fungafunga
Senior Member
- Mar 30, 2010
- 116
- 155
Kabla ya kumshauri naomba kwanza nimlaumu(samahan lakin)
1.Haingii akilini mpaka anafikisha Miaka 60 kazini Hajasimamisha ata chumba kimoja. Huu Ni uzembe wa Ali ya juu na haitakiwi kufumbiwa macho.
2.Kiinua mgongo hakiwekwa ili mtumishi akajenge, kile ni kwa ajili ya KULA TU matunda ya utumishi wake Miaka yote iyo aliyotumikia(kifuta jasho).
Maana yake ile ilitakiwa iwe pesa ya KULA mema ya nchi,utalii na vacation mbalimbali.
Ushauri:
1. Arudi Mkoani alikozaliwa akatafute Kiwanja Cha Bei nafuu, akajenge nyumba nafuu isiyozidi milioni 20-25
Kwanini nasema ivo: Akijitutumua kujenga hapa Mjini kwa mil. 60, atabakiwa na mil 20.
Sijajua ataifanyia nini ila Kama Ni kujiingiza katika utaftaji,
nakuapia atafeli vibaya mno maana purukushani za utaftaji kwa umri huo wa 60+ Ktk mji wetu huu hatoziweza kabisa, ATAKUFA KWA PRESHA BURE.
2. ASIWE NA WASHAURI WENGI WA FEDHA.
hapa wazee wa fursa washanusa mzee atashika mpunga mwingi mdA sio mrefu.
-Wazee wa MR. KUKU
(wekeza laki 7 upate milioni 70 kwa wiki 4)
-wazee wa FOREX
(wekeza Dola 1000 upate Dola 500,000 ndani ya nusu saa)
MSHAURI MZEE ARUDI BUSH ALIKOZALIWA, ALE MAISHA YAKE YALIOBAKI.
Sent using Jamii Forums mobile app
Umetoa ushauri mzuri sana!!