jana niliongea na wanafunzi wachache wageni ambao wanatoka nje ya tanzania. niliongea kwanza na wanafunzi wa msc. badae nikaongea na wanafunzi wa bsc. wanafunzi wa msc walisema wao wanatamani sana kujuwa kiswahili ila wanafunzi wa kitanzania wanawaongelesha kingereza nikauliza mnafikili ni kwanini? wakasema wao waliambiwa na baadhi ya rafiki zao kuwa wanafunzi wa msc. wanapenda kutumia kingereza kwao kama sehemu ya mazoezi ya kuongelea kingereza na watu wengine wasio wanafunzi wakijuwa anaongea na mtu wa nje pia hutumia kingereza. akanijibu mfano hata wewe hapa unatumia kingereza tu, mie nikajibu mimi natumia kingereza kwakuwa nikitumia kiswahili mtaniuliza mambo mengi kuwa niwaelezee hamjanielewa, wakasema siyokweli. nikawahakikishia kuwa ukweli ndiyo huo. wanafunzi wa bsc wamesema wawapo kwenye mijadala wanafunzi wakibongo huwa wanasoma swali kwa kingeleza na kuendelea na maelezo ya kiswahili wakisema tutumie kingereza ili na wenzetu waelewe wanabaki kimya. hiyo inaashilia kunatatizo kubwa kwenye kingereza. na wanasema hata walimu wanachanganya sana wanapofundisha.ndugu zangu katika jf nawasilisha uchunguzi wangu nilioufanya jana.