Kiongozi Mwandamizi wa CHADEMA akutana na Kikwete, Kinana na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa

Katiba ni kila kitu wewe, acha ujinga
Kenya mnasema wana Katiba nzuri, je wamemaliza matatizo?

Vipi SAfrica unadhani wananchi wana raha na nchi yao inayosifika kuwa na Katiba bora kabisa?

Fanya kazi kijana upate hela, Katiba ni struggle kati ya waliopo madarakani dhidi ya wanaotaka kuingia madarakani
 
Kenya mnasema wana Katiba nzuri, je wamemaliza matatizo?

Vipi SAfrica unadhani wananchi wana raha na nchi yao inayosifika kuwa na Katiba bora kabisa?

Fanya kazi kijana upate hela, Katiba ni struggle kati ya waliopo madarakani dhidi ya wanaotaka kuingia madarakani
Kenya na Tanzania is like day and night, mambo ya mafisadi au watawala kujifanyia wanavyotaka kama kubambikia watu kesi , wizi wa kuraau kuonea watu Kenya wamemaliza huo upuuzi, muulize Zuma na uraisi wake kaenda jela
 
Abunuasi...... Mbowe sio gaidi aachiwe haraka na hii serikali ya kishetani
 
Yaani huyo magu wapainzani angewaachia ATA viti50 vilivyobaki wakachukua hizi kerere zote za Katiba tusingezisikia, maana na wapainzani wangekuwa busy kwenye majimbo yao, kuhusu Mbowe serikali ilitumia mabavu, na Mbowe hakuna Sheria yeyote aliyofanya, Sasa hii Kesi imeikalia vibaya serikali, na SSH Hadi wanashindwa waiteme vipi
Magufuli alitumia nguvu nyingi sana kutesa wapinzani angekuwa hai ingetakiwa awaombe msamaha, upinzani ni muhimu imagine Ile nunua nunua jiuzulu rudia uchaguzi was a st.upid idea na aibu kwa nchi yetu, Yani serikali ikawafanya watanzania wenzenu maadui kweli?
Tena Magu wakaharibu na uchaguzi na kusahau kuwa inahitajika idadi ya wabunge kiasi Ili nchi ipate misaada wakaja kugutuka too late ndio kuwapeleka kina Halima mdee kinguvu na kwa kutokufata taratibu.
So upinzani wakipata wabunge hata 70 huwakumbusha serikali wajibu wao ona bunge la Sasa hivi ni hasara kwa taifa letu.
So upinzani iache ubishi wakae na serikali tujemge nchi mama Samia hana Cha kupoteza na hata asipomtoa huyo mbowe atakuwa Rais kwa hyo miaka kumi upinzani ndio utapoteza zaidi, CDM waache ubishi na kususa Susa oooh fisi ukimsusia bucha utaumia mazima
 
Magufuli alitumia nguvu nyingi sana kutesa wapinzani angekuwa hai ingetakiwa awaombe msamaha, upinzani ni muhimu imagine Ile nunua nunua jiuzulu rudia uchaguzi was a st.upid idea na aibu kwa nchi yetu, Yani serikali ikawafanya watanzania wenzenu maadui kweli?
Tena Magu wakaharibu na uchaguzi na kusahau kuwa inahitajika idadi ya wabunge kiasi Ili nchi ipate misaada wakaja kugutuka too late ndio kuwapeleka kina Halima mdee kinguvu na kwa kutokufata taratibu.
So upinzani wakipata wabunge hata 70 huwakumbusha serikali wajibu wao ona bunge la Sasa hivi ni hasara kwa taifa letu.
So upinzani iache ubishi wakae na serikali tujemge nchi mama Samia hana Cha kupoteza na hata asipomtoa huyo mbowe atakuwa Rais kwa hyo miaka kumi upinzani ndio utapoteza zaidi, CDM waache ubishi na kususa Susa oooh fisi ukimsusia bucha utaumia mazima
Magu sijui alikuwa na roho gani,sahivi Bunge limedoda hatri yaaani hatari ata Mimi siwez angalia Hilo Bunge, Samia hasipomtoa Mbowe hatatawala kwa amani mabeberu hawatampa pesa, serikali yake inaitaji pesa maana hali sio poa, na misaada kutoka west imepungua saaanaa, Yaani kwa Mbowe Samia atasanda, mabeberu walimpiga mkwara Kagame Hadi akamuachia yule dada mpinzani
 
Basi tuachie watuhumiwa wote, maana haiwezekani baadhi waachiwe wengine wahenyeke na kesi wakati mahakama ni hizohizo
Yote haya kwa sababu tumesema kwenye kesi ya Mbowe, Mahakama sio ya kuitegemea sana? Hata saa mbovu, kwa siku inapatia mara mbili. Hamna aliyesema kuwa watuhumiwa wote ni innocent. Vile vile si wote wanaotiwa hatiani ni wakosaji.

Amandla...
 
Kwa mujibu wa katiba DPP hapaswi kuchukua amri kutoka kwa mtu yeyote afanyapo majukumu yake.

Ukiona watu wanataka rais amwagize DPP afute shauri fulani basi kimsingi wanakuwa wanataka rais avunje katiba
Dpp ni mteule wa Rais...hivyo kufuata maagizo ya bosi wake sio kuvunja katiba.
 
Jamani, ieleweke vizuri kuwa hakuna h
Jitihada za kumaliza kesi ya ugaidi na uhujumu uchumi inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mheshimiwa Freeman Mbowe, zinaendelea “nyuma ya pazia,” ambapo taarifa za uhakika zinaeleza kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika, amekutana na Rais Mstaafu Jakaya Kikwete, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Abdulrahman Kinana, na Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Diwani Athumani.

Haijaweza kufahamika kama jitihada hizo ni za Mnyika binafsi au zina baraka ya chama hicho, ambacho kwenye mitandao ya kijamii kimetanabaisha kuwa hakitaki suluhu yoyote kuhusiana na kesi hiyo.

Taarifa hizo zinaeleza kwamba kimsingi Mama Samia Suluhu aliridhia ombi la kuachiwa kwa Mheshimiwa Mbowe na ilitarajiwa aachiwe kwa “nolle prosequi” (tamko la nia ya kutoendelea na mashtaka) ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) lakini “yaliyojiri kabla, wakati na baada ya mkutano wa vyama vya siasa huko Dodoma” yalipelekea mpango huo kukwama.

Licha ya jitihada hizo za Mnyika, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Masoud Othman nae aliwasilisha maombi ya Chadema kwa Mama Samia, na akashauri Mheshimiwa Mbowe aachiwe bila masharti yoyote.

Uamuzi wa Chadema kususia mkutano huo wa vyama vya siasa huko Dodoma ambao ulifunguliwa na Mama Samia, inatajwa kuwa moja ya sababu zilizopelekea kukwama kwa mpango huo wa kumwachia Mheshimiwa Mbowe.

Taarifa hizi zinakinzana na kauli zinazoongewa na viongozi na wafuasi wa chama hicho kuwa “hawako tayari kuomba Mheshimiwa Mbowe aachiwe” kwa sababu wanaamini kuwa hana hatia na mashtaka dhidi yake ni ya kutungwa.

Yawezekana tofauti hizo kati ya “kinachoendelea faraghani” na “kinachoongelewa hadharani” zikawa ni mkakati wa Chadema hasa ikizingatiwa kuwa wafuasi wengi wa chama hicho hawaafiki kabisa wazo la kuomba Mheshimiwa Mbowe aachiwe. Moja ya sababu zinazochangia “msimamo huo mkali” ni shinikizo la “wanaharakati wa mtandaoni” ambao wanapinga vikali siasa za maridhiano kati ya chama tawala CCM na vyama vya upinzani.

Hata hivyo, suala hilo la kesi ya Mbowe “limevamiwa” pia na kundi moja ndani ya CCM linalompinga Mama Samia, na ambalo linaiona kesi hiyo dhidi ya Mheshimiwa Mbowe kuwa yenye manufaa kwa kundi hilo kwa sababu inatoa taswira mbaya kuhusu Mama Samia.

Nihitimishe kwa kutanabaisha kuwa haitokuwa jambo la kushangaza endapo Mheshimiwa Mnyika atakanusha taarifa hizi kwa sababu “zinaweza kumletea tabu” katika chama chake.

Jumanne njema
Jamani, ieleweke vizuri kuwa hakuna mwanachadema yeyote adiyependa Mwenyekiti kuachiwa. Ila kinachokataliwa na wanachadema ni kumtaka Mh. Rais amsamehe Mwenyekiti kana kwamba Mbowe ni mkosaji tayari au kumtaka Mwenyekiti Mbowe aombe msamaha. Kama ni serikali kupitia kwa DPP wataifuta kesi bila masharti hakuna shida. Kama mkutano huo wa Mnyika na watajwa ni kweli na unataka kuweka masharti ili Mbowe aachiwe basi itakuwa ni jambo la kuhuzunisha. Tunataka Mwenyekiti atoke mahabusu na aendelee na majukumu yake bila kufungwa breki na lolote ukiachia sheria za nchi ambazo siku zote Mbowe amekuwa wa kwanza kuziheshimu.
 
Dpp ni mteule wa Rais...hivyo kufuata maagizo ya bosi wake sio kuvunja katiba.
DPP ni Mteule wa rais lakini katiba imesema kuwa DPP hatoingiliwa katika majukumu yake. Rais kumuagiza DPP kuinfluence kesi ni kosa la kisheria, maana kama ingekuwa hivyo basi kesi zingechezewa sana kutegemea na utashi wa rais
 
DPP ni Mteule wa rais lakini katiba imesema kuwa DPP hatoingiliwa katika majukumu yake. Rais kumuagiza DPP kuinfluence kesi ni kosa la kisheria, maana kama ingekuwa hivyo basi kesi zingechezewa sana kutegemea na utashi wa rais
Wakati Hayati Magufuli anamwagiza Dpp wake akutane na watuhumiwa wa uhujumu uchumi ili watakaokubali walipe fidia na kupunguziwa adhabu na Dpp akatii hilo agizo....je mahakama iliingiliwa Uhuru wake au Dpp aliingiliwa majukumu yake?...
 
Nilisema na ninarudia tena, hii kesi itakwenda kwenye historia ya huyu mama wa kizanzibar kama changamoto kubwa kuliko zote katika maisha yake.

Asubiri 2025 atakapoanza anza kutuhubiri kuacha siasa za hasira na visasi.
 
Kama walikutana wote kwa pamoja ni dhahiri kuwa joto kubwa sana kutoka nje kuhusu hali ya siasa zetu. Uenda SSH anakemewa vikali na akina EU na USA. Hivyo akina JK na Kinana wanatumika kuzima moto wa CDM. Mbowe aendelee na kesi hii ili tuona mwisho wa SIRRO na genge lake.
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom