Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,445
Kiongozi wa kisiasa unapolazimisha upendwe ni sehemu ya udikteta. Kama mtu hakupendi mpe na nauli kabisa aondoke zake. Ama sivyo unaiua thamani yako wewe binafsi, ya chama na yule aliyekuumba. Na hata raha ya kutawala kwako itakosekana. Ukipendwa utaheshimiwa.
Usipoteze thamani ya muda na thamani yako kwa kujaribu kuhonga au kukenua meno ili upendwe na watu. Upendo huja wenyewe. Asiye na upendo kwako, achana naye au mpe nafasi akapende mahala pengine. Fanya kitu ambacho kitamfanya akuelewe na siyo kulazimisha.
Mwili ni kama taifa lenye kila aina ya madini ya thamani. Ukijichukulia poa unakaribisha wawekezaji wa hovyo. Ambao watakuchukulia kirahisi kwa kukuchimba wakuache kama handaki lenye popo. Kiongozi wa kisiasa huhitaji nguvu kubwa ili upendwe. Timiza ahadi zako upendwe mpaka ukereke.
Tatizo la madikteta duniani tangu na tangu ni kutaka kila mtu ampende. Huo ni wehu, anataka atazamwe vizuri, aongelewe kwa mema, ajadiliwe kwa kusifiwa na kila mtu. Mzee baba 'utadata' au itakuwa 'shotikati' ya kuukaribisha wendawazimu walioupata kina Bokassa nyakati zile.
Ukitaka raia akutukuze tenda kile ulichoahidi kumtendea. Nje ya hapo utatumia njia za wazi na gizani kunyamazisha watu. Na dawa ya raia ni ukweli, na ukweli uwe kwa pande zote mbili. Timiza ahadi yako kwao na wao watimize kwa kuungana nawe kwa kila ufanyalo. Mwisho huwa ni furaha tu.
Kuna vitu Mungu hapendi. Kama mja wake kukosa furaha ya maisha. Ni mpumbavu tu anayefuga maumivu ya hisia moyoni mwake. Kulazimisha, kubembeleza au kuhonga ili upendwe. Ni kosa linalostahili kuwa dhambi ya pekee.
Credit: Dk Levy
Sent using Jamii Forums mobile app
Usipoteze thamani ya muda na thamani yako kwa kujaribu kuhonga au kukenua meno ili upendwe na watu. Upendo huja wenyewe. Asiye na upendo kwako, achana naye au mpe nafasi akapende mahala pengine. Fanya kitu ambacho kitamfanya akuelewe na siyo kulazimisha.
Mwili ni kama taifa lenye kila aina ya madini ya thamani. Ukijichukulia poa unakaribisha wawekezaji wa hovyo. Ambao watakuchukulia kirahisi kwa kukuchimba wakuache kama handaki lenye popo. Kiongozi wa kisiasa huhitaji nguvu kubwa ili upendwe. Timiza ahadi zako upendwe mpaka ukereke.
Tatizo la madikteta duniani tangu na tangu ni kutaka kila mtu ampende. Huo ni wehu, anataka atazamwe vizuri, aongelewe kwa mema, ajadiliwe kwa kusifiwa na kila mtu. Mzee baba 'utadata' au itakuwa 'shotikati' ya kuukaribisha wendawazimu walioupata kina Bokassa nyakati zile.
Ukitaka raia akutukuze tenda kile ulichoahidi kumtendea. Nje ya hapo utatumia njia za wazi na gizani kunyamazisha watu. Na dawa ya raia ni ukweli, na ukweli uwe kwa pande zote mbili. Timiza ahadi yako kwao na wao watimize kwa kuungana nawe kwa kila ufanyalo. Mwisho huwa ni furaha tu.
Kuna vitu Mungu hapendi. Kama mja wake kukosa furaha ya maisha. Ni mpumbavu tu anayefuga maumivu ya hisia moyoni mwake. Kulazimisha, kubembeleza au kuhonga ili upendwe. Ni kosa linalostahili kuwa dhambi ya pekee.
Credit: Dk Levy
Sent using Jamii Forums mobile app