XXX majuzi alikuwa nyumbani kwao. Katika pita pita akakutana na Mmakonde mmoja aliyekuwa anauza vinyago. Alivutiwa sana na kinyago kimoja kilichokuwa kinafanana na panya. Kilichongwa kwa ustadi kiasi ya kwamba hata manyoya ungedhani ni yenyewe; wacha kichwa, miguu, mkia na vingine. Akamwuliza huyo Mmakonde anauzaje hicho kinyago. Akaambiwa ni shillingi mia tano na kikiiisha nunuliwa hakirudishwi. XXX akaona hiyo ni bei poa kwani ni kama bei ya soda. Alilipa mara moja akaondoka nacho.
Hajafika mbali, maajabu yakaanza kutokea. Kila aina ya panya wakaanza kujitokeza majumabani, vichakani, mashimoni na kwingineko wakimfuata XXX akaingiwa na woga na kuanza kukimbia. Lakini wapi. Panya waliongezeka na kuongeza kasi yao. Woga ulimzidi huku akijiuliza afanye nini.
Hapo alipokuwa ni karibu na mto. . Basi akakikimbia kuelekea huko na panya walikuwa bado wanamfuata na wakiongezeka. Kufika kwenye kingo za mto huo mkubwa, alikitupa kile kinyago majini na hapo ndipo maajabu yalipotokea. Wale panya wote waliokuwa wakimfuata, walikifuata kile kinyago huko majini, wakazama nakufa.
Kuona hayo,XXX ilikuwa ni kama amefunuliwa. Aliondoka kwa kasi mithiri ya farasi, akielekea kwa yule Mmakonde. Mara kufika Mmakonde akawa mkali.
Nilichema uchirudishe
Tulia Baba. Una kinyago kinachofanana na Dr. Slaa.
China. Tena nakwambia China kabisa
XXX kesho yake alikata tiketi kwenda China.
HAIJULIKANI XXX ALIRUDI NA NINI KUTOKA CHINA
Hajafika mbali, maajabu yakaanza kutokea. Kila aina ya panya wakaanza kujitokeza majumabani, vichakani, mashimoni na kwingineko wakimfuata XXX akaingiwa na woga na kuanza kukimbia. Lakini wapi. Panya waliongezeka na kuongeza kasi yao. Woga ulimzidi huku akijiuliza afanye nini.
Hapo alipokuwa ni karibu na mto. . Basi akakikimbia kuelekea huko na panya walikuwa bado wanamfuata na wakiongezeka. Kufika kwenye kingo za mto huo mkubwa, alikitupa kile kinyago majini na hapo ndipo maajabu yalipotokea. Wale panya wote waliokuwa wakimfuata, walikifuata kile kinyago huko majini, wakazama nakufa.
Kuona hayo,XXX ilikuwa ni kama amefunuliwa. Aliondoka kwa kasi mithiri ya farasi, akielekea kwa yule Mmakonde. Mara kufika Mmakonde akawa mkali.
Nilichema uchirudishe
Tulia Baba. Una kinyago kinachofanana na Dr. Slaa.
China. Tena nakwambia China kabisa
XXX kesho yake alikata tiketi kwenda China.
HAIJULIKANI XXX ALIRUDI NA NINI KUTOKA CHINA