Kipanya kapiga Ikulu, yaani mwanao afe wa jirani apone

Kipawa ukitumia vibaya inakuwa sio kipawa tena bali laana,tafakari,Kipanya anatumia kipawa chake kueneza chuki,kumbuka hata Rwanda walioeneza chuki ni watu waliotumia vipaji vyao kama Kipanya,Kipanya akitaka siasa ajiunge tu na siasa na si kutumia kivuli cha uchoraji wa vikaragosi,nani asiyejua kuwa Kipanya ni kikaragosi cha Chadema?kumbuka pakichimbika hata hivyo vikaragosi vyake hakuna atakyekuwa na muda wa kuvisoma.Je ina maana unapotoa msaada kwa jirani wewe jamaa zako hawana shida?
Kibaya gani wewe Kipanya kafanya?Hivi kwanini mnapenda kuwatisha watanzania kuitumia Rwanda kama kivuli chenu ili watu wasitoe maoni yao.
Njoo nikwaambie kitu mauaji ya kimbari yalisababiswa Na serikali kwa kukandamiza jamii nyingine hasa ya kitusi,
Na kagame alikuwa mpinzani wa serikali(RPA),Ni sawa na ACT ingawa kagame alitumia kuipinga serikali kwa kuvamia Rwanda kutumia jeshi hasa kutokana na mazingira magumu ya kufanya siasa yaliowekwa na serikali ya Habriamana,Na ndicho tunakiona hapa kwetu hii miaka ya karibuni,Nadhani wote ni mashuda jinsi ulivyo mswada wa vyama vya siasa.
Huwa nafurahi sana mnavyotolea mfano Rwanda kwa kujua au kutokujua kwamba tukimchukulia kagame alikuwa mpinzani akitaka udhalimu,ukandamizaji uliokuwa umeshamiri chini ya utawala wa kihutu ukomeshwe,
Kwa hiyo mnavyowatisha watanzania kwa kutumia Rwanda ni upuuzi,Wale intaharamwe kile ni kikundi kilichokuwa kinaratibiwa na serikali kuendesha mauji,
Je mnavyotumia mfano wa Rwanda kwa hiyo mnawambia wapinzani wa serikali wasiikosoe serikali,kwasababu serikali inaweza kusababisha mauji kama ya Rwanda kama walivyofanya intarahamwe chini ya chama tawala(MRND) hapa kwetu sawa na CCM.
Na chombo cha habari ambacho kilikuwa kinatoa hate speech ni cha serikali na chama tawala k
ilikuwa kinaitwa RTLM sawa na Radio UHURU ya CCM.
Kwa muktadha huu serikali inataka watu wakiikosoa iwafyeke wapinzani wake kama ilivyofanya serikali ya Habriamana na interahamwe.
Halafu nadhani we mchangiaji hujui hata Mauji ya kimbari ya Rwanda chanzo nini acha kukariri kwa sababu Rais katolea mfano,nina uhakika hata mhehimiwa Rais hajui chanzo chake.
Tufike kipindi tuache kuwatisha watanzania ukiminya Uhuru wa watu watautafuta kwa nguvu kama alivyofanya kagame usiku mwema.
Vinara wa mauaji ya kimbari
I) Robert kajuga huyu alikuwa Rais wa intarahamwe.
ii)Jean kambanda-waziri mkuu kwenye serikali ya mpito baada ya kifo cha Habriamana
iii)Augustine Bizimungu) huyu alimbadili Gatsinzi kuwa chief of staff kutokana kuwa extrimist.


iv)Justin Mgenzi
V)Mathieu Ngirumpatse-Aliyekuwa Rais wa chama tawala MRND
Vi)Ephrem Nkezabera -kiongozi wa kamati ya kuratibu mauaji wa intaharamwe
Vii)Andre ntegerura mlezi wa MRND
Viii)Theonest Bagosora huyu alikuwa na misimamo mikali kwa wahutu alikuwa waziri wa ulinzi nyakati za mwisho wa utawala wa MRND.
Wote hao walikuwa ni kutoka ndani ya serikali ya MRND siyo upinzani RPF.
 
Ahahahahahahaaaaaaa kipanyaaaaaaaaaaaaaa.......no caption at all kila mtu akili yake itaamua kuwa hapa amemaanisha nn
Hakuna cha zaidi ya jiwe kusema sitoi chakula huku akipeleka msaada wa chakula kwa jirani zetu msumbiji. Kauli hiyo ameirudia mara mbili maanake nini sasa ndo kipanya kampa za uso
 
yaani mwanao anahitaji wewe unamlisha mwana wa mwingine .. cartoonist nawapenda .
 
Mwanao analia njaa wewe unampa chakula wa mwenzako. Misaada nikikumbuka ya Kagera. Nakosa majibu.
 
msiogope kusomewa Vitabu mlivovitunga.Kitabu cha lissu mlikitunga wenyewe kusomewa mnadai ni msaliti,kasaliti nn sasa hali amesoma kitabu kama kilivoandikwa
 
Watu wa Kagera sijui kama watamwelewa huyu. Wao kicha ya kunyimwa misaada iliyotolewa na watu na siyo serikali alikwenda kuwa kejeli kuwa wamezidi mno kukumbwa na mabalaa ikiwemo vita na ukimwi. Akazungumzia mto ngono na katerero mwisho akasema yeye hakuleta tetemeko hivyo wapambane na hali yao. Sasa wanapoona ndege za jeshi letu zinabeba misaada iliyotolewa na serikali yetu kupeleka nje watakuwa wamebaki bumbuwazi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bukoba walilia baada ya tetemeko wakaambiwa kuwa hakitoki kitu hapa .... Anayeteka kula na afanye kazi!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom