2019
JF-Expert Member
- Dec 31, 2018
- 2,982
- 4,457
Natuamai mko powa.
Toka Rais Samia aapishwe kuna watu wanahisi ni tumaini jipya Tanzania, hotuba hata 5 bado lakini watu wanahisi shida zao zimeisha.
Ni kweli watu wapepata tumaini jipya? Magufuli alianzaje? Tumbua tumbua yake, fukuza fukuza yake, wafanyakazi hewa, vyeti feki, matamko matamu matamu n.k.
Matukio yote hayakufurahisha watu? Bila shaka hata mimi nilifurahi, kabla hajabadili gia wenye maono wakashauri kwanini haya matamko yasitengenezewe sheria ila akitoka yabaki? Watu wakadai hakuna haja wakidhani kesho uhakika.
Sasa mama Samia kaingia, nae mwendo ni ule ule japo yeye katoa uhuru zaidi lakini tuna uhakika na kesho? Leo yupo kesho asipokuepo?
Watanzania tunapaswa kujiuliza tunahitaji matamko,watu au katiba ambayo kila kiongozi atakaekuja ataifuata?
Kama US wangekuwa na katiba na uoga kama wa Tanzania Trump angeibadili na kutawala maisha. Kwa hiyo nyie mnaoshangilia msije lia badae, Samia yuko vizuri lakini bila katiba hakuna jipya kabisa ni swala la muda tu.
Toka Rais Samia aapishwe kuna watu wanahisi ni tumaini jipya Tanzania, hotuba hata 5 bado lakini watu wanahisi shida zao zimeisha.
Ni kweli watu wapepata tumaini jipya? Magufuli alianzaje? Tumbua tumbua yake, fukuza fukuza yake, wafanyakazi hewa, vyeti feki, matamko matamu matamu n.k.
Matukio yote hayakufurahisha watu? Bila shaka hata mimi nilifurahi, kabla hajabadili gia wenye maono wakashauri kwanini haya matamko yasitengenezewe sheria ila akitoka yabaki? Watu wakadai hakuna haja wakidhani kesho uhakika.
Sasa mama Samia kaingia, nae mwendo ni ule ule japo yeye katoa uhuru zaidi lakini tuna uhakika na kesho? Leo yupo kesho asipokuepo?
Watanzania tunapaswa kujiuliza tunahitaji matamko,watu au katiba ambayo kila kiongozi atakaekuja ataifuata?
Kama US wangekuwa na katiba na uoga kama wa Tanzania Trump angeibadili na kutawala maisha. Kwa hiyo nyie mnaoshangilia msije lia badae, Samia yuko vizuri lakini bila katiba hakuna jipya kabisa ni swala la muda tu.