Kiongozi wa NCCR adai Mbowe alinunua bia baada ya kusikia msiba!

Je kuna kosa kwa Mbowe kupiga kileo wakati chacha alipofariki


  • Total voters
    20
  • Poll closed .
Status
Not open for further replies.
Tatizo siyo kunywa katika Msiba,yeye alikunywa na kuwanunulia watu baada ya kusikia habari za msiba.sijasema kama ni kosa ila niimeuliza swali tu..


Wakati mwingine tusipokuwa makini tunaweza kujikuta tunatumiwa bila ya kujijua! Na hii itakuwa ni furaha kwa wale wanaotutumia.

Tujadili hili:

Kuhusu taarifa za kifo cha Wangwe; Kambi ya Upinzani ilianza kuzipata taarifa hizo majira ya saa 6 usiku. Je Mbowe alipewa taarifa hiyo usiku huo huo au la? Je wakati anapokea taarifa hiyo Mbowe alikuwa kwenye sehemu ya kinywaji (Pub/Bar) au la?

Maswali hayo hapo juu yakijibiwa kwa usahihi tunaweza kujadili.

Kuna mtu aliyehudhuria msiba wa Rodney Mutie Mengi? watakubaliana na mimi, suala la msiba na pombe ni kitu cha kawaida sana, na kama mfiwa ana uwezo ndie mwenye kugharamia hivyo vyote, kwa hiyo hili si jipya si hoja ya kujadiliwa, kuhusu Mbowe kununulia watu pombe!
 
Nadhani katika thread hii ulitaka kuonesha kuna uhusiano kati ya kifo cha Wangwe na kununuliwa kwa Bia na Mbowe. Ulitaka watu wahusishe taarifa za kununuliwa bia na Mbowe kupokea habari za msiba, na kuhusishwa huko kungekuwa kwa aina ya Mbowe kufurrahia kifo cha Wangwe. Siyo?

Mzee Mwanakijiji,

Sikudhani wala kufikri unavyosema wewe,Mie nilitaka kuonesha ni jinsi gani viongozi wa upinzani tulio nao,jinsi wanavopenda madaraka,umaarufu na maslahi.

sikutaka kuonesha Mbowe anahusika na kifo hiki,Kamwe sitakuja kufanya hivi na naawachi watu wa aina ya Mtu wa pwani wanaojua zaidi.Sina uzoefu katika hili.Mie nilitaka kufahamu watu wanalichukuliaje suala hili sababu mie kama ni rafiki wangu wa karibu siwezi kunywa bia.

Nimejaribu kuanginisha mambo sana mkuu,Ukiangalia toka Mwenyekiti alipofukuzwa kule Tarime na akashauriwa asiuzulie mazishi ni jambo gani lilikuwa limepikwa?

Nina maswali madogo mawili tu.

1.Unafikiri ni nini kilichomfanya Kiongozi wa NCCR kuongelea sula hili la Mbowe?

2.Nitaiweka habari hiyo muda mfupi ujao tupime ili tuweze kujua alipokea vipi habari hii,Je alishikwa na mshtuko?

3.Kwanini alikataa rambi rambi iliyochangishwa pale?Je yeye au Chama kina fungu la pesa kwa ajili ya kulipia watu wanaohaidi pesa za msiba?
 



Wakati Mwingine Tusipokuwa Makini Tunaweza Kujikuta Tunatumiwa Bila Ya Kujijua! Na Hii Itakuwa Ni Furaha Kwa Wale Wanaotutumia.

Tujadili Hili:

Kuhusu Taarifa Za Kifo Cha Wangwe; Kambi Ya Upinzani Ilianza Kuzipata Taarifa Hizo Majira Ya Saa 6 Usiku. Je Mbowe Alipewa Taarifa Hiyo Usiku Huo Huo Au La? Je Wakati Anapokea Taarifa Hiyo Mbowe Alikuwa Kwenye Sehemu Ya Kinywaji (pub/bar) Au La?

Maswali Hayo Hapo Juu Yakijibiwa Kwa Usahihi Tunaweza Kujadili.

Kuna Mtu Aliyehudhuria Msiba Wa Rodney Mutie Mengi? Watakubaliana Na Mimi, Suala La Msiba Na Pombe Ni Kitu Cha Kawaida Sana, Na Kama Mfiwa Ana Uwezo Ndie Mwenye Kugharamia Hivyo Vyote, Kwa Hiyo Hili Si Jipya Si Hoja Ya Kujadiliwa, Kuhusu Mbowe Kununulia Watu Pombe!


uchagani...mfiwa Kununua Pombe Ni Lazima Hata Kama Hana Uwezo Atajikongoja....na Pombe Na Chakula Kingi Msibani Ni Udhibitisho Kuwa Familia Ya Marehemu Ina Ukarimu..kwa Waliofika Kuwapa Pole....tena Kama Aliyekufa Ni Mwenye Mji Na Ameacha Mali...lazima Idhibitishwe Na Msiba Kutokuwa Wa Njaa Njaa...

...kama Hana Uwezo Wanaukoo Watakuja Na Pombe Msibani...ili Kulinda Hadhi Ya Ukoo...that Is Mila Tu!!
 
MKUU MKAMAP ,CHACHA amefariki nafikiri huu sio wakati mzuri kuongelea mijadala ya marehemu
Kuhusu hayo magazeti ,kwa sasa magazeti yote ya Tanzania habari zao haziaminiki hasa hao NEW HABARI wana beef na MBOWE nimejaribu kufuatilia Mtanzania na RAI tangu CHACHA kafariki heading kwenye frontpage lazima iilenge CHADEMA/MBOWE

Aisee mkuu naona umeweka jina langu hapo sijui limetokea vipi?
Imekaa je ? hiyo ndugu yangu.
 
hivi majuzi tulikuwa kwenye msiba wa ndugu yetu mwingine hapa US, na wabongo walipokutana pamoja na kuwepo msibani walileta vinywaji vya bia kwa wingi tu; sikujua walikuwa wanafurahia kifo cha huyo ndugu yetu. Tena nimeona hili mara nyingi tu. Sijui nchi nyingine kama wabongo wanaleta vinywaji msibani tena hata kabla ya marehemu hajazikwa.

Kama ndiyo hivyo (kusherehekea kifo cha mtu) basi ni kweli Mbowe amekosea na siyo yeye tu bali watanzania wengi wanaoleta ulabu misibani.

Mzee Mwanakijiji,

Jamii nyingi za Kiafrika hunywa pombe kwenye msiba. Ila mtu aliyembali, akionekana anaendelea kuweka kinywaji na wenzake baada ya kupata habari za msiba, hapo watu wengi wanaweza kushutuka.

Baada ya kufika kwenye msiba na kumwaga chozi la nguvu, hapo ndipo unaanza kusherehekea maisha ya marehemu na mnaweza kupata na kinywaji.

Kama mheshimiwa aliendelea kupata moja baridi, moja moto, hiyo ni dalili hakushutushwa na kifo cha marehemu.

Binafsi simlaumu Mbowe kwa hilo. Kama alimchukia Wangwe akiwa hai, kuna haja gani ya kuweka unafiki na kujifanya alikuwa kipenzi chake baada ya kufa?
 
Heshima Mbele,

Habari ambazo zilipamba mageti ya Nyumbani siku ya Jumapili yaliandika Habari kwamba Mhe. Mbowe aliwanunulia Baadhi ya watu raundi ya kinywaji alipokuwa Afrika Kusini na alionekana mchangamfu sana,na alionekana kutoshtushwa na habari za kifo cha Marehemu wangwe.

Nimeona ni vyema tujadili hili,Je ni kosa la Mbowe na linaweza kuwa na Madhara gani hasa kwa chama chake?Inasemekana kuna mmoja wa kiongozi wa kambi ya upinzani alishmwandikia IGP kuhsu hili na kuomba uchunguzi ufanyike.


Gembe ,

Ningependa kujua unaishi kona gani ya hii dunia ? Nikishapata jibu la hilo swali nadhani itakuwa ni rahisi kuichanua hoja yako
 
Ukitafuta magazeti ya jana utaipata hiyo,Nimeambiwa ni magazeti ya Mtanzania,Habari leo na majira.ngoja nicheki then nitaweka hapa.


Magazeti haya ni sauti za mafisadi, na usikute mwandishi wake ni mmoja. they are not reliable sources.
 
Ukitafuta magazeti ya jana utaipata hiyo,Nimeambiwa ni magazeti ya Mtanzania,Habari leo na majira.ngoja nicheki then nitaweka hapa.

Ushirombo,hakuna kioja sababu hata Mhe. Mbowe amekubaliana na hilo na kusema yeye alinunua raundi moja tu,aftera ll hii inasaidia na wala siyo kwa kujenga chuki na Mhe. Mbowe ila malipo ni hapa duniani

Yaani mzee uliweka hii taarifa bila kuangalia kwanza kwenye hayo magazeti? na kila taarifa ya gaezti ni ya kuiweka hapa?? Nina maswali yafuatayo kwako mkuu

1.Je ulipita muda gani tangu Mbowe kupata taarifa na kuwanunulia watu bia?
2.Je huwa ni kawaida yake kuwanunulia watu bia au ilitokea siku hiyo tu wakati amepata taarifa?
3.Ikiwa ni mara ya kwanza kuwanunulia watu bia je si tunaweza kusema alipata na mshtuko na ili kurelief stress zake akanunua bia?
4.Kuna standard gani ya mshtuko ambayo mtu akiipata kuhusu msiba tutasema ama kweli alishtuka!
5.Na je katika 'mashtuko' au vilio vyote ya misiba wanayoipata watu yote huwa ya kweli na mingine haina walakini? Kwa maana kama ulitaka Mbowe ashtuke bado tu angejifanya ameanguka na watu mkaamini(kama yeye amehusika), kwa hiyo hoja ya kushtuka haingii akilini.Watu wametofautiana kuabsorb shocks, na perception za watu zimetofautiana.Ulitaka afanye nini kaka?Nimeona watu wakiact kuwa wamezimia kumbe ndio walioua!
6.Je katika kusema hivyo no matter umepata wapi taarifa hii, je wewe mawazo yako ni nini? unataka kutoa conclusion gani? usizunguke mbuyu?
7.Je wewe ukipata msiba huwa unareact vipi tujue kuwa umeshtuka, katika misiba yote uliyowahi kusikia( here I am talking about your personal experience).?
8.Hiyo picha kwenye jina lako ni nani Mkapa au?


Waberoya
Don't let school interfere with your education
 
Haya maswali hapo juu(votes) mbona hayana uhusiano? nani ameweka?

Mbowe alikuwa rafiki mkubwa wa Chacha 1 12.50%
Mbowe alikuwa sawa kufanya hivi 7 87.50%

Kama nataka kujibu yote mawili kwa nini haiwezekani? kwani kwangu yote ni sawa? Kindly someone help me on this!!!

Waberoya
 
Gembe

Tazama akili zako zilivyo, tazama mlivyo na muda wa ziada, Tazama mnavyojikanganya, sijui tunaelekea wapi, mmejijaza hapa kujadili upuuzi, badala ya kutoa ushauri ili kuboresha upinzani ninyi mnazidi kuubomoa.

Akili zenu ndivyo zilivyo, toeni mapendekezo nini kifanyike ili kuboresha jamani, kisha nagundua kuwa leo hamna kazi za kufanya, fuadi yangu yanisukuma niwaambie jitahidini kuwa na mikakati ya 2010 kuliko kumjadili Mtu(Mbowe) kila kukicha.

Mimi katika thread yangu ile nilimshauri Mbowe ajiweke pembeni ili hawa Mafisadi na wale wate wanaotumiwa na Mafisadi wakose Mshiko.

Sasa tazama wanavyoyabuni, tazama wanavyompaka Tope, Tazama wanavyohakikisha kuwa Demokrasia hii changa haikui.
 
mzee Nimekusoma Na Kukuelewa, Nadhani Ni Ufisadi Wa Fikra Kwa Manufaa Ya Wachache Kabisa....sidhani Kama Mtukufu Gembe Na Wenzake Watalikwepa Hili....na Sijui Wanafanya Hili Kwa Manufaa Ya Nani...

1.nini Maana Ya Neno Mtumikie Kafiri Upate Mradi Wake??.

2.hatua Ya Kwanza Ya Ushindi Ni Kumtambua Adui
 
Acheni unafiki wakijinga kaeni chini andikeni vitu ambavyo vitaikomboa nchi hii siyo kushikilia udaku hapa..hel of you..nyie ndo mafisadi kwa kupelekwapelekwa
 
Jamani mbona mimi huenda misiba mingi tena ya Wakurya na Wachagga wanakuynywa kama kawaida wakati wa msiba?...Hivi hizo pombe huwa zinatoka mbinguni ama! maanake sioni tatizo liko wapi ikiwa ni kawaida ya misiba mingi nyumbani kupata ulabu. Au tatizo kubwa ni nani kanunua huo ulabu! ebu nipeni hizi mila zinavyotufundisha ktk maswala haya..
AU alitakiwa kununua ng'ombe na wangekula wakashiba wangesema ilikuwa sherehe vile vile!
 
Jamani mbona mimi huenda misiba mingi tena ya Wakurya na Wachagga wanakuynywa kama kawaida wakati wa msiba?...Hivi hizo pombe huwa zinatoka mbinguni ama! maanake sioni tatizo liko wapi ikiwa ni kawaida ya misiba mingi nyumbani kupata ulabu. Au tatizo kubwa ni nani kanunua huo ulabu! ebu nipeni hizi mila zinavyotufundisha ktk maswala haya..
AU alitakiwa kununua ng'ombe na wangekula wakashiba wangesema ilikuwa sherehe vile vile!

Mkandara,

Nimeacha kutoa michango yangu kwenye post mbalimbali kwa sababu ya hoja kama hii hapa. Nashindwa kabisa kuelewa mtu anayeibua hoja kama hii ana lengo gani. Kwenye mila nyingi za Kiafrika pombe wakati wa msiba hupewa hata adui mradi tu yuko karibu. Kwetu msiba hutafsiriwa na kuchukuliwa kama aina nyingine ya sherehe na kunywa na kula hutangulizwa na kupewa umuhimu usio kawaida. Mtu aliyeibua hii hoja anahitaji kuombewa.
 
Mimi kama Mtanzania huru kwenye nchi huru nahisi huu ni upandikaji wa chuki wenye maslahi binafsi kwa watu wachache wenye yao mambo!

nimekusoma. Wape ukweli najua habari nyingine zitafutwa ili watu wengine wasizisome na bado watu watasema WHERE WE DARE TALK OPENLY
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom