Kiongozi Wa Juu Wajiuzulu Kwa Ufisadi Pia?

Haika

JF-Expert Member
Mar 3, 2008
2,348
559
Naomba kuuliza swali:
Je viongozi wa juu kama rais, Rais wa Zbar wakitajwa kwenye kashfa wana JF mnaweza kuwashadidia hadi wajiuzulu?
Mfano kama ripoti ya Richmond ambayo haikusomwa, imevuja mtaani na inamtaja Rais kuwa anahusika moja kwa moja na sakata hilo, je kuna mechanism itakayoweza kuuliza maswali? au tutapata kigugumizi?
Je akiondoka (mfano) itakuwaje? nani atashika nchi?
Kwa kweli nimewaza sana hadi naogopa, manake tusijeanza kugombea madaraka hadi tukawa kama Somalia, hatutawaliki, manake kama mnavyojua katiba yetu inaviraka ambavyo vinatafsirika kwa kila dizaini, kutegemea unazungumzia nini, na unalenga nini.
 
God forbid my sistah!! That we should end up like Somalia and the likes
Lakini kama ikibidi nae atastaafu. It is said kuwa JK ndiye anayewahimiza hawa jamaa wastaafu....something is cooking, labda na yeye yuko on the way out... hii ni regime ya kujiuzulu, kama ya Baba wa taifa ilivyokuwa ya kung'atuka. TZ setting the trend, kama kawa
 
Naomba kuuliza swali:
Je viongozi wa juu kama rais, Rais wa Zbar wakitajwa kwenye kashfa wana JF mnaweza kuwashadidia hadi wajiuzulu?
Mfano kama ripoti ya Richmond ambayo haikusomwa, imevuja mtaani na inamtaja Rais kuwa anahusika moja kwa moja na sakata hilo, je kuna mechanism itakayoweza kuuliza maswali? au tutapata kigugumizi?
Je akiondoka (mfano) itakuwaje? nani atashika nchi?
Kwa kweli nimewaza sana hadi naogopa, manake tusijeanza kugombea madaraka hadi tukawa kama Somalia, hatutawaliki, manake kama mnavyojua katiba yetu inaviraka ambavyo vinatafsirika kwa kila dizaini, kutegemea unazungumzia nini, na unalenga nini.


Haika,
Kama una data wewe lete tu, watashambuliwa mpaka waondoke. Lolote linaloingia hapa haliachiwi mpaka liive na kutumbuka.

Katiba inajitosheleza kwa nani atashika madaraka badala yao kwa hiyo hilo wala lisikupe shida. Somalia shida yao sio ufisadi, shida yao kubwa ni ukabila hasa ule wa kundi moja kujiona ni bora kuliko lingine na kutaka kutawala wenzao.
 
Haika, kwa upande wa Rais kweli ni kigugumizi, kwani tumemuona Mkapa watu walisema lakini wapi, tatizo ni kwamba katiba yetu inaonesha kuwa Rais anakuwa na madaraka makubwa, ujue yeye ndiye anayewateua mawaziri, wakurugenzi wakuu wa mikoa hata wilaya
 
Naomba kuuliza swali:
Je viongozi wa juu kama rais, Rais wa Zbar wakitajwa kwenye kashfa wana JF mnaweza kuwashadidia hadi wajiuzulu?

Hili halina tatizo hapa JF. Leta data za kutosha za kujenga hoja.

je kuna mechanism itakayoweza kuuliza maswali? au tutapata kigugumizi?

Hapa naomba waoijua katiba na sheria za nchi vizuri watoe mwongozo. Nafikiri hili ndio swali la msingi sana iwapo Raisi anatakiwa achukuliwe hatua.

tusijeanza kugombea madaraka hadi tukawa kama Somalia

Hali ya Somalia sidhani kama inaweza kutokea katika nchi yetu labda yaktokea mapinduzi ya kijeshi, hivyo usiwe na hofu!

Nafikiri mjadala uende kwenye swali la msingi, "je kuna mechanism itakayoweza kuuliza maswali?"
 
Naomba kuuliza swali:
Je viongozi wa juu kama rais, Rais wa Zbar wakitajwa kwenye kashfa wana JF mnaweza kuwashadidia hadi wajiuzulu?
Mfano kama ripoti ya Richmond ambayo haikusomwa, imevuja mtaani na inamtaja Rais kuwa anahusika moja kwa moja na sakata hilo, je kuna mechanism itakayoweza kuuliza maswali? au tutapata kigugumizi?
Je akiondoka (mfano) itakuwaje? nani atashika nchi?
Kwa kweli nimewaza sana hadi naogopa, manake tusijeanza kugombea madaraka hadi tukawa kama Somalia, hatutawaliki, manake kama mnavyojua katiba yetu inaviraka ambavyo vinatafsirika kwa kila dizaini, kutegemea unazungumzia nini, na unalenga nini.


Haika hata kama Rais ataachia ngazi,wapo wa TZ wengi wenye uwezo wa kuongoza na tukafika salama tuendako.
Soma katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 37:5

(5) Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais
kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu
kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa
kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais
ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi
cha miaka mitano na kwa masharti yaliyoelezwa katika ibara ya
40, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka
Rais atapendekeza jina la mtu atakae kuwa Makamu wa Rais na
uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua
asilimia hamsini ya Wabunge wote.
 
Back
Top Bottom