Kiongozi anayeshutumiwa kufanya kampeni ya kujitenga jimbo la Nigeria akamatwa

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,010
9,875
Sunday Igboho amekuwa akifanya kampeni kwa ajili ya kuundwa kwa jimbo huru la Yoruba


Kiongozi wa anayepigania kujitenga kwa kabila la Yoruba Sunday Adeyemo, al maarufu kama Sunday Igboho, amekamatwa katika nchi jirani yaBenin, wiki kadhaa baada ya kutangazwa kuwa anasakwa kwa madai ya kukusanya silaha.

Bw Igboho alikamatwa na vikosi vya uslama katika uwanja wa ndege wa mji mkuu wa Benin -Cotonou, Jumatatu usiku.

Vyanzo vya habari vimeviambia vyombo vya habari kwamba alikuwa anaelekea nchini Ujerumani na sasa atarudishwa nchini Nigeria Jumanne.

Idara ya huduma za kitaifa nchini Nigeria awali ilisema kuwa inamtafuta Bw Igboho baada ya kukwepa uvamizi uliofanywa kwenye makazi yake kusini-mashariki mwa jimbo la Oyo.

Vikosi vya usalama nchini Nigeria bado havijatoa kauli yoyote juu ya kukamatwa kwake.

Vikosi vya usalama vilifanya uvamizi tarehe 1Julai katika makazi ya Bw Igboho, siku mbili baada ya mwanaharakatihuyo kuitisha maandamano dhidi ya serikali. Shirika hilo lilisema kuwa liligundua rundo la silaha kutoka kwenye nyumba ya Bw Igboho.

Bw Igboho amekuwa akifanya kampeni kwa ajili ya kuunda jimbo huru la Yoruba lililopo kusini-magharibi mwa Nigeria.

Kiongozi huyo anayetaka kujitenga amekuwa akishutumiwa kwa kuchochea ghasia dhidi ya wafugaji wa jamii ya Fulani katika majimbo ya kusini, madai ambayo anayakana.
 
Back
Top Bottom