Kipaumbele Kikubwa zaidi, Kuliko Vipaumbele ulivyoviainisha mwaka 2017 Ni Hiki.!

Heart Wood.

JF-Expert Member
Nov 16, 2014
886
930
Bila shaka Mungu anaendelea kuyahudumia maisha yako, anaendelea kujihusisha na Maisha yako na Familia yako, pamoja na ndugu na Rafiki zako, kwa sababu ndiye aliyetuumba. Kama ndiye aliyetuumba, hakika ni katika yeye ndipo tunafahamu kusudio la Maisha yetu hapa Duniani. Kama hutambui kuwa Mungu ni sababu ya Maisha yako mpaka sasa, basi Maisha yako hayatakuwa na maana yoyote, kwa maana, yote huanza na YEYE kwa sababu ndiye aliye Asili ya mambo yote.

Bila shaka umeweka Mipango mingi tunapouanza Mwaka huu mpya, 2017. Bila shaka umeweka mikakati mbalimbali ili kufikia mafanikio ya mipango yako. Pamoja na hayo, imenipasa kukushirikisha mambo machache ninayodhani yanaweza kukusaidia katika siku zako za Uhai zilizobaki hapa Duniani.

Kwanza kabisa, imetupasa kutambua kuwa, Maisha ya hapa Duniani ni mafupi ukilinganisha na yale tutakayoyaishi baada ya kifo cha Mwili, naam, ni pale roho itakapotengana na miili hii tuliyonayo, ambapo huitwa “kufariki”. Biblia inasema maisha ya hapa Duniani yapata miaka Sabini na ikiwa tuna nguvu ni miaka Themanini (Zab 90: 10), Lakini, maisha ya Mbinguni kwa wafanyao mapenzi ya Mungu imeahidiwa maisha ya umiilele( 1Yoh 2: 17), Lakini, pamoja na hayo,cha kushangaza ni kwamba, tumeyapenda zaidi maisha ya Dunia hii kuliko yale ya Mbinguni bila shaka hii ni kutokana na ufahamu wetu kutiwa upofu (2Wakor 4:4), Laiti kama fahamu zetu zisingekuwa zimetiwa upofu, katika hali ya kawaida tu, ukiambiwa uchague maisha ya milele na maisha ya miaka 80, bila kusita utachagua maisha ya umilele kuliko haya ya miaka 80 yaliyo mafupi sana. Biblia iansema “Msiipende Dunia wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda Dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia, Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake….”( 1Yoh 2: 15 - 17)

Ili kujihakikishia maisha ya Mbinguni, tiketi na kipimo chake kinapatina hapa Duniani, jinsi tunavyoishi, jinsi tunavohusiana na Mungu pamoja na wanadamu.

MWAKA 2017 UWE WA KUENENDA SAWASAWA NA NENO LA MUNGU

Kuishi sawasawa na Neno la Mungu ni tiketi namba moja ya kuyafikia maisha ya milele, Neno la Mungu ndiyo ushindi wa maisha yetu (Mathayo 4: 4).

Imetupasa kutambua kuwa, Kujifunza Neno la Mungu, Kumwabudu Mungu, na kuishi sawasawa na Neno lake si jambo la hiari, na kuwekwa kama jambo la ziada baada ya kukamilisha ratiba zetu za Kila siku, bali ni kiini cha maisha yetu. Imetupasa kulitafakari neno la Mungu kila wakati,usiku na mchana, tuwapo safarini, tuwapo Ofisini, tuwapo shambani, tukutanapo na rafiki na ndugu zetu nyakati za mapumziko, tuwapo katika kusanyiko la Watu wengi n.k,

MWAKA 2017 UWE WA KUKUA KIROHO
Ili ukue Kiroho, lazima ukubali kuwa tofauti na mambo ya Ulimwengu huu, lazima ukubali mabadiliko katika ratiba za Maisha yako, mtindo wa kuishi na namna nyingine za Dunia hii, lazima ukubali kupoteza baadhi ya mambo unayofikiri ni muhimu katika hii Dunia na mengine mengi ya mtindo wa Dunia hii, hauwezi kutaka kufikia viwango wa juu kiroho bila kuruhusu mabadiliko katika mfumo mzima wa maisha yako, ukisema unakua kiroho, huku hakuna mabadiliko kati ya mfumo wa maisha yako ya zamani na ya sasa, huko si kukua, ni kuendelea kudumaa. Kwa muda mwingi, yawezekana kabisa kuwa tangia kuzaliwa kwako, umeujaza ufahamu wako kwa mambo yasiyo ya msingi, mambo yasiyofaa na yenye kusababisha Matengano kati yako na Mungu, kukua Kiroho ni pamoja na kukubali kuondoa ufahamu danganyifu wa Kidunia na kuujaza ufahamu wako kwa kweli ya Mungu kupitia Neno lake. Lazima ufanye mabadiliko ya kile unachokisikiliza na kukitazama, lazima ukubali kuchagua maneno ya kuzungumza, lazima ukubali kubadilisha maeneo ya kutembelea na watu wa kukutana nao, n.k

MWAKA 2017 UWE WA KUJIHUSISHA NA NENO LA MUNGU KWA KIASI KIKUBWA ZAIDI
Imetupasa kufanya bidii zaidi kuutafuta Ufalme wa Mungu kuliko mambo mengine, tukiupata Ufalme wa Mungu, Mahitaji yetu mengine kama Wanadamu hapa Duniani, Mungu atayafanikisha(Mathayo 6: 33), kwa sababu Biblia inasema “Ayang’ang’aniaye maisha yake atayapoteza, lakini yeye atakayeyatoa maisha yake kwa ajili yangu atayaona.” (Mathayo 10:39) Neno linaendelea kusema; “.Kwa maana itamfaidia nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake?(Mathayo 16: 26). Itakufaa nini kuwa tajiri mkubwa mwenye magari na majumba lakini uukose Ufalme wa Mungu.? ( ieleweke kuwa hapa simaanishi kuupinga utajiri ule wa haki, bali ule usio wa haki).

Kama umepanga kuweka bidii zaidi za mafanikio yako kiuchumi kwa Mwaka 2017, basi bidii yako ya kufanikiwa katika maisha ya kiroho iwe mara kumi zaidi ya nguvu na mikakati uliyopanga kufanikiwa kiuchumi, kumuomba Mungu isiwe sehemu ya ratiba ya maisha yako, bali iwe uhalisia, utamaduni, mtindo na tabia ya maisha yako ya kila siku. Neno la Mungu linasema, (Mathayo 22:37 - 38).Yesu akamjibu, “‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote na kwa akili zako zote.’” Hii ndio amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza

Huwezi kumpenda Mungu kwa moyo wako wote kama hupati muda wa kuzungumza naye kupitia SALA mara kwa mara, huwezi kumpenda Mungu kwa moyo wako wote kama hupati muda wa kusoma na kujifunza neno lake. Kama umepanga kusoma vitabu vya jinsi ya kufanikiwa kiuchumi, kisiasa, mahusiano au vinginevyo katika maisha yako kwa mwaka 2017 mara mbili kwa siku, basi kusoma Neno la Mungu iwe mara kumi zaidi. Huo ndio msingi wa kufanikiwa, hatumtumii Mungu ili kufanikisha mipango ya maisha yetu pekee, bali kumruhusu Mungu atutumie kwa mujibu wa kusudio la kuumbwa kwetu, maana yeye alitujua tangu tukiwa tumboni mwa mama zetu, hivyo anatufahamu zaidi kuliko tunavyomfahamu yeye, kama yupo anayetufahamu zaidi na yeye ndiye chanzo cha Maisha yetu, kwa nini kusumbuka kwa fahamu na akili zetu wenyewe na kukataa kumuhusisha yeye atujuaye kwa kila kitu?

Heri na Fanaka za Mwaka 2017 ziwe za kudumu katika Maisha yako, Mungu akubariki na kukushindia katika yote.
 
Toa mistari ya biblia kwanza

Otherwise .....!!!

Tuacheni kutumia vitabu wakati maisha yetu tu ni misahafu tosha

Ukitathmini tulipo, Majibu yanapatikana bila msaada wa Yesu wala ...

Tukishapata majibu yetu sahili

Ndipo tumpe Yesu na Biblia maswali MAGUMU YANAYOMHUSU TU

Otherwise biblia inabaki kuwa muongozo kwenye mikono ya vipofu

Hawatofika mbali ..!
 
Toa mistari ya biblia kwanza

Otherwise .....!!!

Tuacheni kutumia vitabu wakati maisha yetu tu ni misahafu tosha

Ukitathmini tulipo, Majibu yanapatikana bila msaada wa Yesu wala ...

Tukishapata majibu yetu sahili

Ndipo tumpe Yesu na Biblia maswali MAGUMU YANAYOMHUSU TU

Otherwise biblia inabaki kuwa muongozo kwenye mikono ya vipofu

Hawatofika mbali ..!
“Mimi ndimi njia na kweli na uzima. Mtu hawezi kuja kwa Baba isipokuwa kwa kupitia Kwangu" ( YOHANA 14: 6)
 
“Mimi ndimi njia na kweli na uzima. Mtu hawezi kuja kwa Baba isipokuwa kwa kupitia Kwangu" ( YOHANA 14: 6)

YOHANA?

Yaani John?

Nina aleji na huo mstari, jina la kitabu lipo poa

Hivi unadhani hizo ndo zitatuokoa na baa la njaa linalokuja?

Ukishiba ndo unaweza hata kutoa sadaka

otherwise taasisi zenu zitakufa tu!



ACHENI MAIGIZO!!
 
YOHANA?

Yaani John?

Nina aleji na huo mstari, jina la kitabu lipo poa

Hivi unadhani hizo ndo zitatuokoa na baa la njaa linalokuja?

Ukishiba ndo unaweza hata kutoa sadaka

otherwise taasisi zenu zitakufa tu!



ACHENI MAIGIZO!!
"Mtu ambaye hana Roho wa Mungu hawezi kupokea mambo yatokayo kwa Roho wa Mungu, kwa kuwa ni upuzi kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa sababu hayo yanaeleweka tu kwa jinsi ya rohoni" (1Kor 2:14)
 
"Mtu ambaye hana Roho wa Mungu hawezi kupokea mambo yatokayo kwa Roho wa Mungu, kwa kuwa ni upuzi kwake, naye hawezi kuyaelewa kwa sababu hayo yanaeleweka tu kwa jinsi ya rohoni" (1Kor 2:14)


NI SAWA NA KUMSIMULIA KIPOFU RANGI ZA BENDERA YA TAIFA ILI AKUPE MAANA ZAKE

Sitakuelewa kama bado unatumia hiko kitabu!

Huna source nyingine inayotuhusu?
 
NI SAWA NA KUMSIMULIA KIPOFU RANGI ZA BENDERA YA TAIFA ILI AKUPE MAANA ZAKE

Sitakuelewa kama bado unatumia hiko kitabu!

Huna source nyingine inayotuhusu?
Shida yako ni ipi hasa? Kipi unahitaji kukijua?
 
Shida yako ni ipi hasa? Kipi unahitaji kukijua?

Unaweza kutoa evidence sahili ya msaada wa imani zetu hadi hapa tulipofikia?

Shuhuda za watu makanisani? Kweli?

Au maandiko yaliyoandikwa bila kutuhusisha?

Dini ni sumu mbaya sana ikitumika VYEMA!




Wanadini ndio wanaongoza kwa uchafu na unafiki

Mpaka mashoga wana dini?


What is Dini?

Shimo kubwa la takataka za kila aina!!
 
Unaweza kutoa evidence sahili ya msaada wa imani zetu hadi hapa tulipofikia?

Shuhuda za watu makanisani? Kweli?

Au maandiko yaliyoandikwa bila kutuhusisha?

Dini ni sumu mbaya sana ikitumika VYEMA!




Wanadini ndio wanaongoza kwa uchafu na unafiki

Mpaka mashoga wana dini?


What is Dini?

Shimo kubwa la takataka za kila aina!!
Dini kutoka Kiarabu اﻟدﻴن, tamka: ad-din) inamaanisha jumla ya imani ya binadamu kadhaa pamoja na mafundisho wanayotoa kuhusu yale ambayo wanayazingatia ama kuyasadiki, yaani mambo ya roho, kama vile kuhusiana na Mungu, maisha na uumbaji.

Ibada ni nguzo mojawapo iliyo dhahiri miongoni mwa dini kadhaa katika kuunganisha dhamira za mwenye kushika dini na mhimili wa imani, lakini dini inahusu pia mafundisho kuhusu maadili, mema na mabaya, imani na jinsi ya kushiriki katika jumuiya za waumini.

Kwa maana nyingine "dini" inataja jina kielelezo juu ya aina mbalimbali za imani jinsi inavyopatikana duniani, yaani jumuiya za kidini.
Dini kwa maana hiyo yenye wafuasi wengi duniani ni:

Pamoja na hizi kuna dini mbalimbali zinazojulikana tangu karne nyingi duniani hata kama idadi ya wafuasi si kubwa sana kwa mfano:

Pia kuna imani ambazo zinafanana kwa namna fulani, hivyo mara huhesabiwa kama imani mbalimbali za pekee, mara huhesabiwa kama kundi la dini zenye misingi ya pamoja au kama matawi ya imani moja. Zikitazamiwa pamoja idadi ya wafuasi ni kubwa kiasi lakini zikihesabiwa moja-moja idadi ya wafuasi si kubwa sana, kama vile:

SOURCE:Dini - Wikipedia, kamusi elezo huru
Dini ya Kikristo muasisi wake ni YESU KRISTO, alikuwepo hapa Duniani kwa njia ya uanadamu yapata miaka 2017 sasa. Dini hii ilianzia nchi za Mashariki ya Kati na kuenea Ulaya, Amerika na huku Afrika kwa njia mbalimbali kama vile Wamisionari, ukoloni n.k
Hali kadhalika, mahal alikozaliwa YESU huko Bethlehemu ya Uyahudi mpaka sasa panajulikana na watu huenda kupatazama, mahali alipoishi huko mashariki ya Kati pamoja na Misri huku Afrika panafahamika mpaka sasa. Historia na kumbukumbu zipo huko mpaka sasa alikoishi . Hivyo mambo haya si kusadikika bali ni kweli tupu.

Shuhuda za watu makanisani? Kweli?

Ni kweli kabsa bila kigugumizi chochote, usikumbwe na maneno ya wasioamini nguvu na uweza uliopo katika neno la Mungu, maneno ya watu wengi wasiolewa vema mafundisho ya Mungu kupitia Biblia hujaribu kuonesha kuwa kila miujiza inayofanyika kupitia Watumishi wa Mungu mbalimbali ni maigizo, nguvu za giza au kupagawa kisaikolojia. Hayo ni maneno ya kupuuza kabisa na hutakiwi kuyazingatia maneno kama hayo. Hebu jiulize kidogo, kama ni mfuuatiliaji; kinachofanyika kupitia wWatumishi wa Mungu waliopo Tanzania ndicho kinachofanyika South Afrika, Ghana, Nigeria, Marekani, Ulaya na hata Asia. Iweje hayo yote yawe maigizo ??? Wote hao wanaofunguliwa na kutoa Shuhuda wanaigiza ?? Inakuingia akilini na wewe?

Au maandiko yaliyoandikwa bila kutuhusisha?
Hapa sijakuelewa, ulitaka Biblia iandikwe kwa kushirikisha Wananchi kama zilivyo Katiba za Nchi Duniani.? Neno la Mungu haliwezi kudhihirika kwa namna ya kidunia.

Dini ni sumu mbaya sana ikitumika VYEMA!

Thibitisha angalau kidogo namna DINI zinavyokuwa SUMU.


Wanadini ndio wanaongoza kwa uchafu na unafiki

Mtu yeyote anaweza kuanguka katika dhambi kama asipokuwa na bidii ya kuutafuta uso wa BWANA, si Katekista, Shemasi,Mchungaji, Askofu, wala Papa ambaye anaweza kujihakikishia kuwa imara na kuishinda dhambi. Mtu yeyote anaweza kuanguka. Isitoshe, wote waliokaribu na Mungu ndio wanaopambana na sulba nyingi katika Ulimwengu wa Roho( Ni somo pana kidogo). Kwa mfano, mshindani wa U.S.A katika Uchumi haiwezi kuwa Tanzania, mshindani ni yule anayeonekana kujiinua na kuimarika Kiuchumi kama vile CHINA n.k , ndivyo ilivyo katika Ulimwengu wa Roho. Walio upande wa Shetani , Shetani hashindani nao kwa maana tayari wako upande wake.

Mpaka mashoga wana dini?
Dini ni pana kama nilivyoeleza hapo juu. Sasa hata hao ashoga unaosema wanaweza kuwa na DINI yao.

What is Dini?
Shimo kubwa la takataka za kila aina!!

Si kweli ndugu, nadhani unahitaji Elimu na maarifa zaidi kuhusu Mahusiano ya Mungu na Wanadamu.
 
Kiarabu اﻟدﻴن, tamka: ad-din) inamaanisha jumla ya imani ya binadamu kadhaa pamoja na mafundisho wanayotoa kuhusu yale ambayo wanayazingatia ama kuyasadiki, yaani mambo ya roho, kama vile kuhusiana na Mungu, maisha na uumbaji.

Ibada ni nguzo mojawapo iliyo dhahiri miongoni mwa dini kadhaa katika kuunganisha dhamira za mwenye kushika dini na mhimili wa imani, lakini dini inahusu pia mafundisho kuhusu maadili, mema na mabaya, imani na jinsi ya kushiriki katika jumuiya za waumini.

Kwa maana nyingine "dini" inataja jina kielelezo juu ya aina mbalimbali za imani jinsi inavyopatikana duniani, yaani jumuiya za kidini.
Dini kwa maana hiyo yenye wafuasi wengi duniani ni:

Pamoja na hizi kuna dini mbalimbali zinazojulikana tangu karne nyingi duniani hata kama idadi ya wafuasi si kubwa sana kwa mfano:

Pia kuna imani ambazo zinafanana kwa namna fulani, hivyo mara huhesabiwa kama imani mbalimbali za pekee, mara huhesabiwa kama kundi la dini zenye misingi ya pamoja au kama matawi ya imani moja. Zikitazamiwa pamoja idadi ya wafuasi ni kubwa kiasi lakini zikihesabiwa moja-moja idadi ya wafuasi si kubwa sana, kama vile:

SOURCE:Dini - Wikipedia, kamusi elezo huru
Dini ya Kikristo muasisi wake ni YESU KRISTO, alikuwepo hapa Duniani kwa njia ya uanadamu yapata miaka 2017 sasa. Dini hii ilianzia nchi za Mashariki ya Kati na kuenea Ulaya, Amerika na huku Afrika kwa njia mbalimbali kama vile Wamisionari, ukoloni n.k
Hali kadhalika, mahal alikozaliwa YESU huko Bethlehemu ya Uyahudi mpaka sasa panajulikana na watu huenda kupatazama, mahali alipoishi huko mashariki ya Kati pamoja na Misri huku Afrika panafahamika mpaka sasa. Historia na kumbukumbu zipo huko mpaka sasa alikoishi . Hivyo mambo haya si kusadikika bali ni kweli tupu.

Shuhuda za watu makanisani? Kweli?

Ni kweli kabsa bila kigugumizi chochote, usikumbwe na maneno ya wasioamini nguvu na uweza uliopo katika neno la Mungu, maneno ya watu wengi wasiolewa vema mafundisho ya Mungu kupitia Biblia hujaribu kuonesha kuwa kila miujiza inayofanyika kupitia Watumishi wa Mungu mbalimbali ni maigizo, nguvu za giza au kupagawa kisaikolojia. Hayo ni maneno ya kupuuza kabisa na hutakiwi kuyazingatia maneno kama hayo. Hebu jiulize kidogo, kama ni mfuuatiliaji; kinachofanyika kupitia wWatumishi wa Mungu waliopo Tanzania ndicho kinachofanyika South Afrika, Ghana, Nigeria, Marekani, Ulaya na hata Asia. Iweje hayo yote yawe maigizo ??? Wote hao wanaofunguliwa na kutoa Shuhuda wanaigiza ?? Inakuingia akilini na wewe?

Au maandiko yaliyoandikwa bila kutuhusisha?
Hapa sijakuelewa, ulitaka Biblia iandikwe kwa kushirikisha Wananchi kama zilivyo Katiba za Nchi Duniani.? Neno la Mungu haliwezi kudhihirika kwa namna ya kidunia.

Dini ni sumu mbaya sana ikitumika VYEMA!

Thibitisha angalau kidogo namna DINI zinavyokuwa SUMU.


Wanadini ndio wanaongoza kwa uchafu na unafiki

Siyo Wanadini tu, mtu yeyote anaweza kuanguka katika dhambi kama asipokuwa na bidii ya kuutafuta uso wa BWANA, si Katekista, Shemasi,Mchungaji, Askofu, wala Papa ambaye anaweza kujihakikishia kuwa imara na kuishinda dhambi. Mtu yeyote anaweza kuanguka. Isitoshe, wote waliokaribu na Mungu ndio wanaopambana na sulba nyingi katika Ulimwengu wa Roho( Ni somo pana kidogo). Kwa mfano, mshindani wa U.S.A katika Uchumi haiwezi kuwa Tanzania, mshindani ni yule anayeonekana kujiinua na kuimarika Kiuchumi kama vile CHINA n.k , ndivyo ilivyo katika Ulimwengu wa Roho. Walio upande wa Shetani , Shetani hashindani nao kwa maana tayari wako upande wake.

Mpaka mashoga wana dini?
Dini ni pana kama nilivyoeleza hapo juu. Sasa hata hao ashoga unaosema wanaweza kuwa na DINI yao.

What is Dini?
Si kweli ndugu, nadhani unahitaji Elimu na maarifa zaidi kuhusu Mahusiano ya Mungu na Wanadamu.
Shimo kubwa la takataka za kila aina!!


Mkuu hongera kwa kujaribu kuweka illusion zako hapo

Lakini Je, Una ushahidi sahili wa mtu aliyepona ukimwi? (USHAHIDI SAHILI!!)


Je kuna nabii Tanzania anaweza kushusha mana watu wa Dodoma kwenye ukame wakala


Unaweza kuihusisha kanuni ya dini za sasa na maendeleo yetu? (mfano kutoa mimba?)


Unamfahamu Pope vizuri?

Anzia hapo!
 
Mkuu hongera kwa kujaribu kuweka illusion zako hapo

Lakini Je, Una ushahidi sahili wa mtu aliyepona ukimwi? (USHAHIDI SAHILI!!)


Je kuna nabii Tanzania anaweza kushusha mana watu wa Dodoma kwenye ukame wakala


Unaweza kuihusisha kanuni ya dini za sasa na maendeleo yetu? (mfano kutoa mimba?)


Unamfahamu Pope vizuri?

Anzia hapo!
Kuhusu watu waliopona UKIMWI wala si jambo la kufikirika, ni jambo dhahiri. Unajua tatizo ni kwamba siye wanadamu tunamfikiria Mungu kwa rank zetu za utashi wa akili za ki-Uanadamu, sisi tukiona jambo ni gumu, tunadhani pia kwa Mungu ni gumu. Tumefikia hali ya kuweka mipaka ya mambo kuwa yapo yanayowezekana na yapo yaliyo magumu.

Mbele za Mungu hakuna jambo lililo gumu. Ni upofu wa Kiroho kumdhania Mungu katika utashi wa akili zetu za Ki-Uanadamu.

Wewe umetoa mfano wa UKIMWI na wala si Malaria kutokana na Utashi wako kukufikirisha kuwa UKIMWI ni jambo gumu sana na kudhani kwa Mungu pia litakuwa gumu. Huu ni Upofu. Mungu akufungue upate kuona Rohoni.

Siwezi kukutajia moja kwa moja jina la aliyepona UKIMWI, lakini , ukipata kuelewa namna masuala ya Rohoni yanavyofanya kazi, utagundua kuwa UKIMWI ni sawa na kutibu tu KIPELE kwenye ngozi.

Wapo wengi. Fatilia kupitia SHUHUDA za Watumishi wa Mungu utashuhudia. Ukitaka kuelewa mambo haya, usiwe rigid katika ufahamu wako, achilia na uruhusu akili na ufahamu wako kuingiza mambo mapya (ya Rohoni)usiyokuwa nayo na upunguze masuala yasiyo ya muhimu katika fahamu zako.

Kuhusu suala lako la UKAME, Kama nilivyosema hapo awali. Mungu hawekewi UKOMO wa kutenda jambo. Mungu ni yule yule habadiliki. Kama Mungu aliweza kutenganisha Bahari wana wa Israel wakapita, iweje UKAME.? Kama Mungu aliweza kusababisha MVUA kunyesha na Kuangamiza watu enzi za Nuhu na kubakia Nuhu na nduguze peke yake iweje kuhusu UKAME.?

Kama Mungu alilisha maelfu ya watu kwa Mikate mitano na Samaki wawili iweje kuhusu UKAME.? Tatizo ni kwamba tunamuwekea Mungu ukomo wa kutenda kama yeye ni Mwanadamu.
Hata hivyo, Mungu alipotuumba alituwekea na akili za kuishi hapa DUNIANI. Hata kama theory zetu za Kisayansi zinasema Climate ya DODOMA ni ya UKAME, haimanishi kuwa tushindwe kupata chakula huko DODOMA. Mbona Misri sehemu kubwa ni jangwa lakini wanalima??

Hilo suala la Papa siwezi kulijadili hapa, maana si pahala pake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom