Iyokopokomayoko
JF-Expert Member
- Sep 15, 2011
- 1,785
- 441
Usiseme vikombe viwili,weka size in litres,kwani vikombe vyote dunian viko sawa?
Kwa kawaida kikombe kimoja huwa tunamaanisha robo lita (ml 250) mkuu.
Usiseme vikombe viwili,weka size in litres,kwani vikombe vyote dunian viko sawa?
nenda hospitali
Msaada kwenye tuta jamani nini chanzo cha kipanda uso, na nini tiba yake maana mie leo tangu asubuhi kimenicharukia nimejaribu pain killer lakini bado.
JITIBU KIPANDAUSO:Msaada please
Kuumwa na kichwa
kumegawanyka sehemu kuu nyingi sana japo kuwa 1% yake ni hashirio la matatizo ya kiafya ambayo
yameadvance. Kama vile concussion of brain,meningitis,encephaliti, na stroke. Kuumwa na kichwa pia inawezatokana na matatizo ya
taya, meno au hata kula vitu vya baridi zaidi. Vyakula vyenye nitrite au monosodium glutamate.
Sehemu ambazo huuma ni kama ifuatavyo.mfumo wa fahamu ambao upo kwenye fuvu la kichwa.
Baadhi ya neva za fahamu zizlizoko usoni
Misuli ya kichwani
Mishipa inayopatikana kwenye fuvu la kichwana chini ya ubongo kuna mifumo ya fahamu yenye hisia. Kumbuka fuvu na tishuu za ubongo kwa zenyewe haziumi kwani hazna mifumo ya fahamu ambayo inahisia.
Mambo haya 12 nayo yanahusika sana.
1:Nervous tension headaches;
Ni maumivu ya kichwa endelevu upande mmoja au pande zote za misuli ya shingo na upande wa juu wa mgongo,kuumwa na kichwa pamoja na kusinzia. Tumia vitamin b2 na c , ounguza au acha matumizi ya sukari,kahawa,chakula chenye kukusababishia mzio,misongo ya mawazo na ufanye mazoezi yakutosha.
2: Cluster headaches;
Kichwa kuuma haswa upande mmoja wa kichwa kwa maumivu makali, machozi humtoka mtu na makamasi kwa mbali. Kitu cha kwanza ni kutumia chakula chenye protein ya kutosha, epukana na chakula chenye mzio kwako.
3: Hangover headaches;
Hii ni hali ya kichwa kuuma kwa sababu ya matumizi makubwa ya vinywaji vikali haswa pombe. Weka barafu chini ya kichwa yaani maeneo ya kichogoni au shingoni,kunywa maji mengi na juice ya matunda freshi na uache pombe.
4: Exertion headaches;
Hutokea pale ambapo mwili utatumika sana na haswa kwenye ngono. Weka barafu linalouma, kula mlo kamili na usifanye mazoezi.
5: Caffein headaches;
Hali hii hutokea pale ambapo umeacha matumizi makubwa sana ya kahawa kwa ghafla. Kunywa kiasi kidogo cha kahawa kuondoa maumivu na upunguze matumizi kidogokodogo mpaka utakapo acha kabisa.
6: Sinus headaches;
Maumivu haya huanzia upande wa kulia na kushoto wa pua na kupanda mpaka kichwani. Kula vitamini C kwa wingi na umuone mtaalamu wa afya maana saa zingine hii utkana na maambukizi.
7: Bilious headaches;
Kichwa na macho huuma haswa kipanda uso na husababishwa na kula sana, kula vibaya, kutofanya mazoezi na kukosa choo. Fanya mazoezi na kunywa maji yakutosha na kasha fanya enema.
8: Hunger headaches;
Maumivu ya kichwa ambaya husababishwa na kutokula kwa muda. Kula chochote ilimradi kiwe ni protein au carbohydrates .
9: Eyes ram headaches
Haya ni maumivu yanayotokea kwenye macho na wengi hudhani labda wameangalia vibaya japo saa zingine inaweza kuwa sababu. lakini chanzo chake haswa ni ubongo kufanya kazi kupita kiasi. Badili mtindo wa maisha na kama ni mtumiaji wa miwani ni vyema ukamuana mtaalamu aangalie kama lensi zimepotea nuru au la.
10: Menstrual headaches;
Hali hii hutokea kwa kina mama kipindi cha yai kupevuka. Hutokana na mabadiliko ya hormone, muone mtaalamu wa afya.
11: Arthritis headaches;
Haya ni maumivu ya kichwa yanayosikika mpaka shingoni na saa zingine mpaka mgongoni ambayo husababisha maumivu haswa unapozidisha mwendo au shughuli. Kitu kikubwa ni kutibu ugonjwa unaosababisha hali hiyo.
12: Hypertension headaches;
Ni maumivu ya kichwa chote, mwendo mkubwa pia huongeza maumivu. Hali hii husababishwa na shinikizo la damu. Tibu au pambana kushusha shinikizo la damu na halii itaisha bila shaka.
Kabla ya kukupa dawa na ushauri wangu nina maswali nikuulize unijibu.
Je unapata Usingiz wa kutosha? unalala usiku masaa mangapi? je unakunywa maji ya kutosha? una miaka mingapi? Unapata haja kubwa ya kutosha ? Nenda pia kapime macho yako
na ukapime tena kwenye mishipa yako ya fahamu huenda una matatizo. Na kitu kingine unakuwa upo juani uwe unavaa kichwani kofia.
Habarini, naomba msaada kwa hili tatizo; mi ninapata mumivu makali sana ya kichwa katika paji la uso pale ninapo tizama vitu vyenye mwanga hususani mkali, vitu hivyo ni luninga, computer, simu ya mkononi n.k , nikitizama vitu hivi kwa muda fulani mwanga wake unanitanya macho kuuma ikiambatana na maumivu makali sana ya kichwa katika paji la uso.
Pia mimi ni mkandarasi hivyo asilimia 100% ya muda wangu wa kazi ni juani na ninapokaa juani kutwa nzima napatwa na maumivu makali ya paji la uso, khari hii imedumu kwa takribani miaka 10 na wakati mwingi nashindwa kufanya kazi kwasababu ya tatizo hili, na tangu 2004 mpaka sasa nimekuwa na tatitizo la maimivi makali ya kichwa maeneo ya kisogoni nimefanya CT scan na MRI muhimbili hazikuona tatizo katika kichwa na kutumia dawa za nerves bila mafanikio pia miwani nimevaa kwa muda wa miezi 6 bila mafanikio, imefikia wakati hata mwajili wangu kutaka kuni simamisha kazi kwa ajili ya tatizo hili,jamani kwa mwanye kujua tiba ya tatizo hili anisaidie.