujitegemea. Wengi wetu tuliosoma Bongo tunategemea zaidi ajira eventuary tunapigwa jua siku nzima tukitafta ajira.
 
Kama umepata scholarship au una uhakika wa kupata msaada financially hasa mwaka wa mwanzo bora uende nje. Inategemea ni nchi gani kama wengi walivyokushauri kuna mambo mengi yanatofautiana ungekuwa specific ni nchi gani hasa umepata nafasi nadhani pia ungepata ushauri wa uhakika zaidi.
 
huyu bosi yeye kasoma advance diploma ya maendeleo ya jamii pale Tengeru CDTI nahisi nae alikuwa anasikia kwa watu tu maana scholarship nimepata ya nchi ya Russia so akasema kwamba huko watu wanaosoma huko wanakuwa walevi sana na shule ya huko inawafaa watu wa science tu!
 
Nawashukuru sana kwa ushauri wenu niliona niulize hapa sababu nilijua wengi hapa ni watu wenye uelewa mpana juu ya maisha na mambo ya nje na kuna wengine wanaishi huko so wanajua the real situation
 
bongo utapiga photocopy vitabu mpaka semester inaisha.hakuna lolote hapa labda kwa kozi ya medicine kwa kua utakumbana na tropical diseases ambazo nchi zingine hakuna!
 
huyu bosi yeye kasoma advance diploma ya maendeleo ya jamii pale Tengeru CDTI nahisi nae alikuwa anasikia kwa watu tu maana scholarship nimepata ya nchi ya Russia so akasema kwamba huko watu wanaosoma huko wanakuwa walevi sana na shule ya huko inawafaa watu wa science tu!
Nikuambie ndugu,huyo mshauri wako sio kosa lake kwa vile hajuhi alisemalo.Tofauti ya mitaala sio ishu.Na kama anakwambia ati elimu ya bongo ni nzuri kuliko nchi zingine,em muulize elimu hiyo nzuri ya bongo imeweza kutranslate vipi kwenye maendeleo ya nchi,mbona bongo ni masikini wa kutupwa na hiyo elimu wanayojidahi nayo.Facts ni hizi hapa,elimu ya bongo ni mbovu mbovu mno.Waalimu wa bongo hawako serious,mimi nakumbuka kuna ndugu yangu alikuwa mzumbe ananiambia sometimes kaenda class mwalimu hajafika ati ana safari nk nk.Chuo kikuu? what?..vitu kama hivyo havitokei kwenye nchi zingine watu wako serious na elimu yao,muhula ilivyopangwa ndivyo inavyoisha,mwalimu akitokea asiwepo lazima awe replaced.Elimu ya Urusi,China,India,Malaysia,Japan,Korea,Europe and North America n.k ni nzuri mara kibao kulinganisha na ya Tanzania.Huku watu wameendelea sababu ya elimu,ukifanikiwa kupata scholarship ya kutoka bongo,kimbia fasta toka nduki we kimbia!..utajifunza mengi sana nje ya nchi,utajua dunia ilivyo.Mimi nilipata B.COM udsm na Scholarship zote kwa pamoja nikapiga chini B.COM,today am proud of my decision.
 
huyu bosi yeye kasoma advance diploma ya maendeleo ya jamii pale Tengeru CDTI nahisi nae alikuwa anasikia kwa watu tu maana scholarship nimepata ya nchi ya Russia so akasema kwamba huko watu wanaosoma huko wanakuwa walevi sana na shule ya huko inawafaa watu wa science tu!

Ina maana ukibaki bongo ndo huwezi kua mlevi ukitaka???Huo ni uamuzi wa mtu na sio sehemu.Newayz nna watu wanasoma Russia wala hawalalamiki sana......sema baridi ni kali alafu wakati mwingine wazawa wanakua wakorofi kwa wageni....ila sijaskia mtu akilalamika shule sio nzuri!Tumia hiyo nafasi usije ukaitamani baadae ikishapita!
 
huyu bosi yeye kasoma advance diploma ya maendeleo ya jamii pale tengeru cdti nahisi nae alikuwa anasikia kwa watu tu maana scholarship nimepata ya nchi ya russia so akasema kwamba huko watu wanaosoma huko wanakuwa walevi sana na shule ya huko inawafaa watu wa science tu!

bro labda kwa reason nyengine ila kwa ulevi ni ww mwenyewe kama utaendekeza pombe ht bongo unaweza kuwa mlevi sisi tupo huku wala pombe haijawahi karibia kinywa.........
 
Back
Top Bottom