Kiongozi wa Juu BAVICHA amhujumu Dr Slaa

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Hatimaye kile kilichokuwa kumejificha sasa kimewekwa wazi kwamba Kiongozi mmoja wa ngazi ya juu wa Baraza la vijana-CHADEMA BAVICHA ndiye yuko katika harakati za kumchafua Kiongozi wa upinzani nchini Dr Wilbroad Slaa na ameapa kumuangamiza kisiasa kiongozi huyo kipenzi cha watanzania.

Taarifa za uhakika zilizoibuliwa na gazeti la Tanzania Daima Jumapili zinadai mkakati huo uliopangwa kwa ustadi mkubwa ulianza na Katibu wa Itikadi na uenezi Nape Nauye kuhoji sababu za Dr Slaa kumiliki kadi ya CCM huku akiwa kiongozi wa upinzani.

Baada ya tamko la Nape kundi hilo linaloongozwa na kiongozi huyo wa BAVICHA lilipokea mamilioni ya fedha kutoka kwa wanamkakati hao na kutakiwa kutembea nchi nzima kushinikiza Dr Slaa afukuzwe CHADEMA.

Mkakati wa kwanza ulianza juzi kwa mtu anayejiita mjumbe wa mkutano mkuu wa CHADEMA Eddo Mwamalala kuitisha mkutano na waandishi Dar na kutaka Dr Slaa atimuliwe mara moja kwa kumiliki kadi ya CCM.Kundi hilo litaendelea na ziara hizo wiki ijayo katika mikoa kadhaa.

Taarifa zinadai Dr Slaa amekuwa mwiba mchungu kwa chama tawala na chama hicho kiko hatarini kuondolewa madarakani.Inadaiwa mipango mbalimbali imepangwa kuhujumu CHADEMA na mkakati wa kwanza ni kumdhoofisha Dr Slaa.

Ingawa gazeti hilo halijamtaja kiongozi huyo wa BAVICHA lakini ni kwa muda mrefu sasa Makamu Mkiti wa BAVICHA Juliana Shonza amekuwa akihusishwa na makundi yanayomhujumu Mkiti wa BAVICHA John Heche.


Source: Tanzania Daima
Mkuu Pasco na Wanajamvi, kwanza kabisa niweke wazi kuwa hili suala la usaliti ndani ya CHADEMA limeshwahi kuzungumziwa hapa jamvini kwa nyuzi kadha wa kadha. Wengine tulitoa ushauri wa bure kabisa kuhusu hali inayoinyemelea CHADEMA.

Mtakumbuka kuwa kumekuwa na nyuzi kutoka kwa Tuntemeke zikishadidia sana uhasama kati ya wanachama.
Sisi tusiochukua upande tulisema wazi kuwa lipo tatizo kwasababu huyu Tuntemeke ingawa anafinyanga taarifa zake lakini ni insider ndani ya CHADEMA na anaweza kufanya spinning hatari zaidi.

Kulitokea mtafaruku ndani ya CHADEMA ukimhusisha Shibuda. Hilo halikuwa tatizo, hatari kubwa ni pale Makamu Mwenyekiti wa BAVICHA Juliana Shonza ambaye bila kujali itifaki, adabu wala utaratibu alikwenda katika vyombo vya habari na kumdhalilisha Mwenyekiti wa BAVICHA katika uso wa dunia.

Suala la Juliana Shonza lilileta mtafaruku mkubwa sana kuliko la Shibuda. Si kwamba lilionyesha mpasauko ndani ya chama bali lilieleza jinsi gani kuna uhasama na kuhasimiana ndani ya chama.
Tulisimama tukaonya kuwa ni lazima hatua zichukuliwe kuleta nidhamu ndani ya chama.

Juliana kwa umri, ufahamu wa kisiasa na mengineyo si tishio kwa uhai wa chama.
Kwa bahati mbaya nguvu hiyo si yake ina vigogo wazito sana na yeye anatumika kama Conduit.

Wakati tunaonya, wakatoke watu ndani ya CHADEMA na hapa ni Dr Kitila Mkumbo na kushauri kuwa vijana wafundwe.
Katika makala yake Dr Kitila haukonekana kusimama kati na kati na kueleza ukweli wa kilichotokea.

Alipindua issue yote na kuifanya kama Ugomvi wa Heche na Juliana. Tulisimama tena na kuonye kuwa hakukuwa na tatizo BAVICHA bali tatizo ni Juliana anayetumika kukiharibu chama.
CHADEMA wakapuuzia ushauri pengine kwa kuchukua ushauri wa mshauri wa chama. It's ok!

Tunafahamu miezi michache iliyopita kulikuw na kauli zilizoonyesha mtafaruku ndani ya chama huku kila mmoja akienda kivyake. Wengine wakiiimarisha chama huko matawini, wengine M4C na wengine wakienda solo wakitangaza nia zao za uongozi. Kilichotokea ni kuchanganya mambo.
Tukaonya pia kuwa kuna dalili za mgawanyiko ndani ya CHADEMA, hilo nalo likapuuzwa.

Kwa taarifa kama iliyopo hapao juu, ni dhahiri kuwa ule mtandao unaotumika ndani ya BAVICHA na baadhi ya vigogo kutaka kusalitiana sasa ni dhahiri.

Nafahamu fika wengi wasingependa kusikia haya, ninachoweza kusema ni kuwa tahadhari imetolewa sana bila kufikiriwa na tunaandika kusaidia vyama kama tulivyowahi kuonya CCM, CUF au TLP.

Hapa ilipofikia ni too late kumwajibisha Juliana hata kama itathibitika. Kinachotakiwa kifanyike sasa ni kushirikiana na Juliana ili kujua wahujumu wa chama na mtandao mzima unaovuruga chama kwa kasi ya juu sana.

Unapokuwa na wasaliti hilo tu linatosha kuwa kiingilio cha maandui. Ni kwa mantiki hiyo Nape anachomeka hoja zake kwa kutambua kuwa kuna udhaifu tayari. Hata kama hoja zake ni dhaifu na za kitoto katika mazingira ambayo ni volatile kama yalivyo ndani ya CHADEMA hilo tu linatosha kuleta sintofaham.

Kuna watu na si CCM ndani ya CHADEMA wanaoona Dr Slaa ni kikwazo cha kufikia ndoto zao. Hawa ndio wanatumia damu changa ya akina Juliana kuleta udhaifu ndani ya chama. Ukisoma maandishi yao na hoja zao wanaonekana kuwa waumini wa demokrasia, wasichokubali nyuma ya mlango ni demokrasia kuchukua mkondo wake.

Nadhani Dr Slaa kama kiongozi mwingine yoyote anapaswa kuwa scrutinized, questioned etc. Na wala sidhani kama ana kinga ya aina yoyote as political leader. He is as vulnerable as any other politician.

Kitu cha muhimu ni kupambana ndani ya chama kwa hoja na mantiki. Kinachotokea sasa hivi ni usaliti unaoweza kuua chama kabisa. Usaliti unafanywa na viongozi wawili au watatu kwa kutumia vijana wasio na ufahamu kama Juliana.

Wanajamvi tatizo sio Nape, ni viongozi wenye matamanio na wanaotumia nafasi zao na uzoefu wao ndani ya chama kutaka kufikia malengo yao kwa kuwatumia akina Juliana Shonza.
Hawa ndio tatizo na wanapaswa kushughulikiwa mapema, ingawa imechelewa sana.

CHADEMA mnabahati ya kupewa ushauri bure, kwa bahati mbaya siku hizi mumeweka pamba masikioni na kufunga vitambaa machoni. Mnafanya kazi kimakao makuu na hamna contact na Political base yenu, hamna contact wala discussion na forum gharama zake ni kubwa sana.
 
Ahsante mkuu Molemo.

Mimi kila siku huwa nasema hawa mamluki si wakuwachekea hata kidogo kwani wamezoea sana kuendekeza tamaa na majungu na fitina kwa lengo la kukiangamiza chama, yani walivyo na akili za kiduku wanadiriki kumchafua Dr.Slaa alafu upande wa pili wapo kumsafisha Shibuda,...ooh My God!!! Hivi hawa watu mind zao zipo sound kweli?

Jaman tusiache kamwe kuwachana ukweli wajinga hawa.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo hawajui hiki ni kizazi cha dotcom, hatudanganyiki! Halafu kwanini huyu nape siku hizi anajituma sana kuanzisha thread kila siku?
Kuna kikao kimoja cha CCM ambacho moja ya maazimio yake ilikuwa kuhamasisha vijana wao kujaribu kujibu hoja za CDM hasa hapa JF. Kama unakumbuka, wamewahi hata kuihusisha JF na CDM. Hata hivyo wasipokuwa makini harakati zao hizi zinaweza kuwabomoa zaidi badala ya kuwajenga.
 
Ehe! kile tulichokiandika hapa mara nyingi sana kuhusiana na CDM, Uongozi wa chama na BAVICHA sasa kinaonekana kutimia.
Hao waliotajwa ni vidagaa, nina wasi wasi wapo wazee wakubwa wenzetu hapa jamvini watahusishwa moja kwa moja kwa ushiriki wao.
 
Ukishakuwa na akili za nguruwe we zako ni kwenye uchafu tuu, Nape, na yule kipipa wa mtera, hawana jipya wala hawajui wanachokifanya, leo hii hata akiondoka Slaa bado tutawahoji wao kama chama tawala maisha bora yako wapi? elimu bora i wapi? nini nafasi ya mzawa wa Tanganyika katika nchi yake...!
Muda wanaotumia hawajamaa kupambana na CDM wangeutumia vizuri kudili na watendaji waajiriwa wa chama chao lau tungewaelewa..
 
Hakika nawaambieni ya kwamba hawa ccm mwisho wao kwa Watanzania imefika! Sasa angalieni wanachofanya wakijitahidi kueneza chuki yao na sasa hawaoni kila kitu kinalic,mwisho ya siku ccm itakuwa kama ile chama ya majirani wetu hapo Kenya,ile chama cha KANU ilianza hivi na hatimaye siku ya siku imetokomea masikioni mwa Wakenya na haisikiki tena na hata nafikiri haitarudi kusikika! Sasa ccm ndiyo wanachosubiria na nawaambieni ya kwamba tuombe uzima na tutaona kikomo ya chama hiki! Eti miaka 51 ya uhuru wakati kuna Watanzania wanakufa njaa na kiu ya maji halafu mbado mnasema ccm itakuwa hai tu! Kwangu binafsi na mtazamo wangu ni kwamba natamani ccm isiwepo tena masikioni mwa Watanganyika!
 
Hawawezi, wanatafuta matatizo tu na kuchukiwa na umma. Rushwa inaharibu uwezo mtambuka. Hao ni maamuma tayari, ingawa wanavuvuzela. CDM iko makini, sio choo cha standi ya basi.
yap kiukweli hawa wala rushwa na chama chao cha rushwa na wasio na mawazo mtambuka watashindwa
 
Hizo mbinu zimepitwa na wakati CCM haina mbinu nyingine mpaka hii dhaifu?

Hatimaye kile kilichokuwa kumejificha sasa kimewekwa wazi kwamba Kiongozi mmoja wa ngazi ya juu wa Baraza la vijana-CHADEMA BAVICHA ndiye yuko katika harakati za kumchafua Kiongozi wa upinzani nchini Dr Wilbroad Slaa na ameapa kumuangamiza kisiasa kiongozi huyo kipenzi cha watanzania.

Taarifa za uhakika zilizoibuliwa na gazeti la Tanzania Daima Jumapili zinadai mkakati huo uliopangwa kwa ustadi mkubwa ulianza na Katibu wa Itikadi na uenezi Nape Nauye kuhoji sababu za Dr Slaa kumiliki kadi ya CCM huku akiwa kiongozi wa upinzani.

Baada ya tamko la Nape kundi hilo linaloongozwa na kiongozi huyo wa BAVICHA lilipokea mamilioni ya fedha kutoka kwa wanamkakati hao na kutakiwa kutembea nchi nzima kushinikiza Dr Slaa afukuzwe CHADEMA.

Mkakati wa kwanza ulianza juzi kwa mtu anayejiita mjumbe wa mkutano mkuu wa CHADEMA Eddo Makata kuitisha mkutano na waandishi Dar na kutaka Dr Slaa atimuliwe mara moja kwa kumiliki kadi ya CCM.Kundi hilo litaendelea na ziara hizo wiki ijayo katika mikoa kadhaa.

Taarifa zinadai Dr Slaa amekuwa mwiba mchungu kwa chama tawala na chama hicho kiko hatarini kuondolewa madarakani.Inadaiwa mipango mbalimbali imepangwa kuhujumu CHADEMA na mkakati wa kwanza ni kumdhoofisha Dr Slaa.

Ingawa gazeti hilo halijamtaja kiongozi huyo wa BAVICHA lakini ni kwa muda mrefu sasa Makamu Mkiti wa BAVICHA Juliana Shonza amekuwa akihusishwa na makundi yanayomhujumu Mkiti wa BAVICHA John Heche.


Source: Tanzania Daima
 
Hakika nawaambieni ya kwamba hawa ccm mwisho wao kwa Watanzania imefika! Sasa angalieni wanachofanya wakijitahidi kueneza chuki yao na sasa hawaoni kila kitu kinalic,mwisho ya siku ccm itakuwa kama ile chama ya majirani wetu hapo Kenya,ile chama cha KANU ilianza hivi na hatimaye siku ya siku imetokomea masikioni mwa Wakenya na haisikiki tena na hata nafikiri haitarudi kusikika! Sasa ccm ndiyo wanachosubiria na nawaambieni ya kwamba tuombe uzima na tutaona kikomo ya chama hiki! Eti miaka 51 ya uhuru wakati kuna Watanzania wanakufa njaa na kiu ya maji halafu mbado mnasema ccm itakuwa hai tu! Kwangu binafsi na mtazamo wangu ni kwamba natamani ccm isiwepo tena masikioni mwa Watanganyika!

Mkuu LiverpoolFC tatizo hapa ni hawa genge la mamluki ndani ya BAVICHA.
 
Last edited by a moderator:
Hatimaye kile kilichokuwa kumejificha sasa kimewekwa wazi kwamba Kiongozi mmoja wa ngazi ya juu wa Baraza la vijana-CHADEMA BAVICHA ndiye yuko katika harakati za kumchafua Kiongozi wa upinzani nchini Dr Wilbroad Slaa na ameapa kumuangamiza kisiasa kiongozi huyo kipenzi cha watanzania.

Taarifa za uhakika zilizoibuliwa na gazeti la Tanzania Daima Jumapili zinadai mkakati huo uliopangwa kwa ustadi mkubwa ulianza na Katibu wa Itikadi na uenezi Nape Nauye kuhoji sababu za Dr Slaa kumiliki kadi ya CCM huku akiwa kiongozi wa upinzani.

Baada ya tamko la Nape kundi hilo linaloongozwa na kiongozi huyo wa BAVICHA lilipokea mamilioni ya fedha kutoka kwa wanamkakati hao na kutakiwa kutembea nchi nzima kushinikiza Dr Slaa afukuzwe CHADEMA.

Mkakati wa kwanza ulianza juzi kwa mtu anayejiita mjumbe wa mkutano mkuu wa CHADEMA Eddo Makata kuitisha mkutano na waandishi Dar na kutaka Dr Slaa atimuliwe mara moja kwa kumiliki kadi ya CCM.Kundi hilo litaendelea na ziara hizo wiki ijayo katika mikoa kadhaa.

Taarifa zinadai Dr Slaa amekuwa mwiba mchungu kwa chama tawala na chama hicho kiko hatarini kuondolewa madarakani.Inadaiwa mipango mbalimbali imepangwa kuhujumu CHADEMA na mkakati wa kwanza ni kumdhoofisha Dr Slaa.

Ingawa gazeti hilo halijamtaja kiongozi huyo wa BAVICHA lakini ni kwa muda mrefu sasa Makamu Mkiti wa BAVICHA Juliana Shonza amekuwa akihusishwa na makundi yanayomhujumu Mkiti wa BAVICHA John Heche.


Source: Tanzania Daima


Asante Mkuu MOLEMO kwa Taarifa

Mkuu kwa utafiti wako unaweza kujua ni Nani huyo tumchambue humu
 
Mbona kazi waliyopewa ni ngumu sana haitatekelezeka kama ahadi zao zisizotekelezeka.
 
Matendo huzungumza zaidi ya maneno. CDM bila Slaa isingekuwa kama kilivyo hivi sasa. Karatu jimbo aliloliwakilisha hadi sasa ni miaka zaidi ya miaka 17 lipo upinzani. Kila uchaguzi unapotokea, CDM huongeza idadi ya wabunge na CCM hupungukiwa idadi ya wabunge. Halafu anatokea mjinga moja kutubabaisha kuwa Slaa kuendelea kuwa na kadi ya CCM ni msaliti wa CDM. Wote wenye mawazo haya ya kishetani washindwe maana kizazi kipya hakidanganyiki hivyo. Nawashauri CCM waendelee kupoteza muda wao bure badala ya kujikita katika mambo ya msingi. Pia kama kuna yeyote ndani ya CDM anashirikiana na CCM katika mchezo huu mchafu usio na tija, CDM ichunguze na imtimue haraka. CDM ni lazima ijipambanue umakini wake na vyama bongo lala.
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom