Kinondoni, Dar: Hamza mohammed, Polisi Watatu na mlinzi mmoja wauawa katika Majibizano ya Risasi

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,491
54,884
Guys I am informed there’s a guy shooting randomly near Stanbic Bank, anyone with more news?

Inadaiwa kuna watu wameuawa. Ni Karibu na Makao Makuu ya Stanbic.

========

Mtu mmoja ambaye alionekana kufyatua risasi karibu na Ubalozi wa Ufaransa Jijini Dar es Salaam amedhibitiwa na Vyombo vya Ulinzi na Usalama

Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, (IGP) Simon Sirro amethibitisha kuuawa kwa askari wawili kwenye mapambano ya kurushiana risasi yaliyotokea eneo la Daraja la Salenda jirani na Ubalozi wa Ufaransa, Dar es Salaam.

Tukio hilo limetokea leo Jumatano Agosti 25, 2021 baada ya mtu mmoja ambaye hajafahamika kuzua taharuki baada ya kufyatua hewani risasi huku akisikika akisema kuwa anawatafuta polisi.

Akizungumza katika kikao kazi cha maofisa wa polisi, Sirro amesema mtu huyo naye ameuawa kwa kupigwa risasi.

“Mmeziona clip zinaruka sasa hivi akaingia barabara kubwa akawa anatamba na SMG na yeye amepigwa risasi na askari wetu hivyo, askari wetu wamefariki na yeye amefariki” amesema IGP Sirro.

Ameeleza kuwa wanaendelea kufuatilia kufahamu mtu huyo ametokea wapi na baadaye watatoa taarifa kamili.

IGP Sirro amenukuliwa kupitia kipande cha video kilichorushwa kwenye mtandao wa kijamii wa Wasafi Fm.

PIA SOMA:
1. Mashuhuda wasimulia tukio la aliyekuwa akipiga risasi

UPDATE: Waliouawa ni Polisi Watatu na Mlinzi mmoja, wengine sita wajeruhiwa.
Jeshi la Polisi limesema idadi ya Watu waliouwawa na Mtu mwenye Bunduki aliekua akifyetua risasi ovyo karibu na Ubalozi wa Ufaransa Dar es salaam ni Watu wanne huku kati yao Watatu wakiwa ni Polisi na mmoja ni Mlinzi wa Kampuni binafsi ya ulinzi.

"Leo August 25 2021 tumekutwa na tukio baya kabisa, tukio la kihalifu ambalo limepoteza maisha ya Watu wanne na watatu kati yao ni Askari Polisi, limetokea katika makutano ya barabara ya Kenyatta na Kinondoni Askari wetu walikua kazini akatokea Mtu akawashambulia kwa Bastola na alipowashambulia na kuanguka alichukua Bunduki za Askari hao na kuanza kurusha risasi ovyo kuelekea Ubalozi wa Ufaransa"

"Ukiachia Watu wanne waliouwawa leo tuna Watu 6 ambao wamejeruhiwa kwenye tukio hili na wanaendelea na matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, taarifa zaidi tutaendelea kupeana kadri muda unavyokwenda, ni mapema sana kubaini kwanini alifanya vile lakini tumeshaanzisha Timu ya upelelezi na muda sio mrefu tutakamilisha"

"Kuhusu baadhi ya video kusema kwamba huyu Mtu ni Mkazi wa Upanga sisi hatuthibitishi mambo kupitia clips za video, tunathibitisha mambo kupitia upelelezi kwahiyo upelelezi ndio utakaoeleza, kuhusu swali la Waandishi kuhusu kuwepo kwa dalili zozote za ugaidi kwenye tukio la leo hatuwezi kusema chochote hii ni mapema lakini uchunguzi ndio utakaosema kama kuna ugaidi au hakuna ugaidi"

"Kwa sasa hatuwezi kusema amekutwa na kitu gani mfukoni, Polisi bado wapo eneo la tukio... ni mapema sana kusema amekutwa na nini kwasababu Wataalamu wapo kazini, kuhusu kama ni Raia kama sio Raia uchunguzi ndio utasema baada ya upelelezi kukamilika tunachojua sasa huyu ni Muhalifu"

UPDATES: Polis wafika Upanga katika nyumba aliyokuwa akiishi Hamza
kutoka Upanga Dar es Salaam kwenye nyumba aliyokua akiishi Hamza, Mwanaume aliyefyatua risasi na kuwauwa Watu wanne leo Jijini Dar es salaam ( Askari Polisi watatu na Mlinzi wa Kampuni binafsi mmoja).

Polisi wameifunga nyumba hiyo na kuondoka na Ndugu wa Hamza kwenda nao Polisi usiku huu ambapo walifika hapa toka saa kumi na moja jioni, endelea kukaa karibu na AyoTV na Youtube ya millardayo kufahamu zaidi.

olisi wameifunga nyumba aliyokua akiishi Mwanaume aliyefyatua risasi leo na kuuwa wanne Dar es salam, baada ya kuifunga nyumba hii iliyopo Upanga Dar es salaam wameondoka pia na Ndugu wa Mtu huyo aitwae Hamza kwenda nao Polisi usiku huu pamoja na Pikipiki aliyokua akiitumia.

Hamza amekua gumzo leo hii Dar es salaam baada ya kuwaua kwa risasi Watu wanne leo na kujeruhi wengine sita, endelea kukaa karibu na Youtube ya millardayo kufahamu zaidi.









Hii ni developing news…

Kuna mtu mmoja, kapigwa risasi na kuanguka katikati ya barabara


IMG_20210825_132011_040.jpg
Screenshot_20210825-132432.png

Huyu anadaiwa kauawa.
 
Back
Top Bottom