Kingunge Ngombale Mwiru: Nilitofautiana na kupata matatizo na viongozi wa kanisa Katoliki, Nikaacha kwenda Kanisani

Kipi heri? Kuamini kuwa Mungu yupo na kwamba huwapa thawabu watu wote wanaomwamini na kumwabudu AU Kuamini kuamini kinyume chake? Bwana Yesu kristo anatushauri : HERI KUAMINI MUNGU LAKINI BAADA YA KUFA USIMKUTE KULIKO KUTOAMINI HALAFU UKIFA UNAMKUTA! adhabu unayopata huko kwa KUTOAMINI kwako ni MBAYA SANA. Hatuhukumiani lakini pia Tusifarijiane bure. Tusiendekeze na kudanganywa na kiburi cha uzima pamoja na fahari ya Dunia hii inayopita. Sisi ni wasafiri na wapitaji tu hapa. Tusidangangwe na elimu tulizonazo. Elimu ya Dunia hii humjengea mwanadamu moyo wa kiburi. Mambo ya BWANA Mungu mtu huyajua kwa msaada wa Roho Mtakatifu. TUOKOKE wandugu ili tujazwe na Roho Mtakatifu kinyume chake ni vigumu sana kuurithi Ufalme wa BWANA Mungu ambao Bwana Yesu kristo ndiye haswa MFALME wa WAFALME na BWANA wa MABWANA!
 
Mkuu kwani wewe ni mtumishi wa Magu mpaka akukimbize mchakamchaka?
No mimi sio mtumishi wa Magu wala sio mtumishi wa mtu yoyote. Mimi ni miongoni mwa watu wanaitwa wapi dili, kwa kadri Magufuli anavyozidi kukaza, ndivyo wapiga dili tunavyozidi kubanwa na kukosa cha kufanya.

P.
 
No mimi sio mtumishi wa Magu wala sio mtumishi wa mtu yoyote. Mimi ni miongoni mwa watu wanaitwa wapi dili, kwa kadri Magufuli anavyozidi kukaza, ndivyo wapiga dili tunavyozidi kubanwa na kukosa cha kufanya.

P.
hahahahha
Pasco we mtu mkubwa bhana
 
Kingunge kwa akili hizi no wonder ndio maana waliiva pamoja na nyerere
 
siku hizi wanakimbilia kupata Phd lakin wanazidiwa na diploma za kina Mzee Mwinyi za 1940 kwa maarifa, busara na ujasiri na hekma!
Tatizo mfumo unaotumika kupata hizo degree au diploma ni mbovu Sana Ndio mana huwa sishangai Watu WA ngazi ya cheti wanakuwa bora kuliko hao wanaojiita wasomi WA juu.
 
YAFAHAMU BAADHI YA MANENO ALIYOWAHI KUSEMA MZEE KINGUNGE

_"Kwangu mimi kuwa “Mwanafikra huru” ni “evolving of ideas” — “zamadamu” ya mawazo._

_"Kwamba nilibatizwa Mkristo wa Roman Catholic na nilifuata hatua zote za utaratibu wa kanisa isipokuwa tu zile za kuwa Padri,_
_Ilikuwa ni wakati wa enzi za mkoloni, mkoloni Mwingereza, sikuwepo wakati wa mkoloni Mjerumani,"_
_"Nilivyozidi kukua nilijikuta najiuliza sana maswali mengi mengi…juu ya dini, dhehebu la RC, najiuliza toka darasa la kwanza mpaka la kumi…"_
_"Nilipochaguliwa kwenda sekondari Tabora, akili yangu juu ya kuendelea kujiuliza maswali makubwa ikapanuka…"_

"Niliendelea kujiuliza maswali ya msingi kuhusu dini, utatu mtakatifu…niliuliza sana na nilipata matatizo nilipokuwa nauliza maswali kuhusu masuala hayo…"_

"Nilijiuliza kuhusu imani yangu pia…_

_Nikaacha kwenda kanisani…"_

_"Lakini pia nilikuwa najiuliza kuhusu ukoloni…maana kwa wakati ule, “upande mmoja unakutawala, upande mwingine unakulazeni”_
_"Nilitofautiana na kupata matatizo na viongozi wa kanisa katoliki…"_
"Niliambiwa kuwa mimi ni “Mkomunisti” (tukio hilo nikiwa darasa la 6)_
_…ilitangazwa kabisa kanisani, nilitengwa (ex-communicated) kwa tangazo la Padri mmoja mzungu raia wa Switzerland kwa jina Padri Clement…"_
"Baba yangu alikwenda kumuona Askofu Edger Malanja ambaye alikuwa anafanya kazi na kuishi Kigurunyembe TTC Morogoro…_
"Askofu Edgar Malanja hakuwa na taarifa, hakujua kuwa tayari Padri Clement aliisha nitenga na kanisa (ex communicated..!)_ _"Ilitangazwa, ilisemwa kuwa mimi nilikuwa ni Mkomunisti, ingawa kwa wakati huo mimi mwenyewe sikujua “ukomunisti” ni nini.!_
_"Nilitangaziwa ubaya…kuwa mimi ni mtu muovu, Mkomunisti…ndivyo ilivyotangazwa…_
_"Mkakati wa ushawishi (Lobbying) ukafanywa kwa Mkuu wa shule ili nifukuzwe shule, yote haya yalifanywa na yule Padri Mzungu Mromani katoliki raia wa Switzerland..!_
"Mkuu wa shule hakukubaliana na ushawishi huo, hakuona kwanini mambo ya kanisani yaje kushawishi mambo ya elimu ya shuleni_
_"Zaidi pia ilikuwa kwamba, shule yetu ilikuwa muda mrefu haijatoa mwanafunzi kuendelelea zaidi na masomo ya juu…ikaonekana ikiwa mimi nitafukuzwa pengine hilo halitatokea kwani nilikuwa mwanafunzi ambaye darasani nilikuwa naendelea vizuri sana na masomo yangu, hivyo nilikuwa na uwezekano mkubwa kufaulu na kuendelea mbele zaidi…_
"Na kweli nilifaulu shule ya kati (middle school), na kutoka Dar es salaam nilipokuwa nasoma (ni pale ambapo sasa ni shule ya msingi ya Uhuru), nilikwenda shule ya sekondari ya *Tabora*._
_"Baada ya hapo nikajiunga na chama cha TANU kwa harakati zake za kutafuta UHURU…_
_"Ni katika kusoma vitabu ndipo nilipokutana na vitabu hivi vya Bw Thomas Paine: “The Age of reason”, “The rights of man” na “Common sense”…_ _"Nilipenda sana kusoma vitabu na nilisoma vingi…baadhi ya vitabu vilipigwa marufuku, lakini hata hivyo navyo nilikuwa mdadisi kutaka kuvipata na kuvisoma…_
_"Huyu Tom Paine alikuwa Mwana fikra huru (Freethinker)._"Tom Paine aliuliza kuhusu imani za kidini, kuhusu pia tawala za kifalme na kimalkia (monarchy), pia alitetea mapinduzi ya Ufaransa, na aliunga mkono vita vya wamarekani kuwa taifa huru, kutoka utawala wa Mwingereza…_
_"Maandishi ya huyu bwana (Thomas Paine) yalinipeleka hatua nyingine ya juu katika kuijua dunia na jamii_
_"Yalinipaisha upeo wangu wa kuhoji mpaka ikafikia hatua ambapo kwa mambo ya imani za dini nikaanza kuwa na mtazamo tofauti..!_
_"Nilijiuliza kuhusu imani yenyewe, kumbuka nilikuwa najiuliza toka enzi za shule, nilihoji imani ya Kikristo, halafu imani za dini kwa ujumla wake, imani ya maisha baada ya kifo- jee ni kweli kama dini zinavyodai..? hata hilo nilijiuliza pia_
_"Chama cha TANU kilinipeleka Liberia mwaka 1958 kwenda kusoma. Kwa wakati huo upeo wangu katika kuhoji na kudadisi ulikuwa wa juu sana…_
_"Tulikwenda Liberia watatu, kule tulikutana na Dr Gay. Tulifundishwa somo maalum, somo hilo ni FALSAFA (philosophy) yenyewe!_
"Sisi watatu tulikwenda Liberia tukiwa tumechelewa (wengine walikwisha anza). Kwanza tulipewa questionaires — maswali mengi kila mmoja kujibu, lengo likiwa ni kutaka kujua kiwango cha uelewa cha kila mmoja kimasomo na ki — imani (na pia kuchunguza kama kuna ushawishi wa siasa za mlango wa kushoto, ukommunisti)._
_"Ninajihesabia kuwa mtu wa bahati sana kusoma somo la FALSAFA (Mkongwe Kingunge alisema), kupitia kusoma Falsafa tulisoma vitabu vingi vya wana fikra wakubwa na mawazo yao; — Marx, Lenin nk._
_"Tulijifunza sana, Waalimu wetu wamarekani wakitaka kutusawishi tuone ya kuwa mfumo wa ukomunisti si mzuri hata kidogo..!_
_"Ndio…nakili falsafa ya wanafunzi wa kuhoji wa Hegel (Young Hegelians) ya kina Karl Mark ilinivutia,_
_"Yule mmoja nani yule aliyesema…“si kuwa Mungu kamuumba binadamu kwa mfano wake ila ni kuwa binadamu kamfikiria mungu kwa mawazo yake”…hiyo ilinifanya nielewe alaa kumbe Miungu imeumbwa na mawazo ya binadamu..!_
_"Huyo Ludwig Feuerbach, nilimsoma sana, nilisoma sana kitabu chake hicho…_
_Yeye (Ludwig Feuerbach) alinifanya mimi niwe Mwana fikra huru — Freethinker_ _"Ninaheshimu imani za dini lakini mimi sipo (sijaji identify na ) yoyote…_
_"Kwa imani za asili yetu, Wamatumbi wa Kilwa kusini Tanzania wanaamini na kuomba kwa “Mungu wa chini”, na “Mungu wa juu”…_
_"Kwangu mimi hulka hii ya kudadisi na kutafuta kutaka kujua inaendelea…siyo dogma (ng’ang’anizi), na wala si dini nyingine..!_
_" zangu “makomredi” wao ni wafuasi wa Marx…mimi ni “Marxian”, nakubaliana na kipengelele chake cha “Historical materialism” (mgongano wa nguvu za ukinzani — na za hoja pia) kama njia ya kuiangalia / kuichambua jamii.._
_"Waumini wa moja kwa moja wa falsafa ya Marx wao wanakataa uwepo wa Mungu kama vile wao wana ushaidi kwa hilo…itikadi yao inageuka kuwa _"Kuna wakati fulani Balozi wa Urusi ya zamani (USSR) alitutembelea pale chuo cha Kivukoni — Dar es salaam, badala ya kujibu kisayansi kwa kushuku (scepticism), yeye alijibu kama vile wao tayari wana ushaidi, alisema:- sisi Warusi tumekwenda kwenye sayari ya Mwezi (kupitia mwana sayansi wetu Yuri Gagarin ) na kule hakumkuta Mungu…jibu hilo lilinikasirisha kwani mimi nilikuwa ndiye ninayejulikana pale chuoni kuwa nilikuwa naishi bila imani ya dini yoyote…kweli hilo ndio jibu toshelezi..?
_"Mimi siamini lakini sina uhakika, (Agnostic)_
_"Ndio…“Living without religion” kuishi bila dini, maadili bila dini hayo ndiyo maisha yangu
_"mimi sina shida na hilo, mke wangu yeye ni Mkatoliki kabisaa kwa imani yake, hamna tatizo…_ _"Nilipozaliwa mimi, Kipatimu huko kilwa, wengi ni Waislamu._
_Nimekulia na kusoma Dar es salaam, Pwani, wenyeji ni Wazaramo na ni waislamu pia._
_Kwamba pengine kulikuwa na dalili za ubaguzi wowote wa kidini..? hapana_
_"Nilipokwenda Tabora sekondari (katikati ya Tanzania), kule wengi wakawa wakristo…_
"Sihitaji consolation (faraja) ya dini, kwani unafikiri watu wengi wanategemea makanisa au misikiti kwa hilo..?_
_"Sihitaji kumbadili mtu yoyote kwenye imani yake, kuishi kwangu bila dini ni msimamo wa kifalsafa_
_"Dhana ya uumbaji katika kitabu cha mwanzo (genesis) inakwendana na hadithi (myth) ya Waisraeli katika historia yao, na pengine ni sahihi kwao kwa dini yao inayokwendana na utamaduni wao.
 
Mungu hakumuumba binadamu kwa sura na mfano wake,bali binadamu ndio humfikiria Mungu kwa mfano na sura yake ya kibinadamu!!Yaani ni sawa na wale wanaosema siku ya kwanza ukiona sindano ina ukubwa wa mkonge wa Tembo,utajua sindano zote zipo hivyo.

Kusoma Falsafa ni raha sana.Hii ndio "Ajenda" ya Kanisa Katoliki na ndio maana licha ya "madudu" yake linaendelea "kutawala" ushawishi wa dunia,sababu waumini mnahubiriwa kifalsafa mpaka mnalegea.

Ili Padre wa Kanisa Katoliki apakwe mafuta,anaingia darasani kusoma Falsafa kwa miaka mitatu,yaani muda wote huo unasoma mawazo ya watu wanaosema "dini ni upuuzi",unasoma mawazo ya watu wanaosema "Hakuna Mungu",unasoma "African Philosophy" before the coming of Westerners.Unasoma kuwa shetani ni wewe na matendo yako na wala sio kiumbe muasi.

Utasoma kuwa kilichoandikwa kwenye Biblia ni mawazo ya Wanazuoni wa Kiisraeli,na utajifunza kuwa dini ni utamaduni na hivyo kilichopo katika biblia na utamaduni wa watu waliondikwa humo.

Baadae unaingia darasani miaka minne kusoma juu ya "Theolojia".Hapa sasa ndio unajifunza juu ya Mungu.Unawasoma wanatheolojia wabobezi kama kina Thomas Acquinas.Hapa unajifunza juu ya Mungu wa Wamisionari na namna ya kumtangaza.Hapa ndio unajua sasa Martin Luther aliamua kuachana na Wataliano akaanzisha "Lutheran Church-Church of Luther" na Mfalme wa Uingereza akaanzisha "Anglican Church-Anglo-British).Ili kuondoa dhana ya Mapapa wa Kiitaliano kupitia Roman Church-Rome Italy) kuitawala dunia kwa njia ya Papacy Authority.

Ukiyajua haya,utaona kuwa Kingunge yupo sahihi sana.Kwamba hizi dini ni "usanii" mtupu,kwani "Maadili bila dini" ndio msingi wa maisha.

Wamisionary wa Mwanzo kuingia Kilwa Kipatimo walifikia kwa kina Kingunge,na Kingunge alibatizwa kwenye lile kanisa Kongwe na Kilwa Kipatimo ambalo lilikuja kupata dhoruba wakati wa vita vya Majimaji.Alibatizwa na kumbukumbu za Kitabu cha Ubatizo kinaonyeshwa alibatizwa usiku wa Mkesha wa Pasaka na aliitwa "Ambrose"
eeh kwahivyo alibatizwa kabla ya vita vya maji maji??
 
Namnukuu
“Sina ugomvi na uwepo wa Mungu na hili siyo la kuhoji, isipokuwa ndani ya Biblia na vitabu vingine vinavyoitwa vitakatifu, yapo mambo yanayofikirisha na kujenga uwanja mpana wa kuhoji. Binadamu mkamilifu anapaswa kuhoji na kuwaza juu ya kile anachosoma, kuambiwa na hata kufanya na haya ndiyo yanatutofautisha na wanyama wengine,”
 
Namnukuu
“Sina ugomvi na uwepo wa Mungu na hili siyo la kuhoji, isipokuwa ndani ya Biblia na vitabu vingine vinavyoitwa vitakatifu, yapo mambo yanayofikirisha na kujenga uwanja mpana wa kuhoji. Binadamu mkamilifu anapaswa kuhoji na kuwaza juu ya kile anachosoma, kuambiwa na hata kufanya na haya ndiyo yanatutofautisha na wanyama wengine,”
Wapagani ...mlivyo ona amekufa kingunge...mnataka mjipritend kuwa eti alikuwa ndo kiongoz wenu hapa Tz....kiufupi ni kuwa kingunge atazikwa kidini. Na wala sio kipagani.
 
Asante kwa Makala hii na mahojiano haya. Viongozi wetu wengi, huondoka duniani bila kuacha maandishi yoyote. Mpaka sasa, mashuhuda wa Muungano wetu adhimu waliobaki hai ni wawili tuu, Balozi Job Luside na Hassan Nasor Moyo wa Zanzibar. Wakichomoka hawa, bila kuhojiwa kuhusu muungano na kuachwa maandishi, hakuna atakayeijua siri ya Muungano kati ya Nyerere na Karume.

Kwa sasa rais Mwinyi yu hai, Mkapa yu hai, Kikwete yu hai, natamani watokee waandishi mahiri, wafanye mahojiano ya kina na viongozi hawa kwa lengo la hifadhi ya historia kwa ajili ya Vizazi vijavyo.

Mpaka sasa, sijui ni waasisi wangapi wa Tanu bado wako hai?. Mawaziri wa baraza letu la kwanza la mawaziri, amebaki mmoja tuu, Job Lusinde. Sijui ni wangapi wa Baraza la Kwanza la Mapinduzi, wangalipo hai Zaidi ya Moyo.

Wazee hawa ni hazina adimu, kima chao chapita marijani!, tuwatafute, tuzungumze nao, tutunze kumbukumbu hizi adimu.

RIP Kingunge Ngombale Mwiru.

Paskali
Tatizo la hawa wazee wetu, au tuseme tatizo la mifumo yetu, hawawezi kuongea kwa uhuru na kwa ukweli kabisa kutoka moyoni. hawana uhuru wa kuongea kile walichoshuhudia. watasema kile ambacho utawala unapenda kusikia. sasa hapo unapata historia au propaganda? hiyo ni shida ambayo tunayo na tutaendelea kuwa nayo kwa muda mrefu sana. ukweli ni budi tufike mahali tuuthamini. wala nchi haiwezi kupinduliwa eti kwa kueleza ukweli wa Muungano. Muungano ni wa wananchi, siyo viongozi. hayo matatizo ni ya viongozi, na hayawahusu wananchi. tuambiwe ukweli maisha yaendelee. hali ya kusema ukweli ni ya kujengwa. haitatokea kama muujiza.
 
Mungu hakumuumba binadamu kwa sura na mfano wake,bali binadamu ndio humfikiria Mungu kwa mfano na sura yake ya kibinadamu!!Yaani ni sawa na wale wanaosema siku ya kwanza ukiona sindano ina ukubwa wa mkonge wa Tembo,utajua sindano zote zipo hivyo.

Kusoma Falsafa ni raha sana.Hii ndio "Ajenda" ya Kanisa Katoliki na ndio maana licha ya "madudu" yake linaendelea "kutawala" ushawishi wa dunia,sababu waumini mnahubiriwa kifalsafa mpaka mnalegea.

Ili Padre wa Kanisa Katoliki apakwe mafuta,anaingia darasani kusoma Falsafa kwa miaka mitatu,yaani muda wote huo unasoma mawazo ya watu wanaosema "dini ni upuuzi",unasoma mawazo ya watu wanaosema "Hakuna Mungu",unasoma "African Philosophy" before the coming of Westerners.Unasoma kuwa shetani ni wewe na matendo yako na wala sio kiumbe muasi.

Utasoma kuwa kilichoandikwa kwenye Biblia ni mawazo ya Wanazuoni wa Kiisraeli,na utajifunza kuwa dini ni utamaduni na hivyo kilichopo katika biblia na utamaduni wa watu waliondikwa humo.

Baadae unaingia darasani miaka minne kusoma juu ya "Theolojia".Hapa sasa ndio unajifunza juu ya Mungu.Unawasoma wanatheolojia wabobezi kama kina Thomas Acquinas.Hapa unajifunza juu ya Mungu wa Wamisionari na namna ya kumtangaza.Hapa ndio unajua sasa Martin Luther aliamua kuachana na Wataliano akaanzisha "Lutheran Church-Church of Luther" na Mfalme wa Uingereza akaanzisha "Anglican Church-Anglo-British).Ili kuondoa dhana ya Mapapa wa Kiitaliano kupitia Roman Church-Rome Italy) kuitawala dunia kwa njia ya Papacy Authority.

Ukiyajua haya,utaona kuwa Kingunge yupo sahihi sana.Kwamba hizi dini ni "usanii" mtupu,kwani "Maadili bila dini" ndio msingi wa maisha.

Wamisionary wa Mwanzo kuingia Kilwa Kipatimo walifikia kwa kina Kingunge,na Kingunge alibatizwa kwenye lile kanisa Kongwe na Kilwa Kipatimo ambalo lilikuja kupata dhoruba wakati wa vita vya Majimaji.Alibatizwa na kumbukumbu za Kitabu cha Ubatizo kinaonyeshwa alibatizwa usiku wa Mkesha wa Pasaka na aliitwa "Ambrose"
Mkuu Barafu una uhakika kwamba umemwelewa mzee Kingunge? yeye anasema kwamba "Kwangu mimi kuwa “Mwanafikra huru” ni “evolving of ideas” — “zamadamu” ya mawazo." Yaani Kingunge ameendelea ku-evolve mpaka akaamua kuikiri imani hiyo ambayo maisha yake yote alikuwa anaikana! kwa hiyo usiishie pale mwanzo alipokuwa anatafakari mawazo ya Ludwig Feuerbach aliyesema kwamba "si kuwa Mungu kamuumba binadamu kwa mfano wake ila ni kuwa binadamu kamfikiria mungu kwa mawazo yake" - Kingunge aliyatafakari na inaonekana aliyapenda kwa muda fulani, lakini baadaye aliyaweka kando.

Huu "usanii" wa dini unatoka wapi? ni kweli kwamba watu wanatumia dini kwa malengo tofauti, mfano ubaguzi wa rangi, ukoloni, lakini hii haibadilishi asili ya dini. mtu mmoja akitumia kisu kuchonga mpini wa jembe, mwingine akatumia kisu kumuua mwingine, hatuwezi kukilaumu kisu. tutamlaumu huyo mtumiaji.

Katika tafakari hizi kuhusu dini, huwa nashangaa kwamba watu wanaweza kusema "dini za kuja", kama vile ni jambo baya kujifunza anachofanya mwingine. lakini anayesema hayo anatumia kompyuta, kavaa suti, wala haoni kama hayo yote ni ya "kuja".

Swali moja ambalo wengi huwa hawajisumbui kulijibu, ni asili ya binadamu, na maajabu yanayomzunguka. mtafiti mmoja amejaribu kuunganisha mifumo yote ya kompyuta duniani katika internet, na akahitimisha kwamba utendaji wake unakaribia utendaji wa ubongo wa binadamu mmoja! binadamu amejiumba? ame-evolve? ameumbwa? hiyo kauli ya "binadamu kuumbwa kwa mfano wa Mungu" siyo kauli ya binadamu, kwa mujibu wa Biblia. ni kweli kaiandika binadamu, lakini kaipata wapi?

kuna kitu kinaitwa "Revelation", kwamba mawazo ambayo hayatokani na binadamu mwenyewe, bali anaangaziwa. huo ndio msingi wa imani. maana kama ni kwa mawazo tu ya binadamu, ni kweli huo utakuwa ni usanii.
 
Asante kwa Makala hii na mahojiano haya. Viongozi wetu wengi, huondoka duniani bila kuacha maandishi yoyote. Mpaka sasa, mashuhuda wa Muungano wetu adhimu waliobaki hai ni wawili tuu, Balozi Job Luside na Hassan Nasor Moyo wa Zanzibar. Wakichomoka hawa, bila kuhojiwa kuhusu muungano na kuachwa maandishi, hakuna atakayeijua siri ya Muungano kati ya Nyerere na Karume.

Kwa sasa rais Mwinyi yu hai, Mkapa yu hai, Kikwete yu hai, natamani watokee waandishi mahiri, wafanye mahojiano ya kina na viongozi hawa kwa lengo la hifadhi ya historia kwa ajili ya Vizazi vijavyo.

Mpaka sasa, sijui ni waasisi wangapi wa Tanu bado wako hai?. Mawaziri wa baraza letu la kwanza la mawaziri, amebaki mmoja tuu, Job Lusinde. Sijui ni wangapi wa Baraza la Kwanza la Mapinduzi, wangalipo hai Zaidi ya Moyo.

Wazee hawa ni hazina adimu, kima chao chapita marijani!, tuwatafute, tuzungumze nao, tutunze kumbukumbu hizi adimu.

RIP Kingunge Ngombale Mwiru.

Paskali
Tunakuomba utusaidie kwa hili la kuongea na Mzee Hassan Moyo.
 
Back
Top Bottom