Kinyago cha panya na dr. Slaa

ISOPOWER

Member
Sep 17, 2010
41
26
XXX majuzi alikuwa nyumbani kwao. Katika pita pita akakutana na Mmakonde mmoja aliyekuwa anauza vinyago. Alivutiwa sana na kinyago kimoja kilichokuwa kinafanana na panya. Kilichongwa kwa ustadi kiasi ya kwamba hata manyoya ungedhani ni yenyewe; wacha kichwa, miguu, mkia na vingine. Akamwuliza huyo Mmakonde anauzaje hicho kinyago. Akaambiwa ni shillingi mia tano na kikiiisha nunuliwa hakirudishwi. XXX akaona hiyo ni bei poa kwani ni kama bei ya soda. Alilipa mara moja akaondoka nacho.


Hajafika mbali, maajabu yakaanza kutokea. Kila aina ya panya wakaanza kujitokeza majumabani, vichakani, mashimoni na kwingineko wakimfuata XXX akaingiwa na woga na kuanza kukimbia. Lakini wapi. Panya waliongezeka na kuongeza kasi yao. Woga ulimzidi huku akijiuliza afanye nini.

Hapo alipokuwa ni karibu na mto. . Basi akakikimbia kuelekea huko na panya walikuwa bado wanamfuata na wakiongezeka. Kufika kwenye kingo za mto huo mkubwa, alikitupa kile kinyago majini na hapo ndipo maajabu yalipotokea. Wale panya wote waliokuwa wakimfuata, walikifuata kile kinyago huko majini, wakazama nakufa.

Kuona hayo,XXX ilikuwa ni kama amefunuliwa. Aliondoka kwa kasi mithiri ya farasi, akielekea kwa yule Mmakonde. Mara kufika Mmakonde akawa mkali.


“Nilichema uchirudishe”
“Tulia Baba. Una kinyago kinachofanana na Dr. Slaa.
“China. Tena nakwambia China kabisa”
XXX kesho yake alikata tiketi kwenda China.
HAIJULIKANI XXX ALIRUDI NA NINI KUTOKA CHINA
 
Mh!?Ina maana ccm hata wakilala ndoto zao ni dr slaa?Duh!?Kweli huyu jamaa kiboko yao.
XXX majuzi
alikuwa nyumbani kwao. Katika pita pita akakutana na Mmakonde mmoja
aliyekuwa anauza vinyago. Alivutiwa sana na kinyago kimoja kilichokuwa
kinafanana na panya. Kilichongwa kwa ustadi kiasi ya kwamba hata manyoya
ungedhani ni yenyewe; wacha kichwa, miguu, mkia na vingine. Akamwuliza
huyo Mmakonde anauzaje hicho kinyago. Akaambiwa ni shillingi mia tano na
kikiiisha nunuliwa hakirudishwi. XXX akaona hiyo ni bei poa kwani ni
kama bei ya soda. Alilipa mara moja akaondoka nacho.



Hajafika mbali, maajabu yakaanza kutokea. Kila aina
ya panya wakaanza kujitokeza majumabani, vichakani, mashimoni na
kwingineko wakimfuata XXX akaingiwa na woga na kuanza kukimbia. Lakini
wapi. Panya waliongezeka na kuongeza kasi yao. Woga ulimzidi huku
akijiuliza afanye nini.


Hapo alipokuwa ni karibu na mto. . Basi akakikimbia
kuelekea huko na panya walikuwa bado wanamfuata na wakiongezeka. Kufika
kwenye kingo za mto huo mkubwa, alikitupa kile kinyago majini na hapo
ndipo maajabu yalipotokea. Wale panya wote waliokuwa wakimfuata,
walikifuata kile kinyago huko majini, wakazama nakufa.


Kuona hayo,XXX ilikuwa ni kama amefunuliwa. Aliondoka
kwa kasi mithiri ya farasi, akielekea kwa yule Mmakonde. Mara kufika
Mmakonde akawa mkali.



“Nilichema uchirudishe”
“Tulia Baba. Una kinyago kinachofanana na Dr. Slaa.

“China. Tena nakwambia China kabisa”
XXX kesho yake alikata tiketi kwenda China.
HAIJULIKANI XXX ALIRUDI NA NINI KUTOKA CHINA
 
Hii hadithi yako inatufundisha nini mkuu?.....funguka!
 
wazee wa visa....tamaduni zao zinaruhusu visa visivyo vyenye sehemu zisizo unganika..yaani mwanzo na mwisho ni vitu tofauti visivo na kazi.

My last born wa 3 yrs anaweza leta kisa hata cha kutunga kilicho more logical than hiki.Nitamtuma aka mbrush huyu kilaza.Ndio lipumba anasikilizishwa na Ponda..?
 
Mkuu jamaa anamanisha Nchemba alienda china kutafuta kinyago cha kufanana na Dr Slaa ili na yeye awe na wafuasi wengi? Hii inamanisha hakumwelewa mmakonde alivyomwambia china, sasa katuletea balaa.

Nakushukuru wewe ndo umenifanya nielewe stori nzima. Akhasante mkuu
 
Ingawa unatumia kinga ya jukwaa la utani, kumbuka kwamba utani wa kisiasa hasa sasa hivi katika nchi yetu,unaweza kuleta chuki kubwa kwa baadhi ya kundi fulani. On the whole though, it is a nice joke!
 
Mkuu jamaa anamanisha Nchemba alienda china kutafuta kinyago cha kufanana na Dr Slaa ili na yeye awe na wafuasi wengi? Hii inamanisha hakumwelewa mmakonde alivyomwambia china, sasa katuletea balaa.

Tehe tehe tehe!

Nice creativity....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom