Kinondoni kutawala nchi si sahihi

Netanyahu

Senior Member
Oct 2, 2008
147
22
Kuna mdau aliniletea taarifa za kutisha kuhusiana na wilaya ya kinondoni mkoani Dar es salaam.Akaniambia wagombea wote wa Uraisi wa vyama vyote vya siasa wana nyumba na makazi yao ya kudumu wilaya ya Kinondoni.Mawaziri na manaibu waziri karibu wote wana makazi yao na nyumba zao za kudumu wilaya ya kinondoni.

Asilimia zaidi ya tisini ya wabunge wote wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania wana nyumba na makazi ya kudumu wilaya ya kinondoni.Wanachofanya uchaguzi ukifika ni kujiondokea kwenye vijiwe vyao kwenye majumba yao ya fahari wilaya ya Kinondoni na kusambaa nchi nzima mawilayani kwenda kuwazuga wananchi huko kwenye mawilaya mikoani wawape kura wakaendelee kujilia vyao Kinondoni.

Hivi huko mawilayani kwenye majimbo ya uchaguzi hakuna wakazi wa kudumu waishio huko ambao maisha yao ya mwaka mzima huwa huko wawezao kuteuliwa kugombea huko

Hivi ni lazima mgombea awe mkazi wa kudumu wa kinondoni aliyejenga na kuishi kinondoni? Na hivi ni lazima wagombea wengi wanaoteuliwa kugombea ubunge na kupewa viti maalum vya ubunge ni lazima wawe wakazi waliojenga nyumba na wanaoishi kinondoni?

Makatibu wakuu wa mawizara nao ni hivyo hivyo kama huna nyumba na si mkazi wa kinondoniuwezekano wa kuteuliwa ni mdogo maana nao asilimia kubwa ni wakazi wa kudumu wenye nyumba kinondoni.

Hivi ni lini serikali itateua mawaziri wa kutoka wilayani ambao makazi yao na nyumba zao za kudumu ziko kule na mwaka mzima huishi kule kuwa mawaziri au manaibu mawaziri? Au tuseme wilaya ya kinondoni ndio kuna watawala na wabunge wazuri kuliko wilaya zote za Tanzania ndio maana inapewa nafasi kubwa? Hata wakuu wa mikoa asilimia zaidi ya tisini ni wakazi wenye nyumba na makazi ya kudumu wilaya ya kinondoni.Hivi kinondoni kuna siri au umamuluki gani

Ni lini vyama vya siasa vitapata wenyeviti wasio wakazi wenye nyumba na makazi wilaya ya kinondoni?

Bunge letu halina nguvu kubwa ya kukemea mafisadi sababu mafisadi ni wakazi wa wilaya ya kinondoni na wabunge wengi nao ni wakazi wa kinondoni na serikali kwa sehemu kubwa wenye nafasi nyeti wanatokea kinondoni basi hawatafunani maana masingasinga hawa wa kinondoni hufahamiana kwa vilemba ndio maana mifisadi inaendelea kutanua na hakuna wa kuigusa kwani ni timu yao ya kulewa pombe kinondoni

2010 inakaribia na tutaona tena wakazi wenye nyumba na makazi yao kinondoni wakiwemo akina Lowasa ,Rostam Azizi na wengineo wakikurupuka kutoka kinondoni kwenye mahekalu yao wakikurupuka kwenda kutafuta ubunge huko kwa waliolala wakazi wa kudumu kwenye mijimbo ya uchaguzi mawilayani huku wakilindwa na vyama vyao vilivyoapa kuhakikisha kinondoni ndio itaongoza kutoa wagombea ubunge na viongozi wan chi.

Anyway nadhani siasa za nchi zinatakiwa mabadiliko lakini mabadiliko yatakuwa ni magumu kama chi itaendelea kushikiliwa na wakazi wa kinondoni kuanzia bunge,serikali na majaji,majeshi yote.Sidhani hata kiusalama kama ni sahihi kulundika watu wengi kwenye nafasi nyingi za juu na nyeti ambao ni wakazi wa kudumu wa eneo moja.

Wadau naomba kutoa hoja kwenye bunge huria la Jamii Forum
 
hee nami nina nyumba kunduchi kumbe mi ni kiongozi!!!teh teh teh..
 
Analysis nzuri.

Kwa hiyo tusitegemee kuendelea, kwa sababu katikati manispaa ovyo kuliko zote ni Kinondoni na huko ndio viongozi wenu wanakotoka.

Haya bwana.
 
na ubaya ni huu, hata tukimteua mtu toka Tunduru awe katibu mkuu wa wizara yetu fulani akifika dar ana kaa kidogo Temeke kwa jamaa zake na baadae anahamia Kinondoni. Hata mbunge wetu amehamia kinondoni na kuacha nyumba yake Segerea.
 
Mkuu Nentanyahu (jina kali by the way) hapo umeshindilia msumari ndiiii,maana JK,Mzee wa Kiraracha Mrema, Freeman Mbowe, Lipumba ni kweli wote ni wakazi wa Kinondoni na wote wana ambition ya kukamata inji hii(of course JK ye tayari).
 
tatizo siyo kuwa wakazi wa kinondoni,tatizo baada ya kuwa viongozi wanafanya juhudi gani za kuendelezamaeneo mengine hasa ya maeneo yao wanakotoka?
 
Kinondoni bado ina maeneo mengi tu, na hujazuiwa kuishi huko pia! Ina maana wangekuwa wana makazi Temeke hata kama ni wabunge wa majimbo ya mikoani isingekuwa ishu kwako? Au pointi yako ni ipi hasa?
 
Ukweli ni kwamba hata mimi napendelea kinondoni only kwa sababu ya maandari yake nzuri, Kinondoni not environmentaly poluted compared to Ilala na Temeke!!! Nani anataka kufa kwa kansa za koo kwa mimoshi ya viwanda??? Hali ya Beach beach pia ni murua jamani, yaani ka upepo mwanana muafaka kabisa. Kinondoni hata watoto wangu wote watakuwa na makazi huko!!!!! Kama nina nyumba Ilala na temeke ni za biashara!!!!
 
ni kweli kabisa ila kuna haja ya kuwa na mikakati ya kupanua jiji kwa nje ya mji na sio Kinondoni
 
Utafiti uloufanya kuhusu watu kuishi Kinondoni sioni kama kuna tatizo kwani ni kati kati ya jiji.

Ukichunguza zaidi utagundua kuna maeneo mengine yanapendwa kama vile Kwa Komba,Kibaha Maili 1, Mafinga na kwingineko.

Cha muhimu wawatumikie wananchi wasibaki kuwakimbia na kwenda pindi kampeni zinapokaribia.
 
kwa kuwa ikulu haipo kinondoni basi waache wenyewe warundikane huko.........tunawakaribisha wilaya ya temeke kuna viwanja vingi tu na bei ndogo......
 
Mi nafikiri kuwa kama asilimia 60 ya viongozi wa juu wa nchi hii wanatoka wilaya kinondoni basi wilaya hiyo ilitakiwa kuwa mfano wa kuigwa kwa USAFI,USALAMA,MIUNDO MBINU YA BARABARA,MAJI TAKA NA SAFI, MAWASILIANO, NIDHAMU NA MENGINEYO lakini kinondoni ndio imekuwa inaongoza katika uchafu, wizi,utapeli hasa wa viwanja,ukahaba,zinaa, nk humo ndio viongozi wetu wanapoishi. mamlaka zilizopo zinawatukuza viongozi kiasi cha kwamba hawajui madudu na bugudha wanazozipata wananchi wa kawaida.
 
Mwingine akisema Wizara karibu zote, Ikulu maofisi makubwa yapo wilaya ya Ilala utasemaje?

Nchi nyingi huwa na residential district / section kwa viongozi e.g, Oysterbay (although I hear it is increasingly going to the dogs), ambako viongozi wengi pamoja na diplomatic corps hukaa, hivi utasema hizi districts ndizo zinatawala nchi?

Tukiendekeza hivi tutafikia kulalamika mpaka kusema kwa nini samaki wote wanapatikana majini.

Cha kufanya ni kuhakikisha standard of living ya sehemu zote inakuwa acceptable.Kwangu mimi swali si kwamba mbona viongozi wote wanakaa wilaya ya Kinondoni, swali ni kwa nini Wilaya ya Temeke haina huduma muhimu.

Kama alivyosema Jiwe, hii mentality ya kwa nini isituletee moyo wa kutaka kulogana -this is essentially what this is- bali tuwe na ambition ya ku achieve.

Muandishi amefanya causative link sehemu ambayo haipo, ameona kama kukaa Kinondoni ni requirement ya uongozi, wakati if anything, kukaa Kinondoni kunaweza kuwa ni matokeo ya uongozi.

Bottom line ambayo muandishi ame i squander, ni kwamba sehemu zote ziwe na miundombinu inayoruhusu maisha bora.
 
Netanyahu,
Kuna mdau aliniletea taarifa za kutisha kuhusiana na wilaya ya kinondoni mkoani Dar es salaam.Akaniambia wagombea wote wa Uraisi wa vyama vyote vya siasa wana nyumba na makazi yao ya kudumu wilaya ya Kinondoni.Mawaziri na manaibu waziri karibu wote wana makazi yao na nyumba zao za kudumu wilaya ya kinondoni.








  1. Unaweza thibitisha madai yako?
Asilimia zaidi ya tisini ya wabunge wote wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania wana nyumba na makazi ya kudumu wilaya ya kinondoni.Wanachofanya uchaguzi ukifika ni kujiondokea kwenye vijiwe vyao kwenye majumba yao ya fahari wilaya ya Kinondoni na kusambaa nchi nzima mawilayani kwenda kuwazuga wananchi huko kwenye mawilaya mikoani wawape kura wakaendelee kujilia vyao Kinondoni.







  1. Kinondoni ni wilaya kubwa kuliko zote Dar-es-Salaam
  2. Asilimia 60% ya wakazi wa Dar wako Kinondoni?(please correct me)
  • What is the fuss?
Hivi huko mawilayani kwenye majimbo ya uchaguzi hakuna wakazi wa kudumu waishio huko ambao maisha yao ya mwaka mzima huwa huko wawezao kuteuliwa kugombea huko








Kinondoni ni moja yapo ya wilaya, hivyo basi kama wilaya kuna majimbo ya uchaguzi, kama kwenye wilaya zingine,vilevile huko kwenye wilaya zingine naamini kuna wakazi wa kudumu kama wilaya yeyote Tanzania.
  • Sidhani kama kuna mkazi yeyote wa kudumu, ambae hawezi kuteuliwa kugombea sehemu yake ya makazi(wilayani, mkoania taifa au sehemu yeyote ile Tanzania)!
  • Hiyo hapo juu(nyekundu) Hizi ni siasa za chama? Chama gani?
Hivi ni lazima mgombea awe mkazi wa kudumu wa kinondoni aliyejenga na kuishi kinondoni? Na hivi ni lazima wagombea wengi wanaoteuliwa kugombea ubunge na kupewa viti maalum vya ubunge ni lazima wawe wakazi waliojenga nyumba na wanaoishi kinondoni?








  • Thibitisha tu, unayo hoja hapo?
Makatibu wakuu wa mawizara nao ni hivyo hivyo kama huna nyumba na si mkazi wa kinondoniuwezekano wa kuteuliwa ni mdogo maana nao asilimia kubwa ni wakazi wa kudumu wenye nyumba kinondoni.
Hivi ni lini serikali itateua mawaziri wa kutoka wilayani ambao makazi yao na nyumba zao za kudumu ziko kule na mwaka mzima huishi kule kuwa mawaziri au manaibu mawaziri? Au tuseme wilaya ya kinondoni ndio kuna watawala na wabunge wazuri kuliko wilaya zote za Tanzania ndio maana inapewa nafasi kubwa? Hata wakuu wa mikoa asilimia zaidi ya tisini ni wakazi wenye nyumba na makazi ya kudumu wilaya ya kinondoni.Hivi kinondoni kuna siri au umamuluki gani







  • Again, Thibitisha halafu soma Historia yako na Jiografia- hii yaweza kupanua mitazamo yako.
Ni lini vyama vya siasa vitapata wenyeviti wasio wakazi wenye nyumba na makazi wilaya ya kinondoni?







  • Una maana ya Kigoma:D:D
Bunge letu halina nguvu kubwa ya kukemea mafisadi sababu mafisadi ni wakazi wa wilaya ya kinondoni na wabunge wengi nao ni wakazi wa kinondoni na serikali kwa sehemu kubwa wenye nafasi nyeti wanatokea kinondoni basi hawatafunani maana masingasinga hawa wa kinondoni hufahamiana kwa vilemba ndio maana mifisadi inaendelea kutanua na hakuna wa kuigusa kwani ni timu yao ya kulewa pombe kinondoni

  • Ungekua kwenye NEC kule wewe ungekuwa ni msaliti kama sio haini!
2010 inakaribia na tutaona tena wakazi wenye nyumba na makazi yao kinondoni wakiwemo akina Lowasa ,Rostam Azizi na wengineo wakikurupuka kutoka kinondoni kwenye mahekalu yao wakikurupuka kwenda kutafuta ubunge huko kwa waliolala wakazi wa kudumu kwenye mijimbo ya uchaguzi mawilayani huku wakilindwa na vyama vyao vilivyoapa kuhakikisha kinondoni ndio itaongoza kutoa wagombea ubunge na viongozi wan chi.







  • Kuna umuhimu wa kuwaamsha hao waliolala(fanya mwenyewe)
  • Kuna Vyama vingapi?
Anyway nadhani siasa za nchi zinatakiwa mabadiliko lakini mabadiliko yatakuwa ni magumu kama chi itaendelea kushikiliwa na wakazi wa kinondoni kuanzia bunge,serikali na majaji,majeshi yote.Sidhani hata kiusalama kama ni sahihi kulundika watu wengi kwenye nafasi nyingi za juu na nyeti ambao ni wakazi wa kudumu wa eneo moja.








  • Sababu zako haziridhishi
  • Sidhani hii ni sahii kiusalama, kwani unataka kufanya utenganisho, kulundika wote wenye uwezo wa kuongoza na mafisadi pamoja huko kinondoni-ni hatari!
Wadau naomba kutoa hoja kwenye bunge huria la Jamii Forum


Karibu
 
Back
Top Bottom