Ni tabu sana, ninambiwa sasa vijana wapo vikindu sasa...na hali ya mzinga sasa imetulia kiasi.
Yupo kundi gani mkuu?
Uwepo wao ni kwasababu Askari wetu wengi ni failures na waliopo madarakani ni mabingwa wa ngonjera kwenye Luninga, ulishawahi kumuona Kuva akielezea jambazi sugu alivyouwawa au kukamatwa? Utadhani amekamata au kuua tembo mkubwaaaa, maskini kumbe mtu aliyeuwawa alikua hana hata bunduki. Huwa nacheka sana kwa kweli
Uwepo wao ni kwasababu Askari wetu wengi ni failures na waliopo madarakani ni mabingwa wa ngonjera kwenye Luninga, ulishawahi kumuona Kuva akielezea jambazi sugu alivyouwawa au kukamatwa? Utadhani amekamata au kuua tembo mkubwaaaa, maskini kumbe mtu aliyeuwawa alikua hana hata bunduki. Huwa nacheka sana kwa kweli
Nimecheka hilo kundi la wamarekani weusi
Sijui Mbwa mwitu, Panya road na sasa wamarekani weusi mara tutasikia 'sisimizi wa kitaa' . Uwepo wa hivi vikundi ni dalili za udhaifu wa jeshi letu la Polisi ambalo limebakia kufukuzana na wanasiasa wa upinzani. Bila shaka kila mtu anajua hatari ya uwepo wa hivi vikundi hasa kwa wakazi wa Dar es salaam jinsi linavyohatarisha Amani ya wakazi wa huko.
Jeshi la Polisi anzisheni oparesheni ya kuondoa hivi vikundi ipo siku wananchi wataa kuvisaka kimoja baada ya kimoja na kuviteketeza.
UKOSEFU WA AJIRA KWA KIASI FULANI NAO UNACHANGIA.
Mkuu ulikuwa kwenye mawazo yangu.Inavyoonekana wanapata sapoti ya wanasiasa vinginevyo wangekuwa wamewadhibiti
kweli kabisaa
na hawa yawezekana kuna wanasiasa ama kundi kubwa la wenye mamlaka lipo nyuma yao kuwasapoti kama si kuwalinda, haiwezekani jeshi la polisi na intelijensia yao kali vile lishindwe kuwadhibiti mda wote huo.
wanaachiwa wamake headlines, tusije kulaumiana raia wa kawaida nao watakapolipuka na mchafuko mkubwa kuzuka kwa sababu vurugu zao anaeathirika ni raia mwema na mali zake kama hajajeruhiwa basi ataibiwa.....
stay tune Kamanda KOVA na INTELIJENSIA yako
polisi wao ni kupambana na mandamano ya ukawa...tu, ila ngoja siku mtoto wa kigogo afanyiwe kitu mbaya na hivyo vikundi ndiyo watajuaaaaa
UBALOZI WA MAREKANI WANA TAARIFA juu ya uvamizi wa vijana wao nchini?
sijui nani alowatungia hili jina
Na kwa jinsi mnavyowapeleka jkt basi wakiludi inakua saaafi kabisa.