Netanyahu
Senior Member
- Oct 2, 2008
- 147
- 22
Kuna mdau aliniletea taarifa za kutisha kuhusiana na wilaya ya kinondoni mkoani Dar es salaam.Akaniambia wagombea wote wa Uraisi wa vyama vyote vya siasa wana nyumba na makazi yao ya kudumu wilaya ya Kinondoni.Mawaziri na manaibu waziri karibu wote wana makazi yao na nyumba zao za kudumu wilaya ya kinondoni.
Asilimia zaidi ya tisini ya wabunge wote wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania wana nyumba na makazi ya kudumu wilaya ya kinondoni.Wanachofanya uchaguzi ukifika ni kujiondokea kwenye vijiwe vyao kwenye majumba yao ya fahari wilaya ya Kinondoni na kusambaa nchi nzima mawilayani kwenda kuwazuga wananchi huko kwenye mawilaya mikoani wawape kura wakaendelee kujilia vyao Kinondoni.
Hivi huko mawilayani kwenye majimbo ya uchaguzi hakuna wakazi wa kudumu waishio huko ambao maisha yao ya mwaka mzima huwa huko wawezao kuteuliwa kugombea huko
Hivi ni lazima mgombea awe mkazi wa kudumu wa kinondoni aliyejenga na kuishi kinondoni? Na hivi ni lazima wagombea wengi wanaoteuliwa kugombea ubunge na kupewa viti maalum vya ubunge ni lazima wawe wakazi waliojenga nyumba na wanaoishi kinondoni?
Makatibu wakuu wa mawizara nao ni hivyo hivyo kama huna nyumba na si mkazi wa kinondoniuwezekano wa kuteuliwa ni mdogo maana nao asilimia kubwa ni wakazi wa kudumu wenye nyumba kinondoni.
Hivi ni lini serikali itateua mawaziri wa kutoka wilayani ambao makazi yao na nyumba zao za kudumu ziko kule na mwaka mzima huishi kule kuwa mawaziri au manaibu mawaziri? Au tuseme wilaya ya kinondoni ndio kuna watawala na wabunge wazuri kuliko wilaya zote za Tanzania ndio maana inapewa nafasi kubwa? Hata wakuu wa mikoa asilimia zaidi ya tisini ni wakazi wenye nyumba na makazi ya kudumu wilaya ya kinondoni.Hivi kinondoni kuna siri au umamuluki gani
Ni lini vyama vya siasa vitapata wenyeviti wasio wakazi wenye nyumba na makazi wilaya ya kinondoni?
Bunge letu halina nguvu kubwa ya kukemea mafisadi sababu mafisadi ni wakazi wa wilaya ya kinondoni na wabunge wengi nao ni wakazi wa kinondoni na serikali kwa sehemu kubwa wenye nafasi nyeti wanatokea kinondoni basi hawatafunani maana masingasinga hawa wa kinondoni hufahamiana kwa vilemba ndio maana mifisadi inaendelea kutanua na hakuna wa kuigusa kwani ni timu yao ya kulewa pombe kinondoni
2010 inakaribia na tutaona tena wakazi wenye nyumba na makazi yao kinondoni wakiwemo akina Lowasa ,Rostam Azizi na wengineo wakikurupuka kutoka kinondoni kwenye mahekalu yao wakikurupuka kwenda kutafuta ubunge huko kwa waliolala wakazi wa kudumu kwenye mijimbo ya uchaguzi mawilayani huku wakilindwa na vyama vyao vilivyoapa kuhakikisha kinondoni ndio itaongoza kutoa wagombea ubunge na viongozi wan chi.
Anyway nadhani siasa za nchi zinatakiwa mabadiliko lakini mabadiliko yatakuwa ni magumu kama chi itaendelea kushikiliwa na wakazi wa kinondoni kuanzia bunge,serikali na majaji,majeshi yote.Sidhani hata kiusalama kama ni sahihi kulundika watu wengi kwenye nafasi nyingi za juu na nyeti ambao ni wakazi wa kudumu wa eneo moja.
Wadau naomba kutoa hoja kwenye bunge huria la Jamii Forum
Asilimia zaidi ya tisini ya wabunge wote wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania wana nyumba na makazi ya kudumu wilaya ya kinondoni.Wanachofanya uchaguzi ukifika ni kujiondokea kwenye vijiwe vyao kwenye majumba yao ya fahari wilaya ya Kinondoni na kusambaa nchi nzima mawilayani kwenda kuwazuga wananchi huko kwenye mawilaya mikoani wawape kura wakaendelee kujilia vyao Kinondoni.
Hivi huko mawilayani kwenye majimbo ya uchaguzi hakuna wakazi wa kudumu waishio huko ambao maisha yao ya mwaka mzima huwa huko wawezao kuteuliwa kugombea huko
Hivi ni lazima mgombea awe mkazi wa kudumu wa kinondoni aliyejenga na kuishi kinondoni? Na hivi ni lazima wagombea wengi wanaoteuliwa kugombea ubunge na kupewa viti maalum vya ubunge ni lazima wawe wakazi waliojenga nyumba na wanaoishi kinondoni?
Makatibu wakuu wa mawizara nao ni hivyo hivyo kama huna nyumba na si mkazi wa kinondoniuwezekano wa kuteuliwa ni mdogo maana nao asilimia kubwa ni wakazi wa kudumu wenye nyumba kinondoni.
Hivi ni lini serikali itateua mawaziri wa kutoka wilayani ambao makazi yao na nyumba zao za kudumu ziko kule na mwaka mzima huishi kule kuwa mawaziri au manaibu mawaziri? Au tuseme wilaya ya kinondoni ndio kuna watawala na wabunge wazuri kuliko wilaya zote za Tanzania ndio maana inapewa nafasi kubwa? Hata wakuu wa mikoa asilimia zaidi ya tisini ni wakazi wenye nyumba na makazi ya kudumu wilaya ya kinondoni.Hivi kinondoni kuna siri au umamuluki gani
Ni lini vyama vya siasa vitapata wenyeviti wasio wakazi wenye nyumba na makazi wilaya ya kinondoni?
Bunge letu halina nguvu kubwa ya kukemea mafisadi sababu mafisadi ni wakazi wa wilaya ya kinondoni na wabunge wengi nao ni wakazi wa kinondoni na serikali kwa sehemu kubwa wenye nafasi nyeti wanatokea kinondoni basi hawatafunani maana masingasinga hawa wa kinondoni hufahamiana kwa vilemba ndio maana mifisadi inaendelea kutanua na hakuna wa kuigusa kwani ni timu yao ya kulewa pombe kinondoni
2010 inakaribia na tutaona tena wakazi wenye nyumba na makazi yao kinondoni wakiwemo akina Lowasa ,Rostam Azizi na wengineo wakikurupuka kutoka kinondoni kwenye mahekalu yao wakikurupuka kwenda kutafuta ubunge huko kwa waliolala wakazi wa kudumu kwenye mijimbo ya uchaguzi mawilayani huku wakilindwa na vyama vyao vilivyoapa kuhakikisha kinondoni ndio itaongoza kutoa wagombea ubunge na viongozi wan chi.
Anyway nadhani siasa za nchi zinatakiwa mabadiliko lakini mabadiliko yatakuwa ni magumu kama chi itaendelea kushikiliwa na wakazi wa kinondoni kuanzia bunge,serikali na majaji,majeshi yote.Sidhani hata kiusalama kama ni sahihi kulundika watu wengi kwenye nafasi nyingi za juu na nyeti ambao ni wakazi wa kudumu wa eneo moja.
Wadau naomba kutoa hoja kwenye bunge huria la Jamii Forum