Sam Gidori
Senior Member
- Sep 7, 2020
- 165
- 414
Kiongozi wa upinzani nchini Jamhuri ya Kongo (Congo-Brazzaville) na mgombea wa kiti cha urais amefariki kwa COVID-19 ikiwa ni saa chache tu baada ya vituo vya uchaguzi kufungwa.
Guy-Brice Parfait Kolelas alifariki akiwa kwenye ndege akipelekwa nchini Ufaransa kwa matibabu baada ya kuumwa. Saa chache kabla, mgombea huyo alionekana katika video iliyosambaa katika mitandao ya kijamii akiwasihi wafuasi wake kumpigia kura akisema kuwa anapambania uhai wake kutokana na maambukizi ya corona.
Kolelas ni mmoja ya wapinzani 6 waliokuwa wakipambana na kiongozi wa nchi hiyo, Sassou Nguesso ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1979, isipokuwa kwa kipindi cha miaka 5 baada ya kushindwa uchaguzi wa mwaka 1992.
Sheria za uchaguzi za nchi hiyo hazibadilishi matokeo ikiwa mgombea mmoja atafariki. Congo-Brazzavile imeshuhudia visa 9,000 vya maambukizi ya virusi vya corona na vifo 130.
Chanzo: BBC
Guy-Brice Parfait Kolelas alifariki akiwa kwenye ndege akipelekwa nchini Ufaransa kwa matibabu baada ya kuumwa. Saa chache kabla, mgombea huyo alionekana katika video iliyosambaa katika mitandao ya kijamii akiwasihi wafuasi wake kumpigia kura akisema kuwa anapambania uhai wake kutokana na maambukizi ya corona.
Kolelas ni mmoja ya wapinzani 6 waliokuwa wakipambana na kiongozi wa nchi hiyo, Sassou Nguesso ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1979, isipokuwa kwa kipindi cha miaka 5 baada ya kushindwa uchaguzi wa mwaka 1992.
Sheria za uchaguzi za nchi hiyo hazibadilishi matokeo ikiwa mgombea mmoja atafariki. Congo-Brazzavile imeshuhudia visa 9,000 vya maambukizi ya virusi vya corona na vifo 130.
Chanzo: BBC