sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 133
[h=2][/h] Jumapili, Septemba 02, 2012 07:46 Na Eliya Mbonea, Monduli
Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa
MBUNGE WA Jimbo la Monduli, Edward Lowassa amesema kiongozi anayeaminiwa na wananchi wake hapaswi kuwa mtu wa kulialia na kuomba msaada badala yake anatakiwa kufikiri na kutoa uamuzi wa maisha ya watu wake. Lowassa ambaye pia ni Laigwanani Mkuu wa Wamaasai alisema hayo jana kwenye mkutano wa siku mbili uliowakutanisha Malaigwanani kutoka nchi nzima kujadili tatizo la ardhi, Katiba Mpya na suala la elimu kwa jamii hiyo.
Malaigwanani si viongozi wa kulialia, kuombaomba msaada ni watu wa kufikiri na kusema tumechoka na hali na sasa tunaamua kufanya jambo moja, mbili na tatu hatuwezi kuvumilia kuona watu wetu wakiendelea kuumia kila siku wakati sisi ndio viongozi wao, sisi siyo watu wa kulialia, alisema Lowassa na kuongeza:
Lazima leo tuseme kauli ya kuwasaidia wenzetu wa Ngorongoro hakuna kiongozi wa Kimasaai aliyeaminiwa kufanya kazi kisha akawa analialia na kuomba msaada. Ardhi kwa Ngorongoro imekuwa tatizo kubwa nataka leo hapa tulizungumze kwa dhati.
Tumechoka kusikia migogoro ya ardhi, leo naomba tusaidiane tuseme wenyewe hapa tufanye nini, alisema Lowassa.
Akieleza maeneo mengine yenye migogoro kwa wafugaji hao, Lowassa aliutaja Mkoa wa Morogoro na kuwataka viongozi wa kimila waliotoka mkoani humo kubainisha wazi nini cha kufanya ili kumaliza migogoro hiyo ya mara kwa mara.
Tutampata pia mtu atakayezungumza habari ya Morogoro kwa vile napo kuna migogoro mingi ya ardhi nataka leo tuzungumze kwa mapana kuhusu ardhi ya Morogoro kuna tatizo gani na tufanya nini siyo kulialia.
Wananchi wametuahidi, wametuamini, wametuchagua, wametuteua, wanatuheshimu na wanatupa mifugo yao ili tufanye kazi zao, sasa lazima tufanye kazi tusilalamike, alisema Lowassa.
Akizungumza kuhusu kutoa maoni mbele ya Tume ya Katiba Mpya iliyopo chini ya Jaji Joseph Warioba, Lowassa aliwataka Malaigwanani hao kuwa msatari wa mbele katika kutoa maoni yatakayokuwa na msaada kwao na kizazi cha baadaye cha wafugaji.
Alisema katika mchakato wa kutoa maoni unaoendelea hivi sasa Malaigwanani wanapaswa kuangalia wanatakiwa kufanya nini ili wawe kwenye Katiba na watambulike kama viongozi halali wa kimila.
MBUNGE WA Jimbo la Monduli, Edward Lowassa amesema kiongozi anayeaminiwa na wananchi wake hapaswi kuwa mtu wa kulialia na kuomba msaada badala yake anatakiwa kufikiri na kutoa uamuzi wa maisha ya watu wake. Lowassa ambaye pia ni Laigwanani Mkuu wa Wamaasai alisema hayo jana kwenye mkutano wa siku mbili uliowakutanisha Malaigwanani kutoka nchi nzima kujadili tatizo la ardhi, Katiba Mpya na suala la elimu kwa jamii hiyo.
Malaigwanani si viongozi wa kulialia, kuombaomba msaada ni watu wa kufikiri na kusema tumechoka na hali na sasa tunaamua kufanya jambo moja, mbili na tatu hatuwezi kuvumilia kuona watu wetu wakiendelea kuumia kila siku wakati sisi ndio viongozi wao, sisi siyo watu wa kulialia, alisema Lowassa na kuongeza:
Lazima leo tuseme kauli ya kuwasaidia wenzetu wa Ngorongoro hakuna kiongozi wa Kimasaai aliyeaminiwa kufanya kazi kisha akawa analialia na kuomba msaada. Ardhi kwa Ngorongoro imekuwa tatizo kubwa nataka leo hapa tulizungumze kwa dhati.
Tumechoka kusikia migogoro ya ardhi, leo naomba tusaidiane tuseme wenyewe hapa tufanye nini, alisema Lowassa.
Akieleza maeneo mengine yenye migogoro kwa wafugaji hao, Lowassa aliutaja Mkoa wa Morogoro na kuwataka viongozi wa kimila waliotoka mkoani humo kubainisha wazi nini cha kufanya ili kumaliza migogoro hiyo ya mara kwa mara.
Tutampata pia mtu atakayezungumza habari ya Morogoro kwa vile napo kuna migogoro mingi ya ardhi nataka leo tuzungumze kwa mapana kuhusu ardhi ya Morogoro kuna tatizo gani na tufanya nini siyo kulialia.
Wananchi wametuahidi, wametuamini, wametuchagua, wametuteua, wanatuheshimu na wanatupa mifugo yao ili tufanye kazi zao, sasa lazima tufanye kazi tusilalamike, alisema Lowassa.
Akizungumza kuhusu kutoa maoni mbele ya Tume ya Katiba Mpya iliyopo chini ya Jaji Joseph Warioba, Lowassa aliwataka Malaigwanani hao kuwa msatari wa mbele katika kutoa maoni yatakayokuwa na msaada kwao na kizazi cha baadaye cha wafugaji.
Alisema katika mchakato wa kutoa maoni unaoendelea hivi sasa Malaigwanani wanapaswa kuangalia wanatakiwa kufanya nini ili wawe kwenye Katiba na watambulike kama viongozi halali wa kimila.