Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,778
Kipa Ivo Mapunda, Kocha Micho, wang'ara Ligi ya Ethiopia
Na Vicky Kimaro
KIPA wa zamani wa Yanga, Ivo Mapunda na kocha wake Mserbia Sredojevich Milutin 'Micho' wameiongoza St. George kutwaa ubingwa wa ligi ya Ethiopia mapema.
St. George imetangaza ubingwa ikiwa na mechi mbili mkononi chini ya kocha wa zamani wa timu ya Yanga, Micho.
Hadi mwishoni mwa wiki Ivo alikuwa amefungwa mabao saba na hajapaoteza mchezo hata mmoja, hivyo Shirikisho la Soka la Ethiopia huenda likamtangaza kuwa kipa bora.
Micho aliiambia Mwananchi jana kuwa pamoja na nchi hiyo kuingia kwenye matatizo ya kufungiwa na Shirikisho la Soka duniani (Fifa), ligi ya Ethiopia imemalizika vizuri bila matatizo.
Na Vicky Kimaro
KIPA wa zamani wa Yanga, Ivo Mapunda na kocha wake Mserbia Sredojevich Milutin 'Micho' wameiongoza St. George kutwaa ubingwa wa ligi ya Ethiopia mapema.
St. George imetangaza ubingwa ikiwa na mechi mbili mkononi chini ya kocha wa zamani wa timu ya Yanga, Micho.
Hadi mwishoni mwa wiki Ivo alikuwa amefungwa mabao saba na hajapaoteza mchezo hata mmoja, hivyo Shirikisho la Soka la Ethiopia huenda likamtangaza kuwa kipa bora.
Micho aliiambia Mwananchi jana kuwa pamoja na nchi hiyo kuingia kwenye matatizo ya kufungiwa na Shirikisho la Soka duniani (Fifa), ligi ya Ethiopia imemalizika vizuri bila matatizo.