Kipi bora kati ya hivi pindi uwapo na mpenzi wako?

linahbaby

JF-Expert Member
Jul 18, 2020
1,087
3,084
Habari zenu wakuu, hope mko salama na mmemaliza mwaka salama..

Husika na mada hapo juu, leo nataka tupige story kuhusiana na maswala ya simu wakati wa faragha..

Kama mjuavyo mapenzi ni hisia, na pia unapo kuwa na mpenzi wako umakini unahitajika sana hasa kwa yule wa mara ya kwanza kumeet naye..

Watu wengi wamejikuta wanashindwa kuwa romantic kwa mapenzi kwa sababu ya simu, unakuta wako katika muda wa kuwa romantic lkn mmoja wapo yuko busy na kuchart au yuko mtandaoni anaperuz ...

Turejee kwenye mada yetu, kipi bora au nini kifanyike pindi muwapo faragha...

1. Azime simu asipatikane kabisa hewani,

2. Asizime simu iwe hewani ikiita asipokee wala kujibu sms,

3. Asizime simu ikiita apokee na kujibu sms kma kawaida,

4. Asizime simu ikiita atoke akaongelee nje,

5. Au azime tu data simu aiache hewani mawasiliano mengine yaendelee isipo kuwa mtandaoni asiingie,

Kwa upande wangu mimi napenda sana simu izimwe kwa kweli, maana unaweza kuwa hewani ghafla upigiwe simu maybe na family au kazini ukapata taarifa mbaya ikakutoa kwa mood so ukizima simu kwa huo muda mchache itasaidia sana,

Ukiachana na family na kazi kuna michepuko pia, kwa hiyo simu ya mchepuko inaweza kuleta ugomvi na kupelekea kuachana,

Hivyo umakini unahitajika wakati wa faragha..
IMG-20210104-WA0002.jpg
 
Back
Top Bottom