Kiongozi wa Kanisa la Pentecostal Power Ministry, Nabii Eliya Mahela asema hakubaliani na alichokifanya Waziri Lugola

Farolito

JF-Expert Member
Sep 10, 2018
11,634
26,370
Kiongozi mkuu wa kanisa la Pentecostal Power Ministry Nabii Eliya Mahela amesema hakubaliani na kile alichokifanya waziri Lugola cha Kumdhalilisha mchungaji wake pamoja na kumlazimisha kufungua kanisa kukanyaga madhabahu ya Mungu na watu wenye imani tofauti na kuifanya kama ukumbi wa wanahabari kwani kufanya hivyo ni makosa makubwa

Aidha amesema kulikuwa hakuna haja ya kumkamata mchungaji wake kwa namna aliyofanya badala yake angempa wito kufika ofisini kwake au ofisi ya usajili wa vyama vya kijamii.

Pia anashangaa kwanini viongozi wa Makanisa kama KKKT au RC na baadhi ya Masheikh wa Misikiti mikubwa hupewa
wito kufika ofisini panapokuwa na tatizo na sio kuwadhalilisha kama alivyofanya kanisani kwake,kwake anajua akifanya hivyo kwa makanisa hayo hawezi mziki wake.

Aidha amesema Wizara ya mambo ya ndani ndio inayoongoza kwa matatizo tangu kupata uhuru ambapo mawaziri hukaa kwa wastani wa miaka 2 na kuondolewa ambapo tangu Uhuru Wizara hio imekuwa na takribani Mawaziri 60 tofauti na Wizara zingine.

Mwisho ameahidi akirudi atafanya Press conference kuongelea suala hili mara atakaporudi kutoka Ughaibuni.

Zaidi sikiliza audio

 
Ni kweli kwani kuna maeneo yakiimani yanaitaji sana heshima kama kuna jambo kuna njia zkutumia sio unaingia kama umeenda kwenye kibanda cha gongo kwani unawapa butwa watu ambao hawajui kinachoendelea
 
Hivi huyu kiongozi wa dini ana upeo hafifu kiasi gani, kwa kutofautisha serikali na waziri?

Asijidanganye hata siku1 serikali kuitishia nyau! Wenzake wanafanya kazi kama timu1.

Asifikirie kuna mtu atamsaidia kumkaripia waziri hapo.

Pia aelewe kuwa haya madhehebu yao ya kilokole yanafuatiliwa kwa karibu sana sasa hivi, maana serikali imeanza kufumbua macho juu ya dhuluma wafanyiwazo raia kwenye pazia la hawa wajasilia dini.

Wawaulize wenzao wa Rwanda walivyofanyiwa, sidhani hata kama angelipayuka kama alivyofanya kutaka kuitunishia msuli serikali.
 
Hivi huyu kiongozi wa dini ana upeo hafifu kiasi gani, kwa kutofautisha serikali na waziri?

Asijidanganye hata siku1 serikali kuitishia nyau! Wenzake wanafanya kazi kama timu1.

Asifikirie kuna mtu atamsaidia kumkaripia waziri hapo.

Pia aelewe kuwa haya madhehebu yao ya kilokole yanafuatiliwa kwa karibu sana sasa hivi, maana serikali imeanza kufumbua macho juu ya dhuluma wafanyiwazo raia kwenye pazia la hawa wajasilia dini.

Wawaulize wenzao wa Rwanda walivyofanyiwa, sidhani hata kama angelipayuka kama alivyofanya kutaka kuitunishia msuli serikali.
Usajili wa makanisa yao wenyewe umeandikwa kwa pencil kufuta ni dakika 0 tu..
 
Back
Top Bottom