Kiongozi chadema: Ziara ya dr.slaa kigoma,mwanza na tabora, ni woga wa mbowe na slaa.

Wisest man

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
993
332
Upepo wa kisiasa chadema si shwari baada ya maazimio yaliyofikiwa mwezi uliopita
na kamati kuu ya chama hicho ya kuamua kuwavua nafasi zote za uongozi zitto kabwe, na wenzake samson mwigamba pamoja na dr.kitila mkumbo kwa tuhuma za kukihujumu chama kwa kuandaa waraka wa siri unaohimiza kufanyika kwa mageuzi ktk uongozi wa juu chadema na kupewa siku 14 kujieleza ni kwani wazivuliwe kabisa uanachama, baada ya maamuzi hayo ndipo katibu mkuu wa chadema dr.wilbroad slaa kuanza kufanya ziara mikoa ya kigoma,mwanza,shinyanga na tabora kwa kile kinachojulikana kama ziara ya kuimarisha chama, lakini kinachonekana ni mbinu ya dr.slaa na mbowe kupima upepo wa mwanasiasa huyo kijana kama nguvu yake ktk kanda hiyo yanaweza kuathiri maamuzi ya kamati kuu kwani lengo la slaa na mbowe ni kumtimua kabisa zitto, lakini kutokana na matokeo ya ziara hyo inaonekana wazi kuwa hakuna wa kuweza kumfukuza zitto chadema, hii ni kwa mujibu wa taarifa niliyoipata kutoka kwa mmoja wa viongozi waandamizi kutoka makao makuu ya chadema DSM.
 
Kama ana nguvu amesaidia kupata viti vingapi vya ubunge wa CDM Kigoma? Yeye mwenyewe alishinda kwa asilimia ngapi??
 
Wajinga wanaweza kuwaza sawa na mtoa mada

Ni kweli, kwani hata mwanafalsa maarufu aliyeishi miaka 2000's iliyopita aliyeitwa Socrate licha ya kujulikana kuwa ni miongoni mwa watu wenye hekima kutoka na falsafa zake lakini bado yeye alijiona kuwa yeye ni mjinga kama uliyosema.
"I know that I know nothing"
"I'm the Wisest man alive for I know one thing, and that is that I know nothing".
By socrate.
 
huyu aliyeweka mada i.e., west man kweli ni mtu wa magharibi kimtazamo. hakika huyu si mwana chadema hata kwa matope. ni wale wale mamluki wanaopenda na kutafuta namna ya kumwokoa karecho zito msaliti, haini, mzito wa kuona mbali, mgonjwa wa sifa, mpofu wa uzalendo, aliyelaaniwa kama yuda iskarioti, mzee wa kulipuka, mjima wa madaraka, mpenda pesa, mwanachama wa ccm, na kadhalika na kadhalika. jiliwazeni. Mbowe na slaa wanawaumiza sana wanafiki wa mageuzi na wasaliti wa nyerere. MUNGU USIKAWIE KUWALAANI KIZAZI HICHO. WACHA WAPATE MIHELA lakini wafe kwa presha, kisukari, uzito, unene, uzembe, na magonjwa lukuki. pia wapigwe mawe na marungu.
 
Thibitisha kwa hoja hayo mawazo mfu.

Acha kujipindisha akili kwa kujitumainisha ujinga kwenye hoja mfu. Wewe unapoandika tambua wapi ulipo, upo uwanja wa vita au upo chumbani umejifungia huku ukisimulia yanayotokea eneo la vita. Mimi nipo Tabora na huyo unayezani kuwa ananguvu eneo hilo la kanda si kweli. Tena narudia si kweli! Acha umbumbumbu wa kufikirisha kichwa. Mtu si zaidi ya chama na wala chama hakipo ndani ya mtu ila mtu yupo ndani ya chama.
 
Upepo wa kisiasa chadema si shwari baada ya maazimio yaliyofikiwa mwezi uliopita
na kamati kuu ya chama hicho ya kuamua kuwavua nafasi zote za uongozi zitto kabwe, na wenzake samson mwigamba pamoja na dr.kitila mkumbo kwa tuhuma za kukihujumu chama kwa kuandaa waraka wa siri unaohimiza kufanyika kwa mageuzi ktk uongozi wa juu chadema na kupewa siku 14 kujieleza ni kwani wazivuliwe kabisa uanachama, baada ya maamuzi hayo ndipo katibu mkuu wa chadema dr.wilbroad slaa kuanza kufanya ziara mikoa ya kigoma,mwanza,shinyanga na tabora kwa kile kinachojulikana kama ziara ya kuimarisha chama, lakini kinachonekana ni mbinu ya dr.slaa na mbowe kupima upepo wa mwanasiasa huyo kijana kama nguvu yake ktk kanda hiyo yanaweza kuathiri maamuzi ya kamati kuu kwani lengo la slaa na mbowe ni kumtimua kabisa zitto, lakini kutokana na matokeo ya ziara hyo inaonekana wazi kuwa hakuna wa kuweza kumfukuza zitto chadema, hii ni kwa mujibu wa taarifa niliyoipata kutoka kwa mmoja wa viongozi waandamizi kutoka makao makuu ya chadema DSM.

Zitto kwa sasa ni sawa na SHIBUDA unaposema hawana uwezo wa kumtimua sijui unamaanisha nini?
 
Wewe mtoa mada zito kabwe siyo chadema,chadema ni taasisi hivyo hawezi kuipa hofu cdm wasifanye mikutano kwa ajili ya kujenga chama,zito kwenye jimbo lake ana madiwani wawili sasa umaarufu wake uko wapi.
 
Zitto hawezi kufukuzwa Chadema, na siku 14 zimeshapita tangu apokee barua rasmi tarehe 01.12.2013
 
Back
Top Bottom